Jaribio la kutaka kuiangusha serikali ya Nyerere 1982/1983

Jaribio la kutaka kuiangusha serikali ya Nyerere 1982/1983

Huyu ni mpiganaji asilia
Hakuna cha upiganaji wala nini,alisaidiwa na ndugu zke walioko Canafa na Australia.walimpa malori ya mizigo ndo kilichomtoa.mdogo wake yeye walipoachiwa na Mwinyi 1995 aliondoka zake nchini.
 
Wadau naomba kujua jinsi upangaji njama za kufanya Uhaini Serikali ya Hayati Mwl.Nyerere miaka hiyo.
 
Japo historia haisemi wazi juu ya mambo mengi sana Tanganyika na Tanzania ya leo, lakini Mwalimu Nyerere tangu awe kiongozi wa nchi hii amenusurika mapinduzi MATATU,

Moja ni la mwaka 1964, lapili ni la mwaka 1970 na la mwisho ni la mwaka 1980 (Sina uhakika sawa na hiyo miaka)

Jaribio la kwanza ndilo lilipelekea kuundwa kwa JWTZ na lilizimwa kwamsaada wa Malkia wa Uingereza aliyetuma makomandoo maalumu na wakafanikiwa, Jaribio la pili ndilo lililopelekea kuundwa kwa Usalama wa Taifa na kikosi maalumu cha ulinzi wa Rais,

na jaribio la mwisho ndio lilipelekea kubadili sera ya usalama wa Taifa kwa kuwapandikiza kila kwenye sekta na kuwa kila mtu ni mlinzi wa nchi hii (usalama)

Sikumbuki vema lakwanza kama liliongozwa na nani lakini Kambona ndie alimficha Mwalimu, lapili sikumbuki vema, lakini la mwisho liliongozwa na baadhi ya wanajeshi wa kikosi cha Anga cha Ukonga Banana,

Na mipango yao iliharibikia palepale Banana baa baada ya mmoja wao kulewa na kuanza kuongea hovyo hasa akisema yeye anataka cheo cha uwaziri mkuu!

Enzi hizo 1980+ mmoja wa makamanda wa usalama wa taifa aliyeongoza kuwadhibiti waasi hao ni Mabere Marandu,

Na alifanikiwa kuongoza oparesheni za kumsaka na kumuua mmoja wa makomandoo ambae alikuwa ameandaliwa rasmi kumuua Nyerere,

Mapambano yalikuwa ni makubwa kutoka airport hadi kinondoni ulipo ubalozi wa Marekani sasa ndipo walipofanikiwa kumuua!

Jambo la kuwashangaza waasi wale (wanajeshi) wote Mwalimu aliwaita ikulu,

akamwambia kiongozi wa mapinduzi yale (simkumbuki) kuwa

"Shika bunduki uniue wewe mwenyewe kwamkono wako ili uwe rais wa nchi hii"

jamaa aliomba radhi huku akitambaa kisha mwalimu akasema

"nimewasamehe wote"

na aliwapa vyeo na kazi, wengi walikwenda kuwa mabalozi wa Tz nchi za nje!

Sisi hapa tunasema kama porojo tu, lakini yapo mengi sana nyuma ya pazia!

Watawala wanahisi kuyataja ni kama kuharibu sifa ya Tanzania na wengine wanaona kama itaharibu sifa ya Mwalimu.

Mimi binafsi nafikiri kama yatasemwa hadharani yataongeza sifa ya Mwalimu Nyerere na utawala wa ccm ya kale!

Atakuwa ni kiongozi pekee barani afrika na duniani aliyenusurika majaribio matatu ya uasi,

Atakuwa ni kiongozi wa kwanza duniani kuwasamehe waasi kwa mda huohuo wa uasi (baada ya kuwakamata) na kuwapa kazi nyingine za kitaifa

Atakuwa ni kiongozi pekee duniani aliye ng'atuka kwa amani na kwenda kuishi kijiji tena bila hata ulinzi, akitembelea land rover ya shamba miaka mitano tu baada ya jaribio kali la mapinduzi ya Banana Ukonga!

Hizo zote zilikuwa ni sifa zake ambazo watawala wa leo kwa makusudi ama kwakujua au kutojua wamefifisha nyota ya mwana wa Afrika mbele ya uso wa mataifa!

Na kwakuwafahamisha tu ni kuwa mmoja ya wanajeshi hao walioasi ni Meja Gen Hans Popi yule mwenye Sams Super Store pale Mbezi Makonde!

Kwakifupi hayo ndiyo ninayafahamu,
Hadithi za kutengenezwa huwa tamu sana!! Hivi waasi waliokuja kuachiwa na mzee Mwinyi ni kina nani?
 
Hiki kitabu hakijasambazwa maeneo mengine ili kisomwe kwa wingi?? Bei yake ikoje?
 
nzuri hii

Sent from my SM-N900 using JamiiForums mobile app
 
Ndio ni Mabere Marandu huyu wa Chadema,

Nigeria walisaidia sana kuja kuleta amani, tulitawaliwa karibu mwaka mmoja!

Wengi wa waasi walisamehewa, lakini makomando na baadhi waliuawa na wengine kupelekwa Gwantanamo ya Afrika, hicho ni kisiwa kidogo kinachomilikiwa na Tanzania kipo kata ya Zanzibar na Tanganyika,

Sina uhakika kama badoo kinatumika ama kinatumika kwa siri zaidi!
Bongoyo island na mbudya island.

Sent from my Lenovo P1a42 using JamiiForums mobile app
 
Shuleni kwetu haiwezi kutokea na wasumbufu wote tunawafuta shule wenye nafuu tunawashusha madarasa.
 
Pasi na shaka nyerere alikuwa ni moja kati ya watu waliokuwa wakitumia "third eye" yao vizuri kabisa.
 
Nyerere kisha taka kupinduliwa mara nyingi tu.

Ni watu walikuwa hawampendi, kadhulumu mali za watu, kuanzia majumba, mashamba, biashara. Akawa hajui kuongoza nchi, aliongoza kidikteta, atakacho yeye ndio hicho hicho, watu wakawa masikini wa kutupwa, kila mtu mnyonge na kadhoofika, kasoro watu wa mduara wake tu.

Kuna kupendwa hapo? Watu waliompenda ni wa kanisa katoliki tu kwani wao ndio aliwatumikia kwanza kuliko nchi, na hilo kalisema mwenyewe si maneno yangu hayo, anaebisha namwekea nukuu. Anza.
Okay kwa nini babu yako hakuongoza nchi
 
Back
Top Bottom