Jana nimeona jamaa anaibiwa catalys converter

Holly Star

JF-Expert Member
Joined
Aug 25, 2018
Posts
4,327
Reaction score
8,142
Gari yangu juzi nligongwa na boda shavu la mbele mkono wa kushoto baada ya mlango wa abiria mbele, nikapeleka jana garage ili wanirekebishie, sasa mm huwa siwaamini kabisa mafundi so huwa sitoki mpaka gari yangu iishe kurekebishwa.
Jamaa kaja na hariel mpya mbichi namba E nahisi aliingia sehem ya mwamba akatoboa tank ama kitu gani huko chini.
Kaja akawaelekeza mafundi akaondoka jamaa wamehangaika huchoma huko uvunguni mda kama nusu saa hivi mi nikaenda kuchoma chipsi jirani. Ile narudi nakuta jamaa ndo wanaziba kile kipande chenye sega jamaa hata hajarudi. Nimekaa nawaangalia wale jamaa jikaichukia ile gereji mazima
 
Sipendi binadamu wasio waaminifu kabisa, ningehakikisha anakuwa exposed na kuwajibika.

Sasa kuumiza wengine kwa short term gain inawasaidia nini? Upumbavu tu, halafu siku hizi kumejengeka katabia cha watu kutetea wizi as long ni mwengine anaibiwa, very insane.
 

Tupe location ya garage tusikanyage[emoji626]
 
Mwanza nata kuna vijana opp na ghorofa linalijengwa
Huwa wapo roadside hawana garage inayoeleweka kuna walio na mitungi ya ges miwili, hao jamaa sio watu wazuri kabisa
 
We mwanamke mbeya sana, taja jjna la gereji na mahala ilipo.
 
Nafikiri siku nitqkayo wakuta wana fanya huo ufezuli ktk ndinga yangu ndio siku iyo itakuwa mwanzo wa kipelekwa mahakaman mie ..maana sizan kama nita acha mtu salama bila Kipigo cha Mbwa koko
 
Umeshindwa nini kuwaambia na hata kumsubiri jamaa umwambie unkuja kutuambia humu huo umbea.
Angemsubiri jamaa amwambie pia ingekuwa kihelehele,
Umbea na kihelehele vyote sivipendi, Hapo ilitakiwa awambie hao mafundi warudishe walichochukua halafu akaushe bila kumwambia aliye ibiwa kama hakijatokea kitu, Kama hawezi bora angekaa tu kimya kuliko kuwa mbeya.
 
Post hii haimsaidii aliyeibiwa..
Ungechukua hatua hapo hapo...
Kwa kuwaeleza waache
 
Watazolewa kama mizoga maana ukiacha gari garage sasahivi kuja kuchukua chakwanza unaangalia makinikia, na siku hizi ukidakwa unakula kichapo sawa sawa utaje network yako , ukimaliza unalipa hela yakureplace na bado polisi ili utoke lazima ufunguke.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…