kwa kifupi tu,kwa nini mtu anadanganya au anatoa taarifa isiyo sahihi?
ni faida gani mtu anayoipata anapotudanganya kuwa tcu wametoa majina ya vyuo tulivyochaguliwa?
ninaamini wote tuliopo humu ni waelevu,sasa kwa nini ulidhalilishe jukwaa hili?
tafadhali jamani naomba tuwe sahihi kwa kila taarifa tunayoitoa hapa,na ninaomba kwa yeyote anayetoa taarifa ya uongo kwa makusudu afungiwe
nawasilisha
kila mwaka huwa hivi. ya safari hii ilikuwa na ka ukweli kwa waliowahi maana hata ka page ka tcu na nembo yao kalionekana.
huenda tcu walikuwa kwenye test run jamaa akaidaka link. actually ilikuwa poa sana kabla hawajaishtukia.
wakija officially tcu waje na mpangilio huo katika utafutaji wa wapi mtu kapangiwa ni simple na mzuri - unajijazia index number yako, mwaka ulomaliza, jina la kwanza na la ukoo mashine ina search na kukupa data zote na hasa ya wapi unaenda kusomea na sio kuchukua degree!!!!