Sijali
JF-Expert Member
- Sep 30, 2010
- 2,672
- 1,814
Ninapoangalia yaliyowafanya vijana wa Uganda kuamua kujitolea muhanga kutaka mabadiliko, mengi ni yale yale yanayoendelea Tanzania: vijana kutokuwa na fursa, dhuluma ifanywayo na vyombo vya ulinzi, sheria kubanwa kwa uhuru wa kusema, uzuiaji wa mabadiliko ya siasa ya amani. ughali usiolezeka wa Maisha, Ufisadi na rushwa.
Lakini inakuwaje vijana wa Uganda wameyaona hayo na kuamua 'kuirudisha' nchi yao- na kabla yake WaKenya, Zambia nk; lakini jambo hilo linaonekana kuwa gumu Tanzania?
Nimekuja na nadharia:
Kwanza, ni ukweli lugha ya Kiswahili, hata kama naipenda, imetufanya tuwe 'docile'. Hii ni kwa vile lugha ni utamaduni. Utamaduni wa Mswahili ni 'kuvumilia' na kusema, 'hewalla yakhe'. Hilo limetuathiri kinafsia kwa kiasi kikubwa sana, na wala siyo eti uwepo wa amani.
Pili: Kutokana na 'kunyimwa' uelewa wa Kiingereza, tumejijengea kisiwa, kiasi ambacho uelewa nje ya kisiwa hicho ni wa watu wachache sana. Wengi hawajui hata yanayoendelea nchi jirani! Hii inafanya vigumu kwa watu wengi kuathirika na 'experiences' za wengine na kubakia kuimba wimbo mmoja tu!
Tatu: Tunatawaliwa na Chama cha watu 'smart sana' (in a bad sense) kwamba wanajua udhaifu wa Watanzania na wanajua vizuri kupima 'joto' lao. Kiasi kwamba kila joto linapopanda kupita kiasi wanalegeza kibano. Siyo kama ilivyokuwa vyama vya jirani zetu.
Lakini sababu kubwa Zaidi ni 'elimu'. Kwa kweli sasa naamini kuzoroteshwa kwa elimu Tanzania ni kwa kusudi kabisa. Mtu asiye elimu ni rahisi sana kumtawala kwani atakubali tu unayomwambia, kwa vile hajui kingine bora.
Mtu mjinga ni mwoga.
Lakini inakuwaje vijana wa Uganda wameyaona hayo na kuamua 'kuirudisha' nchi yao- na kabla yake WaKenya, Zambia nk; lakini jambo hilo linaonekana kuwa gumu Tanzania?
Nimekuja na nadharia:
Kwanza, ni ukweli lugha ya Kiswahili, hata kama naipenda, imetufanya tuwe 'docile'. Hii ni kwa vile lugha ni utamaduni. Utamaduni wa Mswahili ni 'kuvumilia' na kusema, 'hewalla yakhe'. Hilo limetuathiri kinafsia kwa kiasi kikubwa sana, na wala siyo eti uwepo wa amani.
Pili: Kutokana na 'kunyimwa' uelewa wa Kiingereza, tumejijengea kisiwa, kiasi ambacho uelewa nje ya kisiwa hicho ni wa watu wachache sana. Wengi hawajui hata yanayoendelea nchi jirani! Hii inafanya vigumu kwa watu wengi kuathirika na 'experiences' za wengine na kubakia kuimba wimbo mmoja tu!
Tatu: Tunatawaliwa na Chama cha watu 'smart sana' (in a bad sense) kwamba wanajua udhaifu wa Watanzania na wanajua vizuri kupima 'joto' lao. Kiasi kwamba kila joto linapopanda kupita kiasi wanalegeza kibano. Siyo kama ilivyokuwa vyama vya jirani zetu.
Lakini sababu kubwa Zaidi ni 'elimu'. Kwa kweli sasa naamini kuzoroteshwa kwa elimu Tanzania ni kwa kusudi kabisa. Mtu asiye elimu ni rahisi sana kumtawala kwani atakubali tu unayomwambia, kwa vile hajui kingine bora.
Mtu mjinga ni mwoga.