"jamhuri" tatu taifa moja.

Vujole

Member
Joined
Apr 3, 2013
Posts
33
Reaction score
22
Kwa uoni wa tume, tuwe na jamhuri tatu kumaliza fitna. Tumejiandaa kuziendesha kwa vyama tofauti? Mathalani Zanzibar - CUF, Tanganyika - CDM na Muungano - CCM
 
Serekali tatu ni mzigo napendekeza iwe mbili, kwani serekali huendeshwa kwa Lodi za wananchi.
 
jamani hivi maana ya selikari tatu ni kuwa na maraisi watatu?
 
Serekali tatu ni mzigo napendekeza iwe mbili, kwani serekali huendeshwa kwa Lodi za wananchi.

Hakuna haja ya kuwa na kitu kinaitwa muungano...what is needed ni economic cooperation au reginal integration au serikali moja tu. zanzibar iwe mkoa tu.
 
Maswali yangu ni haya?

1. Hivi hizi zinaweza kuongozwa na ilani tatu tofauti za uchaguzi kwa pamoja? maana huo uwezekano upo.


2. Serikali ya Muungano itapata wapi fedha za kuendesha Serikali yake pale ambapo let say upande mmoja utakapo amua kufuta ushuru wa bidhaa aidha kutokana na mikataba ya forodha ya regional bodies kama EAC, SADC, COMESA, EC ili kuruhusu ushindani wa soko wa bidhaa kati ya nchi hizo?

3. Kama Elimu haitokuwa ni jambo la muungano kama ilivyo sasa lakini angalau kuna namna fulani ya kushahabiana kwa sasa hivi,litakuwa Taifa gani moja kama haliunganishwi na mfumo mmoja wa Elimu? Maana kupitia elimu iliyoratibiwa kwa pamoja ndipo unaweza kujenga Taifa moja. Kuna watu watasema mbona hata sasa hivi kuna shule tofauti na systms tofauti lakini angalau kuna jitihada za kuhakikisha yale masomo maalumu yanafundishwa hata ikiwa kwa kichina, kiingereza au kiswahili.

4. Hivi lets say upande mmoja wa muungano utakapoimarika kiuchumi labda kutokana na kutokana na sera za ilani ya uchaguzi ya chama tofauti au kuwa na mangira mazuri ya kiuchumi ya kiasili hivi serikali hii ya muungano ya chama tofauti ambayo haisimamii mambo ya uchumi pande zote mbili itaweza kuleta uwiano wa kiuchumi au kuleta mpango mahsusi wa kunusuru upande mwingine wakati haina mamlaka ya mambo ya uchumi?
 
Hakuna haja ya kuwa na kitu kinaitwa muungano...what is needed ni economic cooperation au reginal integration au serikali moja tu. zanzibar iwe mkoa tu.

Eti wewe huna adabu
 
Tatizo la kuimba kama kasuku'. Sasa kama hoja ni gharama, the best option ni serikali moja. Kwa nini serikali mbili na sio moja? Najua utanijibu kuwa CCM wanataka serikali mbili, shame on you.
Serekali tatu ni mzigo napendekeza iwe mbili, kwani serekali huendeshwa kwa Lodi za wananchi.
 
Sidhani km znz wataweza kuchangia gharama serikali ya muungano maana bajeti yao tu ni ndogo kuliko ya mambo ya ndani bara
 
Kwa uoni wa tume, tuwe na jamhuri tatu kumaliza fitna. Tumejiandaa kuziendesha kwa vyama tofauti? Mathalani Zanzibar - CUF, Tanganyika - CDM na Muungano - CCM

Tanzania...... au nisema Tanganyika (Tanzania Bara) ni kataifa kasiko kuwa na mwelekeo. Siku zote ni kuganga majeraha badala ya kukwepa ajali. Mnauliza? Hakuna nchi iliyowahi kuwa na Jamhuri tatu ndani ya Jamhuri moja. Watu wazima wananuia kuangamiza nchi yao mchana kweupe kwa kuandaa vitu ambavyO duniani havipo kwa kutafuta kuwazunguka wenzao.

TUTAGANGA MAJERAHA NA KAWAIDA HUWA HATUULIZI YALITOKEA WAPI NA VIPI!
 
Sidhani km znz wataweza kuchangia gharama serikali ya muungano maana bajeti yao tu ni ndogo kuliko ya mambo ya ndani bara

Kwanini udhanii? wawaona wazanzibar hawana pesa? punguza dharau... mafuta wanayo au hujui? karafuu pia... Samaki wa Kupaa Watalii wa nje na wabara na vitu chungu mbavu....

Serikali tatu ni wanaotaka zaidi ni Zanzibar kwani wanaona kuwa wamemezwa na Bara... Karume alisema Hatujasoma lakini tumeelimika....
 
Sidhani km znz wataweza kuchangia gharama serikali ya muungano maana bajeti yao tu ni ndogo kuliko ya mambo ya ndani bara

Kwanza kuku mmekuwa wengi mno. Kukudume huitwa jogoo na kuna Jogoolashamba matandaoni. ZanzibaR wanajitetea wakati wanajua ukweli hata walipopewa KUTAWALA BARA WAKATI WA MZEE RUKHSA? Mbona Katibu Mkuu wa Wizarab ya Elimu Bara alikuwa Ali Vuai?

Si unafiki kuanza kutafuta nafuu ya kupungukiwa ili Bara waseme KARIBU TULE? Tabia ya Ngamia kuingiza kiwiliwili ndani ya hema la Bara mpaka leo ipo, unafiki wa nini? Kama kuna wanaoona heshima yenyewe si Wanzibar wangehamia kwao wote kwanza, lakini mpaka leo Mzee Rukhsa mwenyewe ana mpaka vijumba vya kupangisha anakwenda mitaani na mahakamani akikamata waliomwibia kodi za pango, si aibu hiyo.
 
Hebu tujielekeze kwenye mamlaka ya "jamhuri" hizi.

Anayegawa mikoa/wikaya ni rais wa "jamhuri" na kwa pendekezo lilivyo hakuna atakaye wazuia kuanzisha mikoa/wilaya mpya ambayo huenda yakawa ndio majimbo ya wabunge wa bunge kuu ambalo tumeambiwa jumla ya ni 75.

Fikiri pia sera za vyama kuhusu muundo wa kuendesha serikali. Mathalani, sera ya majimbo ya cdm Au cuf na sera ya uchumi wa kiliberali.
 
Eti wewe huna adabu

heheheheheh...vuai nahodha alikuwa hataki muungano huko nyuma...alipoletwa kuwa waziri huku bara ameonya asali yake, leo hataki serikali tatu anataka mbili ziendelee na muungano usivunjike.
 
  1. Jamhuri ya Muungano
  2. Jamburi ya Tanganyika
  3. Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
............why.......?
Hii ndiyo hoja hapa jamani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…