January Makamba, Nape Nnauye na Mwigulu Nchemba, kama mna ndoto za kuja kuwa Marais kwenye Nchi hii basi futeni hizo ndoto

January Makamba, Nape Nnauye na Mwigulu Nchemba, kama mna ndoto za kuja kuwa Marais kwenye Nchi hii basi futeni hizo ndoto

Ndivyo system ya sasa inavyofanya kazi ni ama ulambe asali ufunge mdomo au upambane na dola
Wanaliwa na system zao za kibwege plus roho za kimaskini kwenda shule na kurudi wezi.😂
 
Vijana mmeaminiwa na Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania kwa kupewa uwaziri lakini mnachokifanya kwenye wizara zenu ni madudu tu. Hamjaonesha kuwa mko competent kuweza kugombea nafasi ya Urais hapo mbeleni.

i.
Wafute ndoto zao kwa wananchi gani,hawa hawa wanaofanya uongozi kuwa mabishano ya Simba na Yanga ?
 
Hakuna uzalendo kwa hao vijana ukiangalia hapo mwanzo tulikuwa na imani nao lkn hakuna kitu ni stomach sorrounder km wengine tu na wametokea familia nzuri wakati nchi nyingine unabaki kujenga nchi ulishaiba vya kitosha lkn wetu hapa ndio kwanza mpk mizizi wanachimba ila ipo siku
Kabisa. Hata wakiongea jambo huoni kama wapo upande wa Wananchi wapo upande wa kujijali wao tu.
 
Ukiona hawafukuzwi maana yake ni utendaji wao unamridhisha aliyewateua
utendaji sio utendaji - wao wanamridhisha aliyewaweka! limits zinazingatiwa na kuwa bendera fwata upepo enough to impress their boss!
 
Wakiamua kugombea urais hakuna mtz yyte WA kuzuia Hilo. Sio wewe sio Mimi Tanzania kama Kuna mwanasiasa umpendi dawa ni moja tu. KUMOMBEA AFE KIFO CHA GHAFLA vinginevyo tutabaki kufarijiana tu JF
 
Kwani inahitaji rocket science kulitambua hili?
Hela za uchaguzi ujao zinakusanywa kwa sababu hatuna vyanzo vingine vya mapato
Hakuna bidhaa za kuuza nje kutuingizia dollars na pesa za kigeni na uchaguzi uko kwenye kona tu
 
Wakiamua kugombea urais hakuna mtz yyte WA kuzuia Hilo. Sio wewe sio Mimi Tanzania kama Kuna mwanasiasa umpendi dawa ni moja tu. KUMOMBEA AFE KIFO CHA GHAFLA vinginevyo tutabaki kufarijiana tu JF
Katiba Mpya itakapatikana muda si mrefu kwa hiyo hiyo ndoto yao ife
 
Katika Jambo Magufuli alijatibu kufanya lenye manufaa ni kuondoa mizizi yote ya wanajiona kama Icon katika Nchi-bahati mbaya baada ya kufariki wamerudi wale wale.
 
Katika Jambo Magufuli alijatibu kufanya lenye manufaa ni kuondoa mizizi yote ya wanajiona kama Icon katika Nchi-bahati mbaya baada ya kufariki wamerudi wale wale.
Kabisa mkuu. Yaani wamekosa maarifa ya uongozi hawa watu. Wao wanapewa vifurushi kupitia kodi zetu, kodi zetu ndizo zinafanya wafanye maamuzi ya hovyo.
 
Vijana mmeaminiwa na Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania kwa kupewa uwaziri lakini mnachokifanya kwenye wizara zenu ni madudu tu. Hamjaonesha kuwa mko competent kuweza kugombea nafasi ya Urais hapo mbeleni.

Mwigulu Nchemba umeshindwa kubuni vyanzo vipya vya kodi badala yake umeweka tozo kubwa na Wananchi ndiyo wanaoumia.

Nape Nnauye umeshindwa kudhibiti mitandao ya simu inajipandishia tu gharama za vifurushi. Hebu fikiria ndani ya mwaka huu mitandao ya simu imebadilisha vifurushi na kupandisha gharama za vifurushi zaidi ya mara tatu mfululizo.

