Mzito Kabwela
JF-Expert Member
- Nov 28, 2009
- 18,887
- 7,673
Mimi hata sijatosheka na simulizi hii, kwa kifupi sijaelewa.
Sio peke yako mkuu
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mimi hata sijatosheka na simulizi hii, kwa kifupi sijaelewa.
Yericko Nyerere,
..ur of the mark katika madai yako kwenye post # 4.
..mfano: Hans Pope hakuwahi kuwa Maj Gen. Pia alipatikana na hatia ya makosa ya uhaini na kufungwa jela.
..pia komandoo aliyeuawa alijulikana kwa jina la mohamed tamim, lakini hakuuawa ktk mapambano toka airport mpaka kinondoni.
..kumbukumbu zako ni sawa na zako kuhusu idadi ya majaribio kuwa ni matatu. jaribio la kwanza, na serious kupita yote kwa mtizamo wangu, ni la 1964. jaribio la pili ni la miaka ya 1970 ambalo lilihusisha wanajeshi, wanasiasa kama Kamaliza,Chipaka, etc inasemekana hawa walijaribu kuhusisha wapiganaji wa vyama za ukombozi. Inasemekana jaribio hili la pili lilikuwa na mkono wa Oscar Kambona. jaribio # 3, liliwahusisha wakina Lugangira,Hatibu Gandhi, Zacharia Hans Pope, etc etc.
@Mzee Mwanakijiji,
..serikali ya Mwalimu Nyerere ilichelewa ktk utekelezaji wa zoezi la Africanization kwa upande wa jeshi.
..hiyo ilipelekea askari wa ngazi za NCO kuanza vurugu za kuwakataa maofisa wa Kizungu waliokuwa wakiongoza jeshi.
..kiongozi wa maasi hayo alikuwa Sgt.Hingo Ilogi. sasa kuna wakati Sgt.Hingo Ilogi na wenzake walikwenda mpaka Ikulu kwa nia ya "kuonana" na Mwalimu Nyerere.
..inasemekana walipofika[Hingo Ilogi & Co] ikulu walikutana na aliyekuwa mkuu wa usalama wa taifa, Emilius Mzena, ambaye alitumia ujanja na kuwadanganya kwamba Mwalimu alikuwa hayuko Ikulu. kuna wanaodai kitendo cha Mzena ndiyo kilimuokoa Mwalimu kwasababu maana baada ya hapo alipelekwa mafichoni.
..kwa mtizamo wangu, askari toka Uingereza ndiyo waliookoa jahazi, vinginevyo tungekuwa tunaongea habari nyingine kabisa hapa.
NB:
..kuna mwana JF anaitwa Shwari, huyu huwa ni msaada mkubwa sana ktk masuala ya kihistoria kama haya.
Yuko wapi uncle Thom aka Father Thom?
Kwanza ilikuwa. 1964 wanajeshi. Colito[. Lugalo]. Barracks walipofanya rioting. Dar es. Salaam. Halafu lilikuwepo jaribio lililofanywa na. Bibi. Titi. Mohammed na wenzake . By the way,yule. Bibi. Titi alikuwa hajui kusoma na kuandika. Hili jambo nimeambiwa na impeccable sources. Halafu jaribio hilo unalozungumzia ndio la mwisho lililofanywa na. Zakaria. Hans. Poppe. Mwalimu alishtuka sana. Zakaria alipofanikiwa kutoka jela. Akaniambia kwa nini wanamwamini yule wanamtoa jela.
yalikua maasi ya wanajeshi sio mapinduzi.yalizimwa na jeshi la uingereza.kuna kitabu cha paulo sozigwa,kama sikosei alikua mwandishi wa rais ndo kimeelezea vizuri hatua kwa hatua kuhusu kilichotokea.ukitafuta library waweza kukipata.
akili ya kawaida sio jambo la kawaida.Hawa CHADEMA ni janga,yani kumbe walianza zamani kuitaka nchi hii kwa mabavu aiseeeee!
