Japo Wakristo na Waislamu ni Watoto wa Baba Mmoja, Nabii Ibrahim na Mungu ni Mmoja, Kati ya Ismail na Isaka ni nani aliyetolewa Sadaka ya Kuchinja?

Ismail ndiye aliyetakiwa kutolewa sadaka.
 

Ujuwe tu kuwa Quran ina miaka 1400 wakati Bibilia ina miaka zaidi ya 2000. Hapo utagundua ni nani kakopi kwa nani?

Halafu kuna watu wanadanganywa eti Mtume wao aliteremshiwa kitabu. Uwongo mtupu
hakuna kitu kama hicho labda unalazimisha ili ukubaliwe na jamii mkristo ni tofauti na muislamu na hawajawahi kuwa watoto wa baba mmjoja kamwe na haijawahi kuwa na haitakaa iwe na miungu yao ni tofaoti pia wala hailingani maana kila mmoja ameagizwa tofauti hivyo hawawezi kuwa na baba mmoja
 
Katika kitabu cha Mwanzo, Mungu anamtaka Ibrahimu amtoe dhabihu Isaka kama sehemu ya agano kwa wana wa Israeli.

NOTE: ... MWANZO 22:2
Akasema, Umchukue mwanao, mwana wako wa pekee, umpendaye, Isaka, ukaende zako mpaka nchi ya Moria, ukamtoe sadaka ya kuteketezwa huko juu ya mlima mmojawapo nitakaokuambia.


Hapo mbona ipo wazi kabisa kwamba ni Isaka ndiye alitakiwa kutolewa sadaka ya kuchinjwa kuonyesha utii kwa Mungu!.
 
Hamia kwenye Hadithi za Maulana utaona Maulana walivyoandika
 
Hamia kwenye Hadithi za Maulana utaona Maulana walivyoandika
Wanapinga kwamba haipo hivyo.

Kauli zao ni kama hii hapa...
"Ni wazi kabisa kwamba Ishmaeli alikuwa mwana wa kutolewa kafara na sio Isaka, amani iwe juu yao wote wawili.

Na wanasema Biblia imepotoka, sasa ukishaona mtu ambaye anapinga kitabu kilichompa mafunuo kiongozi wake, shtuka!.
 

Ndoa ya Ibrahim hakuwahi kuoa Ndoa za Mitala.
Mke wake alikuwa ni Sarah. Kisha alipokufa akamwoa Ketura.

Hajiri hajawahi kuwa Mke wa Ibrahim. Alikuwa ni kijakazi wa Sarah.
Kwa sheria za zamani kijakazi huweza kumzalia Bwana wa Boss wake(Sarah) kama ataruhusiwa.

Isaka ndiye anayetambulika kama mtoto wa familia ya Ibrahim na sio Ishmael.

Wahusika wakuu katika kisa cha Ibrahim ni Ibrahim mwenyewe na Sarah kisha kwenye episode zilizofuata wahusika wakuu wakawa Isaka na Raheli.

Ishmael na Hajiri ni wahusika wadogo sana ambao hata ukiwaondoa kwenye simulizi hiyo stori haitapata dosari kubwa. Ni sawa utoe kijiko cha maji kwenye bahari hakuna tofauti itakayoonekana
 
Kitabu hapo cha kuaminiwa ni Toraut ya wayahudi,kurwani ni kopi na paste ya uongo kutoka kwa mudi ili kupoteza hitoria ya kweli.
 
Kitu muhimu ni tuutafute ukweli, Mungu hakuleta dini wale Yesu hakuleta dini!. Hoja hapa ni nani mkweli na nani muongo?. Mtoto aliyetaka kutolewa sadaka ya kuchinja ni nani?.
P
Biblia inasema ni Isaka. Biblia Ina umri wa miaka 3,537

Quran inasema ni Ishmael. Quran Ina miaka 1,402.
Kazi ni kwake kupima ukweli.
 
Tikiachana na maandiko tukarudi katika hali ya kawaida, inaonekana mtoto aliyetaka kuchinjwa ni Ishmael. Kwa maana ya kwamba ndiye aliyekuwa mtoto wa pekee, kuchinjwa kwa Isaka kusingemuuma sana Ibrahim maana angejua hata akichinja huyu bado anabakiwa na mtoto wake mwingine wa kwanza ambaye ni Ishmael. Huu ni wangu mtazamo wa hisia zangu binafsi bila kuhusisha vitabu vya maandiko ya dini, labda sasa waje wataalamu wa maandiko watuthibitishie ukweli ni upi.
 
Imani hizo za Ukristo na uislam ni matawi ya Judaism. Ukifuata nyaraka za Judaism aliyetolewa sadaka ni Isaac na si ishumail. Quran ni copy ya Bible na edition mbalimbali zilifanywa na waandishi wa mtume s.a.w. Hukuna ukweli juu ya ishumail maana tukio Hilo lilitokea baada ya yule kijakazi na mwanae kuondoshwa. Kuhusi idd(sikukuu) zilikuapo nyingi kabla ya uislam. Hivyo kusema sikukuu ya idd si sahihi maana idd maana yake ni sikukuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…