Japan yaipatia Tanzania mkopo wa Shilingi bilioni 761.8. Zanzibar yapata mgao wa Tsh bilioni 218

Nauchukia sana mfumo wa Muungano huu wa Tanganyika na Zanzibar sema tu ndo hivyo nautafutia mkakati wa kuuvunja kwa amani ili haki ya Watanganyika irudi tena

Aiseeee
 

Mama anaupiga mwingi mtanyooka hakika....
 
Kwani huu Muungano sisi tunaung'ang'ania una faida gani na sisi, kidhati kabisa mie sioni faida kwetu kwenye huu muungano, halafu kibaya zaidi ni sisi ndio tunafosi, wazanzibar wakitaka nchi yao inakuwa msala.

Hahahahba
 
Ningekufunza jambo lakini kwa kauli hii ya "kisiwa cha Zanzibar " basi nimeamua kukuacha na malalamiko yako.

Wengi wenu mnalalama ovyo tu humu, endeleeni kulalama.

Viva Mama Samia Suluhu Hassan. Jambo la mama ni jambo letu

#nyukiwamama

Zanzibar ni kisiwa kilichopo Tanzania sasa unabisha nini?au we jogirafi umesomea unguja au pemba?
 

Zanzibar ifikapo mwaka 2030 kwa migao hii , itakuwa sawa na Brunei​

 
Naona Wakojani awamu hii meno yote nje [emoji16]
Nyerere namkubali sana.
Ila kamwe nitampinga kwa sera yake mbovu ya Ujamaa na pia kwa kitendo chake cha kumbeba mtoto asiye kua miaka yote (Zanzibar)

Hahahahahahhaha
 
Ma CCM yanaumia polepole maana kusema mama anapendelea Zanzibar hayawezi
 
Naona Tanganyika wanawekeza kuijenga zanzibar iwe dubai ya Afrika, kongole sana Tanganyika...........sasa ifkie mahala zanzberi wawaone Tanganyika kama ndugu zao na wakienda kujivinjari hapo dubai ya Afrika wasiwaite majina ya ajabu ajabu ya kuwabagua kama 'chogo huyooooo...........'inabidi wawaone kama sponsors au beberu mweusi.​
 
Hizi fedha zanzibar wanapewa mgao mkubwa , wanatumia formula gani kuzigawa? Ukubwa wa eneo? Idadi ya watu? Au Maza hajui hesabu?
 
Haya ndo mambo ambayo Hangaya kayafanyia kazi! a.k.a kero za muungano yaani Tanzania bara inapata billion 540 na zanzibar wanapata karibia billion 220 huu ni upuuzi wa hali ya juu! Watanganyika mnachekelea tu!
Sisi Watanganyika Elimu zetu hazijatusaidia kabisa. Tunapenda kupotosha mambo for unnecessary. Kuna tofauti Kati ya mgawo fedha kwa Zanzibar na utekelezaji wa mradi wa Serikali ya Muungano ndani ya Zanzibar. Pesa zimeombwa kea specific projects na moja Kati ya projects hizo ni hiyo ya maji Zanzibar. Kuna shida gani kwa serikali ya Muungano kutekeleza mradi wa maji Zanzibar? Mbona kule Arusha umetekelezwa mradi wa Bilioni 500+? Mbona JPM alitekeleza mradi wa shule za kisasa kila Wilaya Zanzibar na Pemba?
 
Hizi fedha zanzibar wanapewa mgao mkubwa , wanatumia formula gani kuzigawa? Ukubwa wa eneo? Idadi ya watu? Au Maza hajui hesabu?
Huo sio mgawo kwa Zanzibar ni fedha zinzazoenda kutekeleza mradi ndani ya Zanzibar na huu si wa kwanza. Hata mradi wa Airport ya Zanzibar ulitekelezwa kwa style hii.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…