Jangwani kunateketea sasa ni official Bangala na Djuma Shabani wanataka kuondoka rasmi

Jangwani kunateketea sasa ni official Bangala na Djuma Shabani wanataka kuondoka rasmi

Kwa ligi yetu iliopofikia mchezaji anaweza kudai hela ya usajiri miaka miwili? humu JF ni sawa na kijiweni kila mtu anakuja na habari ilimradi kuchangamsha genge
Ligi yetu?

Kwani hili swala ni la ligi au ni matatizo ya ndani ya uongozi wa Club?

Yanga Princess wamedai kuwa sio mshahara tu hadi signing fee hawajalipwa. Sasa hapo ligi inaingiaje?
 
Acha pateke
KIVUMBI NA JASHO: DJUMA, BANGALA
.
Djuma Shaban, Lomalisa Mutambala na kiraka Yannick Bangala juzi kwa nyakati tofauti wamegonga mlango wa kutaka kuondoka na kwenye vikao vyao kulihusisha majibizano makali.
.
Djuma na Bangala ndio walianza ambapo waliwasilisha ombi la kusitisha mwaka mmoja wa mkataba baada ya kutumikia mmoja kwa mafanikio Jangwani. Mikataba yao inaisha mwakani.
.
Habari za uhakika ni kuwa wawili hao awali walipewa nusu ya ada ya usajili na katika miezi ya karibuni wamekuwa wakifosi kumaliziwa bila mafanikio, hivyo Katika hoja zao ni kwamba kile kiasi walichopewa awali ni cha muda waliofanya kazi kwa hiyo wanachodai kitumike kusitisha mkataba sehemu iliyobaki jambo ambalo limeibua mjadala mzito ndani ya uongozi na hata kikao cha jana hakikufikia muafaka.
.
Mabosi wa Yanga wamepata uhakika kwamba wakishafanya uamuzi huo tu ndani ya siku mbili watani wao Simba na wapinzani wao Azam watashtua kwenye kurasa zao za mitandao ya kijamii kwamba “mgeni tumempata”. Simba na Azam zinashindana kimyakimya kusaka saini ya Bangala ambaye msimu mmoja uliopita alikuwa mchezaji bora wa ligi kwenda kuimarisha eneo la kiungo wa chini.View attachment 2660502
PATEKETee wanasema wanae GSM
 
Na ile ya Manara kuwa wenye akili ni wawili nayo hairuhusiwi kujumuishwa hapo juu?
Manara alisema akiwa Simba hivyo haina nguvu maana mpinzani anaweza kuongea chochote hata madai ya uwongo dhidi ya upande mwingine .

Kauli ya Rage inapaswa kuwekewa Lamination kabisa ...
 
Manara alisema akiwa Simba hivyo haina nguvu maana mpinzani anaweza kuongea chochote hata madai ya uwongo dhidi ya upande mwingine .

Kauli ya Rage inapaswa kuwekewa Lamination kabisa ...
Ilikuwa haina nguvu kipindi kile akiwa Simba.

Saizi ina nguvu kwasababu imeonesha dhahiri shahiri kuwa ni ukweli alichokiongea kupitia kitendo cha nyie kumpokea tena.
 
Ligi yetu?

Kwani hili swala ni la ligi au ni matatizo ya ndani ya uongozi wa Club?

Yanga Princess wamedai kuwa sio mshahara tu hadi signing fee hawajalipwa. Sasa hapo ligi inaingiaje?
Nna ongelea NBC premier League huko timu za wanawake hakuna timu haidaiwi labda JKT Queens
 
Nna ongelea NBC premier League huko timu za wanawake hakuna timu haidaiwi labda JKT Queens
Simba Queens uliona wapi ikidaiwa?

Mkataba wa 1B kwa mwaka walioingia na M-Bet kwa hadhi yao unatosha kulipa kila kitu na machenchi yanabaki.
 
KIVUMBI NA JASHO: DJUMA, BANGALA
.
Djuma Shaban, Lomalisa Mutambala na kiraka Yannick Bangala juzi kwa nyakati tofauti wamegonga mlango wa kutaka kuondoka na kwenye vikao vyao kulihusisha majibizano makali.
.
Djuma na Bangala ndio walianza ambapo waliwasilisha ombi la kusitisha mwaka mmoja wa mkataba baada ya kutumikia mmoja kwa mafanikio Jangwani. Mikataba yao inaisha mwakani.
.
Habari za uhakika ni kuwa wawili hao awali walipewa nusu ya ada ya usajili na katika miezi ya karibuni wamekuwa wakifosi kumaliziwa bila mafanikio, hivyo Katika hoja zao ni kwamba kile kiasi walichopewa awali ni cha muda waliofanya kazi kwa hiyo wanachodai kitumike kusitisha mkataba sehemu iliyobaki jambo ambalo limeibua mjadala mzito ndani ya uongozi na hata kikao cha jana hakikufikia muafaka.
.
Mabosi wa Yanga wamepata uhakika kwamba wakishafanya uamuzi huo tu ndani ya siku mbili watani wao Simba na wapinzani wao Azam watashtua kwenye kurasa zao za mitandao ya kijamii kwamba “mgeni tumempata”. Simba na Azam zinashindana kimyakimya kusaka saini ya Bangala ambaye msimu mmoja uliopita alikuwa mchezaji bora wa ligi kwenda kuimarisha eneo la kiungo wa chini.View attachment 2660502
Kama wanadai haki yao, viongozi wangewalipa mapema iwezekanavyo. Haya mambo ya madeni/madai huwa yanashusha sana morali ya wachezaji.

Mimi nilifikiri labda waliamua tu kuomba kuondoka, ili kwenda kutafuta changamoto mpya! Kumbe wanadai fedha zao za usajili!! Viongozi wa Yanga waache uswahili.
 
Ilikuwa haina nguvu kipindi kile akiwa Simba.

Saizi ina nguvu kwasababu imeonesha dhahiri shahiri kuwa ni ukweli alichokiongea kupitia kitendo cha nyie kumpokea tena.
Kwa hiyo timu ikamsajilli mchezaji aliyewahi kuwafunga wanakuwa hawana akili ?
 
Back
Top Bottom