James Mbatia: Hakuna Chama kiranja wa vingine

James Mbatia: Hakuna Chama kiranja wa vingine

The Sheriff

JF-Expert Member
Joined
Oct 10, 2019
Posts
747
Reaction score
2,112
Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi, James Mbatia, amesema hakuna chama cha siasa ambacho ni kiranja kwa mwenzake, huku akivitaka vyama katika uchaguzi mkuu kushindana kwa hoja.

Sambamba na hilo, ameitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuhakikisha haki inatendeka kwenye uchaguzi huo kwa kusimamia sheria na kuwaondoa wale wote wanaotaka kuitia doa Tume hiyo.

Kauli hiyo aliitoa wakati akizungumza na watiania 113 wa nafasi za ubunge kupitia chama hicho Tanzania Bara. Alisema Chama hicho ni cha kuunganisha Taifa na sio cha mkoa mmoja na kabila moja, hivyo kwenye uchaguzi vyama vishindane kwa hoja za msingi na si kwa propaganda.

“Wale wanaosema NCCR kinataka kufungua NGO ni ndoto za alinacha sisi upole wetu sio dhaifu…Na sio vyama vingine vitake tufuate mbinu zao, hakuna chama ambacho ni kiranja wa mwenzake hapa hakipo,” alisema.

Mbatia aliongeza: “Mbona kuna watu wengi waliondoka NCCR hatukulalamika na tuliwatakia kila la kheri wengine sasa wamerudi kwenye asili yao imeibuka minong’ono, hapa ndio asili ya mageuzi ya nchi, uwezo huo tunao na twende kifua mbele kwa kujiamini na tunaweza.”

Mbatia alisema katika uchaguzi Tume ihakikishe haki sawa inatendeka katika kampeni na uchaguzi. “Kwenye kura tupigiwe kura sisi halafu tutulie tuseme sisi ni watu wa utu hiyo hapana, yaani nione Selasini amepigiwa kura Rombo ameshinda, haki yetu lazima tuitafute kwa gharama yoyote lakini gharama ya amani, maelewano, sheria na kuifanya Tanzania kuwa sehemu salama ya kuishi,” alisema.

Aliviomba vyama vingine kutambua kuwa mambo ya uchaguzi ni shirikishi na kuvumiliana kwa kuwa na fikra tofauti.

“Itikadi yetu ni kati ya itikadi bora duniani, sisi tutahubiri yaliyomema, Watanzania tunaomba wachague madiwani, wawakilishi, wabunge wa NCCR Mageuzi,” alisema.

Kadhalika, alisema chama hicho kinaamini haki ya mtu binafsi kugombea.

Alisema kwa kuchagua wabunge na madiwani wa chama hicho ana uhakika kilio chao cha kupata Katiba mpya kitasikilizwa.

Chanzo: IPP Media
 
Angalau sasa Tanzania itapata chama kikuu cha upinzani NCCR, kitakacho waunganisha Watanzania kama taifa na sio kuwagawa kama wa mtaa wa Ufipa.
 
The Sheriff,
Mh mbatia. October 2020 chama Cha hakutakuwa na mbunge hata mmoja bungeni.. hata wewe hutapata.ushsuri wangu kwako tafuta biashara au kazi nyingine ya kufanya a Hana na siasa kwa Sasa.
 
Mbatia acha kuwadanganya Watanzania. Unajua uchafu na dhuluma unayoifanya.

Unatumia pesa ya walipa kodi kuhonga watu wahame vyama lengo ni kudhoofisha upinzani. Iko hivi hakuna mwenye nia njema na wananchi wote ni wapiga deal. Si upinzani si watawala nia yenu ni moja 'mkwanja.
 
Inategemea ukubwa wa chama chako upoje, kukubalika kwa chama chako katika jamii, itikadi yako na chama rafiki ni wapi...

Sasa kama una urafiki na CCM, unataka CHADEMA pia wawe rafiki na wewe? hapana ikifikia hatua kama hii ni kupambana na hali yako tu hamna jinsi.
 
Mbatia Wewe ni nembo ya upinzani usituangushe, isimamie serkali kwa uzalendo wako usikubali kutumikia Mabeberu kama kile chama kipo Ufipa.
Hawezi akawaangusha inategemea na ukubwa wa dau, na muwe mnampatia chake kadri ya makubaliano.
 
Ni vyema Tanzania tupate chama cha Upinzani kiwe na sera nzuri sio tu kutukana na kupinga kilakitu ndani ya nchi wakati wowote. Hata kodi zetu zikitumika vizuri zikajenga barabara bado nikupinga tu.

Sasa hapo upinzani unapoteza dira.
 
Hapo kwenye "chama Cha mkoa mmoja na kabila moja"bila shaka ni chagadomo
 
Mbatia anafaa kwa Urais ni chaguo ma Mungu 2020.

jamaa huwa ana pointi, sio kama hawa wengine yaani ukiwauliza kwanini wanagombea wanasema kuitoa ccm madarakani hawana sera yaani wao kuitoa ccm madarakani ndo pointi yao
 
Back
Top Bottom