Jaribio la kutaka kuiangusha serikali ya Nyerere 1982/1983

Nachingia kidogo nawakumbuka alikuwepo Murtaza Lakha, Issa shirvji

Nadhani Mama Tatu Ntimizi naye alikuwemo kwa upande wa serikali, kama kumbukumbu zangu zinanijia sawasawa, wakati huo alikuwa jeshi la Polisi.
 
Tamim, nadhani aliuawa pale KINONDONI, au siyo?
Sahihi kabisa, naikumbuka vema siku hiyo. Nilikuwa nimempiga uncle wangu mmoja mzinga kidogo ili kuongezea nguvu nikirudi shule kesho yake niwe na nguvu ya ziada.
Sasa kwa vile yeye alikuwa anaishi Mwananyamala habari zikawa zimeenea kuwa maeneo hayo sio salama kwenda na mie kesho yake narudi shule Moshi.
Ikala kwangu
 
Mtuhumiwa mmoja wapo wa hiyo kesi ni Zakaria Hans Pope wa Simba..
Alifungwa miaka zaidi ya kumi lakini sasa hivi ni Tajiri.
 
Hii stori mbona ina imperfection nyingi sana ,kama akina nani walishitakiwa?ilikuaje?kesi hukumu yake ilitolowaje and proceedings za kesi zilikuaje

Duh, pengine siyo vizuri kuwataja humu, kwani wengi bado wapo na wana nyadhifa nzuri kwenye private sector na nadhani mpaka kwenye sports.
 
Remember the Asian Advocate Murtaza Lakha?
Enzi hizo gazeti zuri kuliko yote lilikuwa mfanyakazi likitoka jumamosi. ukiwa bara unalipata jumatano. enzi za akina james nhende the late katabaro hemedi kimwaga etc.

Yule ni Hemed KIMWANGA na siyo 'KIMWAGA'
 
Duh, pengine siyo vizuri kuwataja humu, kwani wengi bado wapo na wana nyadhifa nzuri kwenye private sector na nadhani mpaka kwenye sports.
Waliohusika ni

Hatty MacGhee
Eugene Mahanga(rip)
Z Hans Pope
Kadego...n.k
 

Aaah, kweli comrade, mimi wakati ule nilikuwa naishi Mwenge basi habari zilizagaa kimya kimya
 
Waliohusika ni

Hatty MacGhee
Eugene Mahanga(rip)
Z Hans Pope
Kadego...n.k

Aaahaa, eeh bwana, acha kuwataja watu bwana, mambo yale yalikwisha,siyo vizuri mnavyofanya
 
Aaahaa, eeh bwana, acha kuwataja watu bwana, mambo yale yalikwisha,siyo vizuri mnavyofanya
Mkuu 1954 sheria ya mtandao nimeikiuka kifungu gani? Niambie niandae utetezi.
 
Sijui Kama Serikali hii inaweza kuruhusu ama kutoa kibari cha kucheza hiyo Movie, but Ni idea nzuri!
 
Tamim, nadhani aliuawa pale KINONDONI, au siyo?
Exactly. Tamimu aliuawa pale Kinondoni mkwajuni. Kipindi hicho na mimi nilikuwa nikiishi maeneo ya Kindondoni mkwajuni. Tamimu alikuwa akitoka kwenye kikao kwenye nyumba moja iliyopo maeneo hayohayo ya Mkwajuni. Nakumbuka ile nyumba ilizungukwa na askari takriban week nzima. Hata kupita tu karibu na ile nyumba ilikuwa ni marufuku. Eneo lote la mkwajuni lilijaa askari kanzu. Nakumbuka hata eneo la mkwajuni lilifungwa kwa siku mbili tatu hivi. Mashuhuda walisema, askari kanzu (usalama wa taifa) walivamia nyumba kilimokuwa kinafanyika hicho kikao kwa nia ya kuwakamata wote kwenye kikao, lakini Tamimu aliwazidi ujanja na kiwango. Akafanikiwa kuchomoka na kuruka ukuta. Alipotua nje akawakuta wametanda. Ukapigwa mkono wa kufa mtu. Akawazidi tena kiwango, akawachomoka na kuelekea kilipo kituo cha daladala upande wa kuelekea Morocco. Jamaa nao walikuwa wanamfukuza, Tamimu alipofika maeneo ya kituo cha daladala aliona gari ya beer ikipita. Alidandia gari ya beer na kuanza kuvurumisha chupa za beer kwa askari kanzu wale. Tamimu ndio alikuwa anawatoka hivyo. Nadhani askari kanzu wale walijipanga vizuri na waliamini Tamimu hachomoki. Hivyo nahisi hawakuwa na plan B. Hivyo Tamimu alikung'utwa za kifua na kufariki palepale. Pia nilibahatika kusoma kitabu chote cha kesi ya uhaini. Sikumbuki nilikitupia wapi. Mawakili walionifurahisha walikuwa ni Lakha na Lamwai. Sijui kama Lamwai wa ile kesi ndiye yuleyule wa NCCR Mageuzi.
 
Mkuu, ni vigumu kupata melezo ya kutosha kutoka kwa sisi wanajukwaa wa kawaida ,ila kwa habari za kina wasiliana na watu wa New habari media kwani wakati fulani gazeti la Rai lilichapisha maelezo marefu ya marehemu Gasper Eugien Maganga aliyekuwa mshitakiwa katika kesi ile.

Hata hiyo kwa uhakika ni kwamba Maganga, barozi Ngaiza, George. na Hatty Gandh ni marehemu.
 

Duh, wewe ni kiboko, umeeleza vema, isipokuwa sina uhakika na hilo jina la LAMWAI. Ila ile incidence naikumbuka sana. Yule TAMIM alikuwa noma sana, kwa mapambano, alikuwa ni komandoo haswa. Sina hakika sana yule jamaa, nadhani alikuwa wa Tanga kama sijakosea, but I am not so sure...ila lile kundi (wahaini) lilikuwa infiltrated sana, wao wenyewe walikuwa hawajui, basi tu hatuwezi kusema mengi humu JF. Ila TISS ya wakati ule ilikuwa kiboko, walikuwa wanachapa kazi kweli kweli, wazalendo, committed to their profession. Walikuwa wanakuwa vetted kweli kweli, lakini siku hizi, aaah, sijui bwana....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…