Jamani tuache huu ushamba

fimboyaasali

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2011
Posts
8,617
Reaction score
8,244
Hii tabia ya watu wakipanda ndege wanajifanya wao ni wao, wanabadili lugha na kuongea kiingereza na kujifanya ni wataalamu wa ndege kwa kuelezea ndege inavyoruka, inavyokimbia na cha kumchukua za ni kuanza kuelezea jinsi walivyosafiri nchi mbalimbali duniani na kusifia viwanja vya ndege vya nchi hizo.

Ushamba mtupu, hebu tuache mambo haya!
 
Hongera kwa kupanda ndege. Na pole kwa kukaa siti pembeni ya mshamba mwenzio.

Vipi mlitua Chatle airport au Mwanza?
 
fimboyaasali hahaahha ngoja nicheke kwanza. Kwa mara ya kwanza nakuona umeweka thread hapa jukwaa la habari mchanganyiko. hahahahahaahaha
 
sipati picha ulivokuwa una muangalia uyo mshamba wako unatamani amalize story uangalie zako mawingu kwa kioo... teh teh
 
Hongera kwa kupanda ndege mkuu,unaelekea wapi?
 
Mimi sijawahi kupanda ndege kwa hiyo simo kwenye hilo kundi la washamba unaowazungumzia
 
Nami huwa najiukiza kwanini maskini huwa hapendi kusikia wengine wakielezea ukweli wa mafanikio yao?
Acha roho ya kimaskini
 
Kwa uzi huu mleta mada ndio mshamba.
 
Aisee umenikumbusha mara ya kwanza napita pale Zurich bado kidogo nichelewe kwa kushangashanga!
 
jitahidi nawe upande jamani
 
Tafsiri ya haraka haraka ya neno ushamba ni kwamba;
Ushamba ni ile hali ya kushangaa jambo ambalo wenzako wanaliona ni la kawaida tu! mleta mada tafakari,chukua hatua.
mekumiss hatuonani siku hizi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…