Jamii ilivyoshindwa kumsaidia Christopher Alex Masawe

Jamii ilivyoshindwa kumsaidia Christopher Alex Masawe

X_INTELLIGENCE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2014
Posts
10,400
Reaction score
14,339
"Nimekuita jamaa yangu kwani hali yangu kama unavyoiona. Rafiki zangu wote wamenikimbia, nimebaki na mama kama unavyoniona ila kumbuka nilikuwa mchezaji mkubwa, naomba jamii inisaidie.

Maisha yameenda kombo kwangu kwa sasa, nahitaji msaada kwani hapa wakati mwingine hata fedha ya kula mtihani. Nakubali kwamba nilikuwa 'supastaa' lakini kwa sasa mambo hayapo vizuri kama unavyomuona mama naye ni mtu wa kuhangaika, iambie jamii inisaidie. Katika maisha kila mtu anakosea, sawa, inawezekana nikawa nimekosea lakini siyo kiasi kikubwa hivyo. Besti andika na hili, vijana wanatakiwa wakumbuke kuna maisha baada ya soka, pia wakumbuke kuna nyumbani kwani maisha yanakwenda kasi.

IMG-20150222-WA0008.jpg

MAMA ALEX ALIMLILIA MWANAE

"Mwanangu mwenzio kama hali yake unavyoiona anahitaji msaada wa hali na mali ili aweze kurudi katika hali yake ya kawaida kwani kwa sasa anasumbuliwa na ugonjwa wa kifua kikuu ambao ulimuanza muda mrefu lakini hakuweza kupata matibabu. Iambie jamii imsaidie ili aweze kupata fedha za matibabu".

Nukuu ya kiungo wa zamani wa Simba, Christopher Alex Masawe pamoja na mama yake mzazi wakiiomba jamii imsaidie Alex pesa za matibabu siku chache kabla ya kifo chake alipokuwa akizungumza na mwandishi wa gazeti la Dimba, Ramadhan Hassan.

Marehemu Alex anakumbukwa kwa kupiga penati ya mwisho jijini Cairo, Misri wakati Simba ilipoivua ubingwa wa Afrika klabu ya Zamalek mwaka 2003.
 
Alipata dili la kucheza Supersport ya south africa tena bila majaribio akadengua jamaa walifanya kila jitihada kumchukua lkn akagoma matokeo yake jamaa wakambeba matola ambae tayari alikua kimeo...hii tabia ya kujuta baada ya mambo kwenda kombo tushaizoea sasa...any way R.I.P..kiungo mstaarabu uwanjani..
 
Alipata dili la kucheza Supersport ya south africa tena bila majaribio akadengua jamaa walifanya kila jitihada kumchukua lkn akagoma matokeo yake jamaa wakambeba matola ambae tayari alikua kimeo...hii tabia ya kujuta baada ya mambo kwenda kombo tushaizoea sasa...any way R.I.P..kiungo mstaarabu uwanjani..
pengine alilewa umaharufu...nadhani ndio maana kwenye maneno yake anaonekana kujutia kile alichokifanya....tutamkubuka kwa mengi mazuri alale mahala pema peponi.
 
RIP Massawe.
Pombe kupita kiasi na ngono zembe zimemgharimu.Alifikia hata kuchukua gari ya jeshi alipokua na rafiki yake mwanajeshi eti kaazima defender maramoja!kaenda kupiga mzinga huku akiwa amelewa
 
RIP Massawe.
Pombe kupita kiasi na ngono zembe zimemgharimu.Alifikia hata kuchukua gari ya jeshi alipokua na rafiki yake mwanajeshi eti kaazima defender maramoja!kaenda kupiga mzinga huku akiwa amelewa

Halafu baada ya zile ishu ndio akaacha soka..yaani kaacha soka wakati bado yupo juu kbs..wakati wakongwe kina machupa na shekhan wanapambana ughaibuni yeye alex eti amesusa kucheza soka yaani akaisusa kazi yake ..leo hii eti wanalaumiwa watu wamemtosa....
 
