Uchaguzi 2020 Jambo wanalopaswa kufahamu CHADEMA, ni kwamba muda wa kufanya siasa za kistaarabu umekwisha

Uchaguzi ujao mtafanya peke yenu mshinde kwa 200% maana wapinzani waliposhiriki mlipata 100%.....
CCM sio kama haitaki upinzani No!,ni wapinzani ambao kwa sasa wanaitwa "wapingaji"ndio hawaitaki CCM, badala yakuja na sera mbadala na kuwauzia wananchi wao kila wakisimama jukwaani wao ajenda yao ni "tutaitoa CCM madarakani"na vijikashfa vya hapa napale.
 
Ushauri au maoni haya ya Mr.Mkiki ni dalili za WAZI kwamba sasa watu wamechoka.CCM sikio la kufa halisikii dawa.
 

Ni kweli ila ww umevuka kiwango cha heshima umehamia kwenye kujipendekeza na kuogopa hata kukosoa udhaifu wake kisa ni rais, na hata wale wanaothubutu kumkosoa, unawatafsiri kama wakosa nidhamu huki ukijificha kwenye rais kutukanwa as if ni jambo lilifanyika au linafanyika 24/7-365 a year.

Hii tabia ya kufumbia macho uovu eti kisa ni cheo cha rais inazigharimu tawala nyingi hasa nchi za kiafrika. Ndio maana unamtaja rais kwamba ni mtu mkubwa na sifa ya ukubwa ni hasi kwamba anaweza kukupoteza! Seriously hii ni sifa ya maana ya kutuonyesha uwezo wa rais? Kujipendekeza na kujitia upofu kwenye maovu sio jambo jema.
 
Ndo siasa ulitaka wasemeje hatutaki kuitoa ccm madarakani!!!?.....Ummalizapo adui ndio mwanzo wa adui mpya.....jipangeni kutafuta adui mpya miongoni mwenu...maana Sina hakika Kama Upinzani watakuja simamisha mgombea Tena....kwa katiba hii nasema Sina hakika.....
 
Point yangu hujaipata ndio maana ccm iwatawala milele.
 

Usitake kujitoa ufahamu kwa kubeba utetezi dhaifu. Usidhani watu wanaoshabikia upinzani ni wajinga kwamba wanafurahia tu ccm kutolewa madarakani. Kwanza lengo la chama chochote cha siasa ni kukamata dola. Na kwenye kukamata dola lazima watumie sera na mbinu mbalimbali na hilo sio kosa kwani ndio kanuni ya mchezo. Hapa unataka kuonyesha wapinzani wao wakipanda jukwaaani hawaongei chochote cha kuhusu wananchi bali ni kuitoa ccm tu madarakani.

Bunge lipo na hansard zipo, huko huwa wanatoa bajet zao kivuli na michango yao iliyovutia wananchi. Ccm ndio tunaishangaa haitaki kuachia madaraka kwa kisingizio cha kuleta maendeleo as if ni pesa toka mfuko wa ccm ndio zinazoleta maendeleo. Matokeo yake ndio hapo kura wanazidiwa wanatumia dola kulazimisha wao ndio waongoze. Sasa hivi watu hawataki kupiga kura kwakuwa haziheshimiwi, na sababu ni ccm kujitangaza bila ridhaa yao.
 
Kwaiyo

unataka wafanye Fujo na kuhatarisha amani ya nchi? Tutawadeal
Amani ndiyo kichaka chenu cha kufanyia maovu.
 
Point yangu hujaipata ndio maana ccm iwatawala milele.

Kutawala milele sio shida, unatawalaje hapo ndio issue. Hats rais Kamuzu Banda wa Malawi alijitangaza atakuwa rais wa milele wa Malawi aliweza? Mugabe naye aliamini atafia madarakani mpigie simu leo yuko ikulu ipi? Huu mtindo wa ccm kulazimisha kukaa madarakani, leo hii chini ya awamu ya tano nchi yetu kwenye jumuiya ya kimataifa tuko kundi moja na nchi kama Burundi, Rwanda, Uganda na Congo. Hii ni aibu kwa kipindi cha miaka chini ya mitatu nchi kuingia humo. Hapo kama hakuna tatizo kuna nini?
 
Sijawahi hata kuona japo kipeperushi tu cha ilani ya chama cha upinzani.
 
Sio wewe tu hata Jiwe anaamini hivyo....atatawala milele.
Ndivyo CCM wanavyoamini.Ndiyo maana mara wanapo ona wanatikiswa kisingizio chao ili wabaki madaraki ni "amani ya nchi".Lakini wapinzani kuuawa,kuchomwa visu,mapanga ,kupotezwa na kila aina ya mateso kwao haina maana yoyote.Wapinzani HAWASTAHILI AMANI YA NCHI WANAOIHUBIRI.

Halafu "Ati njooni kwangu ninyi nyote mnausumbuka na kulemewa na mizigo,nami nitawapumzisha".Huku ni kunajisi maandika Matakatifu.
Labda kama wanamwamini mungu wao na siyo Mungu MFALME WA AMANI anayeabudiwa na KUTUKUZWA NA WATU WEMA NA WATENDA HAKI.
 

Dhumuni Kuu la Chama chochote ni kushika Dola ili kitimize yale kinacho Ahidi ktk kampeni na kuongoza Nchi.Nikukumbushe tu Malaika Mkuu amesha sema ,nna nukuu Sehemu ya alicho wahi kukisema " CCM ita Tawala Milele".Na huyu tumuweke Kundi gani ?
 
Mkuu, umeangalia upande mmoja wa ccm bila kuangalia jinsi ndani ya cdm hakuna demokrasia[emoji12] ! Kama wanataka demokrasia ianzie ndani yao cdm. Charity begins at home.
 
Dhumuni la chama chochote kilichopo madarakani ni kung'ang'ania dola isichukuliwe na wapinzani.

Kama vile CCM inavyo vitumia Vyombo vya Dola na Taasisi zake kusalia Madarakani kupitia Katiba inayo toa Mwanya kwa Taasisi hizo kutumika kirahisi.
 
Ww kutokuona kitu hakumaanishi kitu hicho hakipo. Huu ni utetezi wa kijinga.

Achana nae huyo anae ulizia kipeperushi wakati CCM wamejaza Makabati yenye Ilani lkn utekelezaji wake ukawa Ziro..
 
Ww kutokuona kitu hakumaanishi kitu hicho hakipo. Huu ni utetezi wa kijinga.
Sijawahi kuwasikia chadema majukwaani wakiongelea sera mbadala zaidi ya kuishambulia ccm.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…