Jana ilikuwa siku ya Furaha kukutana na Graduate anachoma mahindi Barabarani

1m in 20 working days..
 
Fanya kila muhindi anapata profit ya 500 then kauza mahindi 30-50
30×500=15000
40×500=20000
50×500=25000
Hiyo si hela ndogo.
 
Ninapoishi kuna Mzee ana mashamba, amejenga nyumba bora kabisa na watoto wasoma chuo kikuu bila mkopo kwa biashara ya kuchoma mahindi..
Don't judge, naamini angekuwa na elimu angekuwa mbl zaidi.. Huyo wa it mpeni muda na nafasi
 
Natoa mfano hai kabisa.
Niliamua kuwa mjinga nikatafuta kijana ,akaanza kuuza supu.
Tulianza na mtaji tsh 25000. Kijana aliamka SAA 9 usiku akaenda kufuata nyama vingunguti 15000/=
Kuni 2000
Ndimu +pili pili 2000.
Tulipokata nyama tukatoa vipande 50,@ tukauza buku.
Faida nusu kwa nusu.
Baada ya siku tano dogo akaniambia br nafanya mwenyewe chukua mtaji wako. Nikakataa asubuhi take kasepa na hela kaanzisha kijiwe anapiga hela.
Nikamkuta akanipa hela yangu tukaachana.
Anasongesha maisha.
Endelra kudharau
Utatembea na bahasha mpaka ukome.
Elimu ikukomboe.
 
Nitapiga picha ya nyumba moja ya Mkulima aliyojenga kwa kuuza mboga za matembele halafu uniambie ,atakupangisha kwa kiasi gani.
 
Ahh siungi mkono hoja.. Huyo jamaaa chuoni alikua anacheza inamaana kutengeneza simu kashindwa sawa... Tutasema hana vifaa na kufanya PC maintainance pia kashindwa?...

Alafu mwisho... Inamaana kashindwa kutafuta pa kujitolea??

Sipingi kwamba jamaa anafanya kazi... ya mahindi.. Its okay lakini kama
Alitaka kufanya hiyo biashara angeanza mapema kulikuwa hakuna umuhimu wa kwenda chuo.. Kapoteza muda bure
 
IT ameshindwa kujiongeza hata akaanza kutengeneza simu?


Hata kutengeneza simu lazma uwe na mtaji ndo maana kaona achome mahindi ili anunue meza ya kuweka simu na makorokoro mengine. Asingeweza kukaa chini ya mti na kuweka simu kwenye magazeti wakati zikiingia vumbi ni habari nyingine.
 
Hivi mtu anaonekana wa maana pale anaposomea kufua nguo akaenda kuosha vyombo????
 
Hindi la wapi mkuu unalonunua sh 200 na kuuza 2000 acheni hesabu za abunuasi bwana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…