Jamani tuwe makini tunapotoa 'lift' za magari.

kwanza asante kwa kuushona moyo wangu....mpaka leo haujafumuka hata nyuzi moja.......
mambo mengine kuwa mpole bana
Preta banaa unajua upole mwingine unaweza ukasababisha mshtuko wa moyo lol anyway ngoja nisubirie mechi ya marudiano sijui itaisha 4-0 au 0-0 au 2-1 au 1-1
 
Hiyo inatokea hasa kwa wale wanawake wenye njaa wanajiuza. Ilitokea kwangu siku moja pale magomeni. Sikufunga milango wakaja jamaa wawili wananichekea nikafungua kioo kuniona wakasema ooh kumbe tulidhani ni fulani, ila si mbaya tunaomba lift mpala hapo Kigogo. Akili yangu haikufanya kazi fasta nikawambia ingieni. Pochi niliweka kiti cha nyuma nikasau kuiondoa. Bwana we walivyofika tu kwenye gari nikaona wanahangaika sana. Kucheki kwenye site mila naona mtu anafungua pochi yangu.

Dah! sijakaa sawa nikalock milango yote fasta, natafuta wapi niingie tuwachape ki-uzuri. baadae mmoja akasema ngoja tushuke hapa tusikusumbue, nikamwambia subiri hapa siyo sehemu nzuri ya kupaki, nilivyofika pale msikiti wa magomeni baada ya taa, nikaingia ndani mule, nikawaitia mwizi, eebwana walichapwa na wanachi wenye hasira, wakavuliwa nguo na hela zote walizokuwa nazo na wallet yangu wakarudisha. Niliwaacha mule wakipiga kwata la ijumaa.

ki ukweli kama mtu humjui, usijifanye msamalia mwema utakutoka puani.
 
Siyo uroho wa wanawake, bali aliomba msaada, kama binadamu akaamua kumsaidia. Tatizo ktk msafara wa mamba na kenge wamo. Just pray kwani pale ambapo hutaraji ndo yanatokea haya.

wengi wanatoa lifti kwa wanawake, mwanaume unaweza pitwa alafu hatua chache mbele akapewa mwanamke tena hata bila kuomba.
 
Mie hata mtu naemfahamu akisema nimshushe manzese nitamshusha tiptop tena mahali ambapo hakuna mtu
 
dah... mjini balaa... watu wanambinu za kutafuta pesa bana
 
Huyo Kaka yalomtokea aisee mstaarbu na pia pole zake, I think hata huo dada alisoma hio trait kwa mkaka. Na kuna dada wanatumika pia kuiba gari kwa kunyang'anya anakuambia nashuka sehem flani kumbe jamaa tayari wanamsubiri. Ogopa sana dada mwenye confidence ya kuomba lifti na humfahamu wala hakufaham otherwise muwe wawili!
 
Halafu utasikia watu wanalalamika eti wengine wanatupita na magari yao nao wamo ndani peke yao bila ya kutupa lifti.

Hii dunia imebadilika sana, ni heri ujifanye husikii tu. Hata wanafunzi wa shule nao wamekuwa wajanja. Zamani nilikuwa nawapa lifti mpaka mwenzetu mmoja ofisini alipochomolewa vitu vyake kwenye begi lake na hao hao wanafunzi.
 
kinacho waponzeni wanaume ni uroho na pupa zenu za kutaka kila mwanamke mrembo

Sidhani kama kila mwanaume anayetoa lifti hutoa kwa dhumuni hilo,ni kila mtu na tabia yake na sio wote.
 
Yani naye anasubiri mpaka watu wanamjalia kibao, ajaondoa gari tu...!?
Ningekuwa mimi, break ya kwanza Mbezi kama sio kwenda kumshusha Mlandizi.
 

Ushauli mzuri, kwani unapokuwa unamsaidia mtu, unakuwa na nia njema ila matatizo hutokea.
 
Yani naye anasubiri mpaka watu wanamjalia kibao, ajaondoa gari tu...!?
Ningekuwa mimi, break ya kwanza Mbezi kama sio kwenda kumshusha Mlandizi.[/uSIZE]



Ilikuwa ghafla na hakutaraji. Alishikwa na butwaa kiasi kwamba watu walipoanza kuzingira gari alipata hofu kutokana na mfadhaiko. Mdada anaongea kwa kujiamini utafikiri katoka naye nyumba ya wageni kikweli. Pale Manzese angekomaa naye angepoteza zaidi ya hiyo Tshs 10,000/=.
 

Mkuu,
UMENICHEKESHA SANA KTK HILI
 
Heri mimi natoa lift kwa ma sister wa katoliki tu.
 
Heri mimi natoa lift kwa ma sister wa katoliki tu.

Unaposema masista, unamaanisha wanaovaa vilemba vyeupe au? Hujaiona ya padre aliyeingia kwenye huo mtego?
 
mpelekee pole zangu!!!

mwambie siku nyingine aanze na Bwana asubuhi kbl hajatoka nyumbani.
 
mpelekee pole zangu!!!

mwambie siku nyingine aanze na Bwana asubuhi kbl hajatoka nyumbani.

Thanks, nitamwambia. Ila kumbe huruma inaponza sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…