Japo Wakristo na Waislamu ni Watoto wa Baba Mmoja, Nabii Ibrahim na Mungu ni Mmoja, Kati ya Ismail na Isaka ni nani aliyetolewa Sadaka ya Kuchinja?

mbona swali ni jepesi tu, kwa ushahidi wa maandiko ni nani alitakiwa kuchinjwa kati ya Isaka na Ishmael?
Hakuna yeyote aliyetakiwa kuchinjwa, watafsiri wa Qur'an wamekosea sana tafsiri, sijuwi hilo la kuchinjwa mtoto wamelitowa wapi.


Nijuavyo limetumika neno "dhabih" ambalo kitafsida linamaanisha kukatwa jando.
 
Kwa mujibu wa Quran yeah, uislam maana yake unyenyekevu kwa Mungu'

Kuna pahala kwenye bible pameandikwa Ibrahim alikua mnyenyekevu kwa Mungu',Kama kumbukumbu zangu si chakavu,ambapo bible ya kiarabu itakua imeandika Ibrahim alikua muislam
Hahaha kwahiyo Yesu naye ni muislamu?

Mathayo 11:29

[29]Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;
 
Ibrahim hahusiani chochote na ukiristo,hakuwa mkiristo, wakiristo wao Imani yao inatoka na yesu ambaye kwao ni Mungu na mwana wa Mungu pia, Mungu wa Ibrahim alikua mmoja tu,Hana mwana Wala hakuzaliwa Kama ilivyo Imani ya kiyahudi
Tena wala haitoki kwa Yesu, Yesu kaondoka hakuna anayeitwa Mkristo wala Ukristo.
 
Hebu soma kisa cha Penina na Hana, Hana akiwa mke mkubwa na Penina mke mdogo

1samwel 1:1-21 halafu uje tena tuelewane
Mkuu Habari?
Story ya Elikana na Story ya Ibrahim haina mfanano hata Kidogo..

Kwanza Ibrahimu Amezaliwa kabla ya Kuletwa kwa Sheria na Torati kwahyo Misingi yote ilikuwa Inategemea Maagizo ya Mungu na Kumsikiliza anasema nini na kulikuwa hakuna sheria..

NA Elikana kazaliwa Kipindi ambacho Musa Ameshaweka Torati na sheria zipo wazi mpaka za Kuhandle wake wawili au Mmoja jinsi ya Kuoa na Jinsi ya Kuishi..

Hata Yakobo angezakiwa kipindi Cha baada ya Musa asingeweza Kumuoa lea na Rahel kwa pamoja maana Torati hairuhusu kuoa wanawake kutoka Nyumba moja..

Pili Ibrahimu Alipomuoa Hajari, Hajari hakuwa Mwebrania alikuwa Mmisri hivyo haki zake kama Raia zilikuwa Finyu sana na Ni vyepesi kutengwa na kuteswa..(KUMBUKA KISA CHA MUSA ALIPOMUOA MKUSHI)...
wakati elikana alimuoa Penina na Hana wote walikuwa waebrania..

Story zinakaribia kuendenana ila Ziko era Tofauti na Themes tofauti kabisa
 
Afa Afadhali hata Biblia imeongea kisa kizima na kumtaja Isaka.
Kuliko hicho kitabu kingine.
Ukiacha makosa machache ya kiuandishi.
 
Asiyeelewa hapa asubiri kuitwa na spika
 
Mtu anayejiita mkristo halafu hana uhakika na amachokoamini si mkristo. Maana Kristo ni kweli na kweli inakuweka huru. Mtu mwenyewasiwasi wa Imani kama huyo jamaa hamjui Kristo kama inavyompasa
 
nilichokuwa nataka uelewe ni treatment kati ya mke na mjakazi, wajakazi wote walikuwa chini ya mke sio mume, ni sawa na housegirl siku hizi mara nyingi wanakuwa chini ya mke, na ndo maana utaona Ibrahimu anakuwa hana maamuzi juu ya Hajir kwa sababu alizaa naye tu hakuwa mke bali alikuwa mjakazi aliyezaa na Boss wake, Milka na Bilha hawajawah kuwa wake wa Yakobo bali wajakazi licha ya kwamba alizaa nao, status yao iliendelea kubaki kuwa wajakazi tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…