Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
RIWAYA: MPANGO WA CONGO
SEHEMU YA 14
Zilipita dakika kadhaa ndipo alipohisi kuna hali ya tofauti kutoka pale alipokuwa amelala.
Mwili hakuwa na nguvu lakini alisikia joto jingi huku akianza kupaliwa na alipofumbua macho akakutana na wingu la moshi mzito.
Nyumba ilikuwa inaungua!!.
Akajaribu kuinuka ila hakuwa na nguvu,akajaribu tena akashindwa.
Akakata tamaa na tayari alisikia mmomonyoko wa mabati kutokea huko vyumbani.
Kifo kilinusa pua za Solomoni Bukaba.
****
“Yule boya kakuotea leo aisee” alisema bwana mmoja mrefu aliekuwa anaendesha gari kwa kasi kutoka lango lango huku akipishana na magari na baadhi ya raia waliokuwa wameanza kujazana barabarani kushangaa moto mkubwa uliokumba baadhi ya nyumba zilizokuwa zimepakana na nyumba ya Solomoni Bukaba.
“Ndio mana kitengo kina Helper hasa killer akishindwa” alisema binti.
“Wapi sasa” aliuliza yule bwana.
“Club D nishushe pumzi” alijibu binti huku akiegemea kwenye kiti.
“mmh nadhani urudi nyumbani uoge” alishauri bwana dereva.
“ Haina shaka”
Gari ilichochewa moto.
****
..NCHINI CONGO..
Honda alihakikisha maelezo aliopewa na mateka wake yamemkaa sawia na hakutaka kuendelea kuhoji zaidi kwa wakati huo mana hakutaka kupoteza muda zaidi kwa kuwa alijua hapo ndipo ukomo wa ukweli kutoka kwa yule mateka na zaidi ya hapo ni kwa jasho na damu ndo ukweli atapata au kukosa kabisa.
Hakutaka kucheza bahati na sibu na muda.
Lazima amtafute X ambae kwa mujibu wa marehemu Bulembo ni Mtanzania na pia ni Club lakini kwa maelezo ya mateka; ndie aliewatuma wamkamate.
Akabaki na maswali kadhaa hivi.
Je X inahusu watu wangapi ama inahusu mtu mmoja?
Hakuwa na jibu.
Akajizoa zoa kutoka pale alipokuwa kisha akamsogelea mateka wake
“Kwanini mnamuita X?” aliuliza Honda Makubi.
Mateka akatoa cheko la kebehi kisha akajibu;
“Kwa sababu hafahamiki na hajulikani hata kwa sura!!”
“Duh!!” akaguna Honda kisha akaendelea kumsikiliza mateka wake.
“Kwa hiyo uliniona mjinga kukwambia tumetumwa na Mr X? au ulidhani ningemfahamu ninge….” Mateka hakumaliza kauli yake akajikuta anaelea hewani huku akishindwa kujitetea sababu ya kufungwa kamba ngumu kwenye kiti.
Mateka hakuwa na namna akasambaratika chini kama zigo la maharage mabichi.
Honda alijua kuna sababu za kuambiwa bila kukurukakara mwanzo na sababu aliipata na hakuwa tayari kuendelea kudhihakiwa hivyo akamtandika teke kali yule mateka lililomwacha akiwa hana msaada huko alikoangukia.
Honda akamwinua kisha akamshika kosi wa shati lake na kumvutia kwake wakawa wakitazamana kwa karibu.
“Nikirudi utanieleza aba,cha,da zote unazozijua Kimburu wewe” alichimba mkwara Honda kisha akamwachia na kukusanya vilivyo vyake na muhimu akavitia kwenye kwenye mkoba na kuuvaa kisha akatoka na kufunga milango yote vizuri na kuruka ukuta na kutokomea kuwahi pahali.
****
Kiza kilipoanza kuingia, Honda alikuwa nje ya ubalozi wa Tanzania nchini Congo.
Alikuwa amevaa kofia ya pama na suti matata iliomkaa vyema mwilini na kubadilisha mwonekano wake kwa kiasi kikubwa.
Wakati huu alivaa suti kwa sababu kwa waliomzoea kamwe hawakuwahi kumuona akiwa amevaa suti.
Mkononi alishika mkoba mweusi ambao alijua kabisa una uhumimu mkubwa licha ya kuhifadhi vitu asivyovifahamu maana yake.
Tayari wafanyakazi wengi walikuwa wameanza kurudi makwao.
Muda bado ulikuwa unaruhusu kwa watu wenye dharura kuingia na kutoka pale ubalozini kwa wakati huo.
Alijichanganya na watu hatimae alifanikiwa kuingia hadi mapokezi na bahati bado ilikuwa upande wake,mapokezi kulikuwa na watu kadhaa huku sehemu ya kupumzika kukiwa na watu wengine waliokuwa wakingoja huduma.
