Half american
JF-Expert Member
- Sep 21, 2018
- 38,283
- 97,793
Sio majungu nimejaribu tu kuwaza kwa maandishi 😂😂Wana JF mna majungu jaman😆😆🙌
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Sio majungu nimejaribu tu kuwaza kwa maandishi 😂😂Wana JF mna majungu jaman😆😆🙌
Sasa tuanze mipango ya sendoff....Nilishamsamehe dada
Tukipendana sie inatosha 😅Mie Leo ndio nitasutwa kabisaaa na mdogo wangu😆😆😆Ila kweli alidis Sana,Hadi nilimwambia asiseme hivyo Kuna watu wema na wabaya humu
Ngoja mwenyewe aje atupe utaratibu tusije ambiwa Kwan ni sisi tunao sendiwa off 😂Sasa tuanze mipango ya sendoff....
Yaani Mimi na wewe ni ndugu visheti🤣🤣🤣🤣ndio mawazo gani Sasa hayo?Sio majungu nimejaribu tu kuwaza kwa maandishi 😂😂
haha 😄 huyu demu ni pisi kali sana ila sasa si unajua Waimba kwaya?usirudi kutusumbua kwamba umeyachoka mapenzi
Dawa imekuingia Hadi mahali pake 😂😂huyu demu sijui ana kizizi😀
🤣🤣🤣🤣Vipi Unataka kupindua meza?huyu demu sijui ana kizizi😀
We ni ndugu yangu hata iweje, hata tuwe ndugu kashata fresh tu 😂Yaani Mimi na wewe ni ndugu visheti🤣🤣🤣🤣ndio mawazo gani Sasa hayo?
Sasa unafikiri mtu anavaa chupi ina picha ya msalaba si unaogop kwenda motoni😀🤣🤣🤣🤣Vipi Unataka kupindua meza?
Na hashindwi kutusumbua,na vile Leo tumejifanya wajuaji😆😆😆tungoje kwanzaNgoja mwenyewe aje atupe utaratibu tusije ambiwa Kwan ni sisi tunao sendiwa off 😂
Mvua zikiendelea kunyesh atalegeza kamba😀Dawa imekuingia Hadi mahali pake 😂😂
Sie damu damu👍👍❤️We ni ndugu yangu hata iweje, hata tuwe ndugu kashata fresh tu 😂
Nitaongezea sabuni za mo extraHongera bibie...ukijifungua useme nikuletee diapers nauza za jumla kutoka uturuki..
Wewe tayari ushaingia kwenye mfumo beki azikabiMvua zikiendelea kunyesh atalegeza kamba😀
Kyupi Inakukumbusha madhambi yako.Sasa unafikiri mtu anavaa chupi ina picha ya msalaba si unaogop kwenda motoni😀
msimbe bana!"Apataye mke apata kitu chema; Naye ajipatia kibali kwa Bwana."
MITHALI 18:22.
Wapendwa nilitaka nipotee kimya kimya, ila kwa namna hii ID yangu ilikaribishwa kwa upendo na kwa upendo nilionao kwa marafiki na ndugu zangu zangu niliojipatia hapa JF nimeona sio ubinadamu nikaitelekeza hii ID bila kuwaaga halafu niwaache wapendwa wangu wakijiukiza Clepatina kapatwa na nini mbona kapotea jukwaani.
Wapendwa, Mungu akitoa kibali November ninaolewa na mchumba niliyempatia hapa JF.[emoji1787][emoji3590].
Huyu jamaa hajanikuta single. Alinikuta nikiwa kwenye uhusiano na jamaa ambae hata hapa jukwaani nishawahi kumtaja kama Mgweno.
Kwa huyu mgweno ndiko moyo wangu uliko. Nilimpenda sio kwa moyo wangu wote bali kwa vyote vilivyotumika kuniumba. Nilimpenda sana huyu mwanaume kiasi cha kuwaona wanaume wengine wote walionitongoza kama wachumba tu[emoji1787].
Baadae nikagundua ninampenda Mgweno zaidi ya anavyonipenda na nikawa mtu wa kulalamika kila siku.
Hata hivyo Mgweno ndio aliyesababisha huyu shemeji yenu mpya atangaze ndoa fasta fasta.
Ni hivi,wakati nakutana na Mgweno nilikua na stress sanaa kiasi kwamba nilikua naonekana kama nina mara mbili ya umri wangu. Nilikua nimechoka sana. Nilikua kibibi[emoji1787] lakini mahaba na faraja alizonipa Mgweno zikarudisha peace of mind na stress zikaisha na Clepatina nikawa pisi kali tena[emoji1787].
Amini usiamini, mwanamke akipendwa na mwanaume anayempenda uzuri wake unarudi[emoji1787]. Ndio maana mtu ukiwa single hufatwi ila ukipata tu wa kukupenda utashangaa kila mwanaume anakutaka[emoji1787].
Sasa baada ya kuona Mgweno haeleweki/kabadilika nikapambania penzi haijasaidia, ndio kajitokeza huyu shemeji yenu mpya na japo hatuna muda mrefu na siwezi kusema namjua vizuri ila nafsini mwangu nahisi amani juu yake.
Kwa hatua alizochukua na gharama alizoingia juu yangu nina imani yuko serious katika kutaka kunioa.
Yeye na familia yake yote ni walokole kama mimi na ninajihisi salama kuwa mikononi mwa mwanaume amchae Mungu.
Ndugu zangu, mwanaume Mcha Mungu, msomi, mwenye ofisi zake kubwa kubwa, handsome, mpole ila mkali kwenye upuuzi, asiyependa wanawake wengi na mwenye mapenzi kama kapewa limbwata, hatoki kokote zaidi ya Mbinguni kwa baba Mungu, Mungu wa ishara na miujiza. Mgweno anisamehe ila naamini huyu ndie niliumbwa toka ubavuni mwake[emoji3590].
Hii itakua ni post yangu ya mwisho hapa. Kwa sasa najikita zaidi kusoma biblia kama alivyoniomba mume wangu mtarajiwa na pia kutumia free time yangu kujifunza kupika. Sijui kupika ndugu zangu[emoji24] na shemu wenu kasema kutojua kwangu kupika ni tatizo na mpaka siku ananioa niwe nimeshajua kupika.
Najua ndoa zina changamoto, najua mume wangu mtarajiwa atakuwa na madhaifu yake, najua kuna siku za kulia na siku za kucheka najua kuna siku tutapata na kuna siku tutakosa najua kuna mengi mazuri na mabaya yatajitokeza ila hata itokee nini kamwe sitafanya yafuatayo;
1) Sitamcheat hata akipoteza dushe yake.
2) Sitamdharau hata akikosa uwezo wa kunipa jero.
3) Kamwe sitajiona nina akili kumshinda.
4) Kamwe sitapaza sauti yangu ninapoongea nae.
5) Kamwe sitonyanyasa watoto wake ambao mama yao amefariki, kwani tayari nawapenda na wao wananipenda kama nimewazaa mimi.
Kwa mnaonipenda naombeni mniage kwa neno zuri la ushauri.
Joannah Half american Gily
I CAME, I SAW, I CONQUERED.