Cc Baba V
Nadhani Kawawa ni lile tukio la mwisho, na ndio jina la simba wa yuda lilipoanziaCompanero,
Si kweli kwamba Oscar ndiye aliyemwokoa na kumficha Mwalimu katika mapinduzi ya 1964. Huyu mtafiti amekosea. Nadhani Kawawa alikuwa na jukumu kubwa zaidi kumshawishi Mwalimu kujificha kuliko Kambona. Kambona hakujua alipofichwa Mwalimu.
nini kilitokea hadi baadaye Kambona akakimbia nchi!Kuasi kule kwa Wanajeshi Januari/20/1964 (Tanganyika Rifles) wala sio jambo la zamani sana kiasi cha kusema kwamba Historia ile imetupwa na hakuna anayesema ukweli,nilikuwa nahisi Viongozi kama Mwalimu,kawawa na Kambona wangeyaweka katika maandishi mambo yale muhimu ktk Historia ya Nchi yetu kabla hawajatutoka.Hakuna mahali mambo haya yameandikwa na ndio maana Vijana wanaotaka kujua historia ya Nchi yao wanakuja na hizi hear/say
Askari wale wa Tanganyika Rifles waliasi...Miongoni mwa mambo waliyokuwa wanadai ni hali nzuri ya maisha ya askari mtanganyika,mshahara ulikuwa mdogo,hawakupandishwa vyeo na hakukuwa na Watanganyika katika vyeo vya juu ndani ya Jeshi lile.Askari waliasi na kuingia mjini,na wengine walikwenda kwenye Makazi ya Maafisa wa kiingereza (Raia) na kuwashikilia.Waziri wa Ulinzi wakati huo alikuwa Oscar Kambona....Mwalimu na Mzee Kawawa kwa usalama wao walitoroshwa na kwenda kujificha,inasemekana Maficho yao yalikuwa Kigamboni.Waziri wa Ulinzi (Kambona) alijaribu kupita ktk Barracks na kuwaomba askari watulie bila mafanikio.
Hali ile iliendelea kuwa mbaya,na Mwalimu kwa ushauri wa Kambona na Kawawa akaomba msaada kwa Uingereza ili waje waokoe hali ile ambayo ilikuwa inaelekea kuwa mbaya,kufuatia kuasi kwa Askari wetu,askari wa Kenya na Uganda nao waliasi kwa sababu sawa kabisa na za UASI wa Tanganyika Rifles.Malkia alituma kikosi maalumu cha Askari wa Uingereza ambao walikuwepo ktk ghuba ya Aden,Askari hao walikuja na Meli kubwa ya kivita HMS Centaur ambayo ilikuwa na Makomandoo (45 RM),askari na helikopta.Walifanikiwa kutuliza maasi yale,na Mwalimu na Kawawa wakatoka mafichoni na kuonekana hadharani wakiwa na Waziri wa Ulinzi,ambaye alifanya kazi kubwa bila mafanikio kuwaomba askari(Waliokuwa wananuheshimu sana) waache uasi na madai yao yatafanyiwa kazi.Ukitaka kupata mambo mengi kuhusu maasi yale pitia kitabu "Dar Mutiny Of 1964" by Christopher MacRae
Alikuwepo na marehem EUGEN MAGANGA cheo chake ni cptnJapo historia haisemi wazi juu ya mambo mengi sana Tanganyika na Tanzania ya leo, lakini Mwalimu Nyerere tangu awe kiongozi wa nchi hii amenusurika mapinduzi MATATU,
Moja ni la mwaka 1964, lapili ni la mwaka 1970 na la mwisho ni la mwaka 1980 (Sina uhakika sawa na hiyo miaka)
Jaribio la kwanza ndilo lilipelekea kuundwa kwa JWTZ na lilizimwa kwamsaada wa Malkia wa Uingereza aliyetuma makomandoo maalumu na wakafanikiwa, Jaribio la pili ndilo lililopelekea kuundwa kwa Usalama wa Taifa na kikosi maalumu cha ulinzi wa Rais,
na jaribio la mwisho ndio lilipelekea kubadili sera ya usalama wa Taifa kwa kuwapandikiza kila kwenye sekta na kuwa kila mtu ni mlinzi wa nchi hii (usalama)
Sikumbuki vema lakwanza kama liliongozwa na nani lakini Kambona ndie alimficha Mwalimu, lapili sikumbuki vema, lakini la mwisho liliongozwa na baadhi ya wanajeshi wa kikosi cha Anga cha Ukonga Banana,
Na mipango yao iliharibikia palepale Banana baa baada ya mmoja wao kulewa na kuanza kuongea hovyo hasa akisema yeye anataka cheo cha uwaziri mkuu!
