Jando ya kitaifa inaweza kuibua kizazi cha kizalendo nchini?

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2023
Posts
7,189
Reaction score
10,375
Kwa wasichana ni unyago, na kwa wavulana ni jando! Katika huu uzi, ,neno "jando" limetumika kama neno la jumla kwa wavulana na wasichana! Haya, twende sasa!

Kama umeshafika kwa Wakurya, Wamasai, Wamakonde, na makabila mengine yenye utaratibu wa kuwaingiza watoto wao ukubwani kwa njia ya tohara ambayo mara nyingi hufanyika bila ganzi, utakuwa unaelewa maana ya jando.

Mvulana akishaingia jando, huhesabiwa ni mtu mzima hata kama ni mdogo kiumri! Cha kufurahisha, hutarajiwa pia kubadilika kitabia kwa sababu sasa naye ni "mtu" mzima aliyefunzwa mambo ya utu uzima kwa mujibu wa jamii yao. Na kwa hakika, wengi wameonekana kuwa waaminifu sana kwa yale waliyofunzwa, na wengi walimudu kuyaishi hayo kabla ya Elimu waliyopewa jandoni haijafifishwa na Elimu nyingine toka vyanzo vingine!

Nasikia hata Israeli nayo ina utaratibu unaoweza kufanana na huo, ingawa sijui kama bado unaendelea kutekelezwa. Inasemekana, watoto wanapofikia umri wa miaka kumi na tatu, hupelekwa kwenye makambi ya pamoja na kuanza kufunzwa rasmi itikadi za Kiyahudi zitakazowafanya wajitambue Kiyahudi mahali popote watakakokuwa. Wengi ni mashahidi kuwa Wayahudi wengi, bila kujali uraia walio nao na nchi wanazoishi, wameendelea kuwa wazalendo kwa nchi yao ya asili nyakati za shida na raha, kwa uwaziri na kwa uficho.

Inawezekana ni mafunzo waliyopewa ndiyo yanayowasaidia kuwa hivyo?

Labda, na sisi tukiamua kuanzisha mfumo wa JANDO YA KITAIFA, ambapo watoto wamalizapo darasa la saba wanapelekwa kwenye makambi na kujengewa itikadi itakayowafanya kuwa wazalendo kwa nchi yao, hakutatusaidia kuibua kizazi cha kizalendo?

Ikiwa tutaweza kuwafunza watoto wajifunze kuliweka taifa mbele katika mazingira yoyote, hata kama itawafanya wakosane na wazazi wao, hatutaweza kuondoa tatizo la ufisadi huko mbeleni?

Ikiwa tutaweza kuwajengea watoto misimamo mikali katika kuipenda nchi yao, kama vile makundi ya kigaidi yanavyofanya kwa wafuasi wao kiasi cha kuwa tayari kuifia imani yao, hatutaifanya nchi yetu kuacha kuchezewa na wachache?

Kama mbinu tulizozizoea hazijafanikiwa kuinua kiwango cha uzalendo nchini, kwa nini tusijaribu mbinu ya jando ya kitaifa kwa maslahi mapana ya vizazi vijavyo?
 
Wajaluo na wahaya itakuwaje?
 
Tuanze na wale wa Msoga wa mwaka jana kama sikosei walitembelewa na Mstaafu au Prince, je wameleta matunda gani chanya kwenye jamii yao?
 

Tunayo matatizo makubwa:

1. Kule Lucas Mwashambwa, Tlaatlaah, johnthebaptist na timu nzima.

2. Huku usishangae hapo mmojawapo kuwa Fortila, Fundi Nchundo, binti kisiwi, Dritfer, au kina sisi wengine:



Safari bado!
 
Ukiwa kapuku Tz ndio uzalendo wenyewe Sasa.
Hulu wahubiri uzalendo Ni wezi wa kutupa na wa kuishi maisha ya Anasa.
 

Attachments

  • 20241219_172147.jpg
    120.3 KB · Views: 1
  • downloadfile-29.jpg
    100 KB · Views: 2
nawasubiri kwa hamu kubwa sana panzi na Manyumbu,

kwanza manichelewesha sana, mje kwa haraka nimalize kazi tukafanye mambo mengine gentleman πŸ’ πŸ’

Kwani mwamba naye amedhamiria kuniga kofia nyekundu?

 
Tunayo matatizo makubwa:

1. Kule Lucas Mwashambwa, Tlaatlaah, johnthebaptist na timu nzima.

2. Huku usishangae hapo mmojawapo kuwa Fortila, Fundi Nchundo, binti kisiwi, Dritfer, au kina sisi wengine:

View attachment 3196869

Safari bado!
nawasubiri kwa hamu kubwa sana panzi na Manyumbu,

kwanza manichelewesha sana, mje kwa haraka nimalize kazi tukafanye mambo mengine gentleman πŸ’
Kwani mwamba naye amedhamiria kuniga kofia nyekundu?

View attachment 3196918
 

Attachments

  • 20241219_172147.jpg
    120.3 KB · Views: 1
nawasubiri kwa hamu kubwa sana panzi na Manyumbu,

kwanza manichelewesha sana, mje kwa haraka nimalize kazi tukafanye mambo mengine gentleman πŸ’
Makijani yote ayafukie humo kabisaa,ila rangi zingine zisizikwe
 
Gentleman,
kwahiyo unataka kusemaje kuhusu huyo mnafiki wa baraza la maaskofu katoliki Tanzania kuelekea uchaguzi wa chadema ngazi ya Taifa?πŸ’
Ukiwa kapuku Tz ndio uzalendo wenyewe Sasa.
Hulu wahubiri uzalendo Ni wezi wa kutupa na wa kuishi maisha ya Anasa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…