Mwaka jana tu, tumenunua vifurushi GB 1 kwa TZS 1000 na 1500, lakini tangu tuanze mwaka huu mpaka sasa hivi vifurushi TZS 3000. Hivi kweli umeshindwa kudhibiti mitandao ya simu isiwe inapandisha gharama kiholela pasipo utaratibu maalumu? Watu wengi siku hizi wanafanya biashara kwa kutumia mtandao wa intaneti, sasa mnapopandisha gharama kiholela hamuoni kama mnazidi kuongeza ukali wa maisha kwa Wananchi?

January Makamba umeshindwa kutafuta majibu ya nishati hapa Nchini. Kila siku umeme unakatika na kuwa wa mgao. Sababu mnazotoa ni kuwa maji machache. Hivi kweli sisi tunategemea maji pekee kuzalisha umeme? Hivi sisi si tuna gesi nyingi tu? Hivi sisi si tuna maeneo mengi yenye upepo wa kutosha? Hivi sisi si tuna makaa ya mawe mengi tu? Kama ni ndiyo hizo sababu za visingizio zinatoka wapi?

Mbona kipindi cha Magufuli umeme ulikuwa haukatikati kila siku kama sasa hivi? Kuna hujuma mnafanya nyie. Huwezi kutoka waziri na kutoa sababu ya kwamba umeme ni wa mgao kwa sababu ya upungufu wa maji wakati tuna njia nyingi za kupata umeme.

Linakuja suala la maji. Hivi kweli sisi ni wa kuwa na mgao wa maji wakati tumezungukwa na maji kila kona? Hapa Dar ES Salaam tumezungukwa na bahari, lakini mmeshindwa kutengeneza mifumo bora ya kupata maji?

Mpaka sasa ni dhahiri kwamba CCM imeshindwa kwa kila kitu. Haiwezekani kama CCM ipo, inaruhusu mambo ya hovyo kama haya yaendelee kutokea.

CCM na nyie vijana niliowataja hapo juu tutawahukumu hapo mbeleni kwa uzembe mnaoendelea kuonesha sasa hivi kwenye uongozi wenu.

Mwendo huu mnao enda nao, endeleeni kwenda nao mpaka mwaka 2025. Natoka mimi.
Hawa uliowataja, ninadhani sisi raia kuwataja kila mara na bila ya Rais kuwaondoa kwa madhaifu yao ya wazi, anawaunga mkono.

Na katika baraza lao la mawaziri, mwenyekiti akiwa ndiye Rais, maovu yote wanayotutendea bila ya kumumunya maneno, yana baraka zake.

Haiwezekeani lijitokeze ombwe la kutisha la uongozi kwa kipindi kifupi hiki cha uongozi wake akae kimya bila kutia neno, ni ngumu sana!

Magufuli aliwaondoa kwa aibu kwa sababu aliona hawafai, Rais wa sasa muda huo yeye akiwa naibu na mshauri mkuu!

Alivyowarejesha kwa kubadili gia angani tukadhani anawafuta machozi ya pole ya kuondolewa kwao kwa uonevu, kumbe walipokea "sakramenti" inayowahusu na hawakustahili msamaha wa "kabila" hiyo.

Asipowapumzisha na akiendelea kuwakumbatia kama vifaranga, wanamharibia sana tena wazi wazi utawala wake huu ambao watu waliuchukulia kama wenye kuleta matumaini.

Jamani, ama ni mbinu ya kumchafua huyu Rais ili nchi isitawalike wao wakamate uongozi?

Maana tukumbuke kuwa, wote hao walichukua fomu za kugombea urais '15 nadhani wana ajenda ya siri inayohusu uchu wa madaraka!

Tunakoelekea hali hii isipobadilika, nadhani itafika pahala waTz wote tutaongea lugha moja bila kujali itikadi zetu za kisiasa, kidini ama kikabila isipokuwa kwa genge dogo la walamba asali ambao ni la wachache na hapo ndipo patakapokuwa patamu.
 
Back
Top Bottom