Enzi hizo 1980+ mmoja wa makamanda wa usalama wa taifa aliyeongoza kuwadhibiti waasi hao ni Mabere Marandu,
Na alifanikiwa kuongoza oparesheni za kumsaka na kumuua mmoja wa makomandoo ambae alikuwa ameandaliwa rasmi kumuua Nyerere,
Mapambano yalikuwa ni makubwa kutoka airport hadi kinondoni ulipo ubalozi wa Marekani sasa ndipo walipofanikiwa kumuua!
Jambo la kuwashangaza waasi wale (wanajeshi) wote Mwalimu aliwaita ikulu,
akamwambia kiongozi wa mapinduzi yale (simkumbuki) kuwa
"Shika bunduki uniue wewe mwenyewe kwamkono wako ili uwe rais wa nchi hii"
jamaa aliomba radhi huku akitambaa kisha mwalimu akasema
"nimewasamehe wote"
na aliwapa vyeo na kazi, wengi walikwenda kuwa mabalozi wa Tz nchi za nje!
Sisi hapa tunasema kama porojo tu, lakini yapo mengi sana nyuma ya pazia!
Watawala wanahisi kuyataja ni kama kuharibu sifa ya Tanzania na wengine wanaona kama itaharibu sifa ya Mwalimu.
Mimi binafsi nafikiri kama yatasemwa hadharani yataongeza sifa ya Mwalimu Nyerere na utawala wa ccm ya kale!
Atakuwa ni kiongozi pekee barani afrika na duniani aliyenusurika majaribio matatu ya uasi,
Atakuwa ni kiongozi wa kwanza duniani kuwasamehe waasi kwa mda huohuo wa uasi (baada ya kuwakamata) na kuwapa kazi nyingine za kitaifa
Atakuwa ni kiongozi pekee duniani aliye ng'atuka kwa amani na kwenda kuishi kijiji tena bila hata ulinzi, akitembelea land rover ya shamba miaka mitano tu baada ya jaribio kali la mapinduzi ya Banana Ukonga!
Hizo zote zilikuwa ni sifa zake ambazo watawala wa leo kwa makusudi ama kwakujua au kutojua wamefifisha nyota ya mwana wa Afrika mbele ya uso wa mataifa!
Na kwakuwafahamisha tu ni kuwa mmoja ya wanajeshi hao walioasi ni Meja Gen Hans Popi yule mwenye Sams Super Store pale Mbezi Makonde!
Kwakifupi hayo ndiyo ninayafahamu,
Did you know Hans Poppe spent more than 10 years behind bars? Nafikiri aliachiwa baada ya kuanza kwa vyama vingi. Hata hivyo ni mmoja ya watu wenye uwezo mkubwa kiakili na kwa jinsi anavyopeleka mambo, he was not a soldier by accident! ndio maana ameweza kujibadili na kuwa mfanyabiashara mkubwa kwa kipindi kifupi baada ya kutoka lupango.
Ndio huyo huyo.Ambaye alikuwa yuko huko UKAWA ni mtu wa TEAM LOWASA na alikuwa bega kwa bega kwenye mbio zake za uraisi.Ndio hao nadhani Kingunge alikuwa akijivunia kuwa Lowasa akishindwa nchi itawaka moto.Lowasa alikuwa na mtandao wa ajabu acha tu.Mungu kainusuru TanzaniaHivi ni huyu Hans Pope wa Simba sports club?
tumshukuru munguNdio huyo huyo.Ambaye alikuwa yuko huko UKAWA ni mtu wa TEAM LOWASA na alikuwa bega kwa bega kwenye mbio zake za uraisi.Ndio hao nadhani Kingunge alikuwa akijivunia kuwa Lowasa akishindwa nchi itawaka moto.Lowasa alikuwa na mtandao wa ajabu acha tu.Mungu kainusuru Tanzania
Hicho ni cheo kipi mkuu?Maganga alikuwa Luteni.Alikuwepo na marehem EUGEN MAGANGA cheo chake ni cptn
Alikuwa Captain. Na hivyo ndivyo tulivyomuita tulipokuwa chuoni (UDSM): Captain Maganga. Kuna makala ya Eric Kabendera ambayo imepotosha ukweli na kusema alikuwa Luteni. Ninamfahamu marehemu binafsi.Hicho ni cheo kipi mkuu?Maganga alikuwa Luteni.
Mwanakijiji ni wapi naweza pata vitabu vya historia ya TanganyikaJamani kama hamjui historia ya nchi yenu msiitengeneze..