Janga la pombe kali na anguko la kizazi: Kilio cha wazazi na hatari kwa Taifa

Wengine mnaishi Tanzania gani jamani, hao vijana wanaongamia na pombe hatuwaoni wengine, mnakuza tatzo tu, achen watu waburidike, pombe ipo miaka nenda miaka Rudi,
 
Pombe ni tatizo kweli kweli,hata juice nyingi. Za viwandani na energy si salama sana.ninafikiria ni wakati muafaka wa serikali kuweka sheria kuhusu utengenezaji wa vyakula na hata hizo pombe za kienyeji.fikiria Kuna mkoa watu wakisindika pombe za kienyeji wanaweka sabuni ya unga kama catalyst,na hizo zinamadhara kiafya.
 
Catalyst is any chemical substance used to alter the chemical reactions and remains unchanged.

Kwaresma Njema
 
Mimi nilikuwa mnywaji mkubwa wa pombe kali kwa miaka mingi hivyo najua ninachokiongea ni kitu gani.

Marafiki wanaendelea kuteseka kwa figo kuathiriwa na pombe, majuzi tumemzika mwingine. Alikuwa mlevi kupindukia.

Pombe ina sukari na sukari inaharibu ubongo, yapo madhara mengine mengi tu.
 
Na wengi wakilewa wanashikishwa ukuta so pombe na ushoga huwezi vitenganisha
 
mkuu leo umezungumza ukweli juu ya madhara ya pombe na huu ndio uwalisia wako kongole kwa hilo, nguvu hii itumike pia kufutilia mbali ile mada ya walevi na wanywa pombe kwani kwa namna moja au nyingine inawapa mshawasha vijana kuingia kwenye ulivi leo wa bia kesho visungura hadi gongo wakifikiri hayo ndio maisha. kwa sasa naona mada zako zimejikita katika ubunifu jambo ambalo ni zuri tofauti na ulozi na pombe hapo kabla hapo kwakweli umekaza buti meku...,ni kweli hatuwezi kuwanasua wote basi tuwabunguze kwani walevi(wapumbavu) hawawezi kuisha
 
Hali ni mbaya sana,muda mwingi tunalinda viongozi badala ya vizazi vijavyo,namshukuru mleta mada.Pombe kali zinaua vijana na kuwazeesha haraka,nguvu kazi imepungua mno.Ukikosea ukampa kibarua sh 5000 akatoka kidogo tu anarudi amelewa chakari.Usalama usiwe mambo ya Siasa na uongozi tu,hiki kizazi kinaangamia kwa ulevi nani ataoa watoto wenu na wato wetu!!?
 
"Usalama wa Taifa sio bunduki tu na askari wa kulinda mipaka"..

Hapo ndio matatizo yetu yanapoanzia na kuishi kizamani bila kujua mifumo sasa inahitaji watu wenye akili nyingi na maarifa mengi na kukiweka kila kitu under control.
 
Inawezekana unaishi maisha ya kipweke sana,ungeishi maisha ya kujichanganya ungegundua jinsi tatizo lilivyokubwa kongole kwa mtoa mada ameliona hili.
Katika mihangaikoyangu kwa hapa Tanzania nimelishuhudia hili tatizo kila nilikofika na kila niendako wanapombeyao kali iliyo maarufu kuna pombe kali za maziwa radha ya tangawizi,pipi kifua kahawa nk,kunasehemu nilifika watu wanaagiza cocktails za hizo radha kwa sh 2000!
e mnaishi Tanzania gani jamani, hao vijana wanaongamia na pombe hatuwaoni wengine, mnakuza tatzo tu, achen watu waburidike, pombe ipo miaka nenda miaka Rudi,
 
Nakumbuka double kick ilimuua bro angu mmoja hivi mtaani. Hivi visungura sijui vismat jin sio poa kabisa
 
Yaani mtu mzima na akili zake timamu anashindwa kulinda afya yake kwa kuepuka huo ulevi wa izo pombe kali mpka serikdli ingilie kati inasikitisha sana.

Kama umeshindwa kujione huruma mwenyewe unasubiri serekali zetu izi za kiafrica ikuhurumie niseme tu labda usubirie mauti tu hakuna jengine.
 
Kitoko, smart gin, Simba rock, ambiance
 
Sasa mkuu, bado ni uchaguzi wa mtu.

Na pombe hainywewi bila pesa, acha wachangie pato la taifa.

Hao wanaokata moto ni kua wanazidisha, na kama pombe imeruhusiwa nchini sio rahisi kumpangia mtu anywe kiasi gani.

Na hizi pombe za plastic ni matokeo ya kuzipiga marufuku zile pombe za karatasi.
 
Starehe ya muda mfupi, utafika wakati wa mateso ya afya kwa mnywaji.
 
Vijana wanapotea na kuangamia kabisa, pombe kali zipigwe marufuku.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…