Apumzike kwa amani.
Lakini pia ametiachia funzo kubwa kwetu sisi,
tuishi tukijua hakuna aijuaye kesho yake.
Nidhamu na kujituma ndo msingi wa kesho yetu.
 
Sitawalaumu watu ila huyu ana baba na huyo baba ni tajiri mno, baba huyo hakumsaidia kabisa...sikujua sababu ila naamini itakua kulikua kuna ugomvi kati ya Carlos na chriss au Carlos na mama yake Chriss.
Ila Carlos ana roho ngumu mno
 
Sitawalaumu watu ila huyu ana baba na huyo baba ni tajiri mno, baba huyo hakumsaidia kabisa...sikujua sababu ila naamini itakua kulikua kuna ugomvi kati ya Carlos na chriss au Carlos na mama yake Chriss.
Ila Carlos ana roho ngumu mno
huyu jamaa alikua na baba yake mdogo hapo hapo dodoma naye pia anapesa nyingi tu lakini wala hakumsaidia
wadau wa dodoma wanasema inawezekana sababu ya huyo baba yake mdogo kutomsaidia ni kitendo chake cha kwenda simba wakati huyo baba yake mdogo ni mwanachama wa yanga
 
Sitawalaumu watu ila huyu ana baba na huyo baba ni tajiri mno, baba huyo hakumsaidia kabisa...sikujua sababu ila naamini itakua kulikua kuna ugomvi kati ya Carlos na chriss au Carlos na mama yake Chriss.
Ila Carlos ana roho ngumu mno

Carlos ni nani?
 
"Nimekuita jamaa yangu kwani hali yangu kama unavyoiona. Rafiki zangu wote wamenikimbia, nimebaki na mama kama unavyoniona ila kumbuka nilikuwa mchezaji mkubwa, naomba jamii inisaidie.

Maisha yameenda kombo kwangu kwa sasa, nahitaji msaada kwani hapa wakati mwingine hata fedha ya kula mtihani. Nakubali kwamba nilikuwa 'supastaa' lakini kwa sasa mambo hayapo vizuri kama unavyomuona mama naye ni mtu wa kuhangaika, iambie jamii inisaidie. Katika maisha kila mtu anakosea, sawa, inawezekana nikawa nimekosea lakini siyo kiasi kikubwa hivyo. Besti andika na hili, vijana wanatakiwa wakumbuke kuna maisha baada ya soka, pia wakumbuke kuna nyumbani kwani maisha yanakwenda kasi.

IMG-20150222-WA0008.jpg

MAMA ALEX ALIMLILIA MWANAE

"Mwanangu mwenzio kama hali yake unavyoiona anahitaji msaada wa hali na mali ili aweze kurudi katika hali yake ya kawaida kwani kwa sasa anasumbuliwa na ugonjwa wa kifua kikuu ambao ulimuanza muda mrefu lakini hakuweza kupata matibabu. Iambie jamii imsaidie ili aweze kupata fedha za matibabu".

Nukuu ya kiungo wa zamani wa Simba, Christopher Alex Masawe pamoja na mama yake mzazi wakiiomba jamii imsaidie Alex pesa za matibabu siku chache kabla ya kifo chake alipokuwa akizungumza na mwandishi wa gazeti la Dimba, Ramadhan Hassan.

Marehemu Alex anakumbukwa kwa kupiga penati ya mwisho jijini Cairo, Misri wakati Simba ilipoivua ubingwa wa Afrika klabu ya Zamalek mwaka 2003.
Oooh Too lat. Ila TB inatibiwa bure. |Sisi ni binadamu tunaweza kufanya makosa, aidha vijana wa sasa wajue kuwa soka la zamani lilikuwa halilipi kama la sasa hivi! , haina haja ya kumsimanga marehemu muacheni apumzike kwa Amani. May Alex's Soul Rest in Peace Amen.
 
Back
Top Bottom