Dr Rutagwerera Sr
JF-Expert Member
- Dec 21, 2011
- 5,809
- 11,462
Ningependa kuandika hili juu ya wakati tulionao wa mwezi wa Ramadhan.
Nimegundua na kujionea sana wakati huu ndio wakati chakula kingi hupikwa majumbani na watu wakakichezea na kisha kukitupa. Nimealikwa, na hali kadhalika nimejionea kwa jamaa zangu pia namna chakula kingi kikipikwa na kuwashinda walaji.
Hoja yangu ni kwanini watu hupika vyakula vingi na mwisho vikawashinda na kuvitupa.?Binafsi naona moja ya faida ya kufunga wakati huu ni kula kiasi kwa lengo la kupata manufaa ya kiafya, kinyume ni kana kwamba kufunga ni adhabu. Unakuta familia ya watu wachache lakini inapikwa futari mithili ya shughuli ya watu wengi.
Tubadilike ndugu zanguni. Kuchezea chakula ni moja ya tabia mbaya sana. Na hili liende na kwa watu wengine wenye tabia kama hii.
Nimegundua na kujionea sana wakati huu ndio wakati chakula kingi hupikwa majumbani na watu wakakichezea na kisha kukitupa. Nimealikwa, na hali kadhalika nimejionea kwa jamaa zangu pia namna chakula kingi kikipikwa na kuwashinda walaji.
Hoja yangu ni kwanini watu hupika vyakula vingi na mwisho vikawashinda na kuvitupa.?Binafsi naona moja ya faida ya kufunga wakati huu ni kula kiasi kwa lengo la kupata manufaa ya kiafya, kinyume ni kana kwamba kufunga ni adhabu. Unakuta familia ya watu wachache lakini inapikwa futari mithili ya shughuli ya watu wengi.
Tubadilike ndugu zanguni. Kuchezea chakula ni moja ya tabia mbaya sana. Na hili liende na kwa watu wengine wenye tabia kama hii.