Akatumia nafasi ile kwa wafanyakazi kuwa bize akapita na kupanda juu kuelekea kwenye ofisi za Mkurugezni wa uhamiaji Papi Mndewa.
Alipofika karibu na mlango wa ofisi za Mkurugezi; Honda akasita kwenda zaidi akarudi nyuma kidogo akaangalia kushoto na kulia, hakuona mtu.
Kumbukumbu ya picha alioiona mezani kwa mhudumu wa mgahawa wa Tunde ikajijenga tena kichwani kwake.
Na hapo akajaribu kutazama tena ni wapi alipopigwa picha na mpigaji alipiga kwa kulenga kona akitokea upande gani!!
Hatimae macho yake yakatua kwenye kona iliotenganisha ofisi ya Balozi na chumba cha mawasiliano.
Konani pale kulikuwa kuna kamera ndogo mbili za usalama.
Macho yake akayahamishia tena kwenye kona iliotumika kutenganisha ofisi ya balozi na Mkurugenzi.
Tofauti na kona ya mwanzo yenye kamera mbili zilizofungwa pamoja, kona hii ilikuwa na kamera moja tu ambayo hata yeye alijua ilikuwepo na kona nyingine pia ilikuwa na kamera moja na ndivyo ilitakiwa iwe kila siku.
Alah!!!
Kamera ya pili ilitoka wapi na kwanini ilikuwa pale na ilikuwa na faida gani!!
Makubwa jama!!
Honda aliweka kituo kichwani kwake kumaanisha amefikia mwisho wa kufikiri wakati huo.
Wakati akitaka kufungua mlango wa mkurugenzi,mlango ukafunguliwa haraka akarudi nyuma.
Macho yao yakagongana.
Alikuwa ni mkurugenzi ambae alikuwa anataka kutoka kwenda kwake.
“Honda!!” aliita kwa kushangaa Mkurugenzi.
Honda akamwonyesha ishara warudi ofisini.
“Aisee nilijua nimeshakupoteza komredi” ndilo aliloweza kusema Mkurugenzi huku akimtizama Honda kama asieamini uwepo wake pale.
“Sio kunipoteza tu, hata uhai ningeupoteza na usingeniona kabisa” alisema Honda huku akikaa juu ya meza na kubaki wakitazamana kwa sekunde kadhaa.
“Nilijua wale jamaa watakuwa si watu wazuri japo kuwaingilia kiharaka vile kungeleta mkanganyiko wa kidiplomasia!!” alisema kwa masikitiko Mkurugenzi Papi Mndewa huku akitupa gazeti mezani pale alipokuwa amekaa Honda.
Honda alilitizama gazeti lile kisha akatabasamu.
“Kwani limeshatoka?” akauliza Honda bila kujishugulisha kulichukua mana ukurasa wa mbele ulikuwa umepambwa picha yake.
Picha ile haikumstua mana alishaiona tangu akiwa Tunde.
“Kwani linatoka lini hili gazeti mbona limesambaa sana!!” akauliza Honda.
“Nimeletewa na mtu wetu alieko huko linakopikwa na linatoka kesho.” Alijibu Papi.
“Kwani ilikuwaje!!” aliuliza Papi.
“Ni hadithi ndefu kidogo komredi ila kifupi tunazungukwa na watu wenye akili na ujuzi pia lakini ni lazima tupambane, na mchawi wetu wa kwanza anaanzia hapa hapa,unaionaje hiyo picha hapo?” alimalizia kwa swali Honda.
“ulipigwa wakati ukiingia hapa ofisni. Nimefikiria sana kuhusu mtu aliepiga picha hii na..!” Papi hakumalizia kauli yake alikatishwa na Honda.
“Picha haijapigwa na kamera ya mtu ila imepigwa kamera ilioko humu, lakini swali la kujiuliza, imewekwa lini na nani alieiweka?” akauliza Honda na kuacha swali lile likiambaa kichwani mwa Papi Mndewa.
Ukapita ukimya kidogo!
“Hii hatari sasa!!” alisema Papi huku dhahiri akionekana kuzama kwenye tafakuri!!
“Komredi mmefikia wapi na nyie!” alisema Honda.
“kiukweli tumeshindwa kujua kilichosababisha mawasiliano kukatika wakati balozi aliposhambuliwa. Tumejaribu kupitia kamera na miundo yote ya usalama ili kuona ni wapi hujuma ilianzia,lakini kote kulikuwa shwari aisee na nimeagiza baada ya kumsafirisha Balozi basi tuanze uchunguzi upya mana kuna ukakasi pahali” alimaliza kueleza Papi.
Honda akazishusha pumzi kwa mkupuo.
“Hali ni tete, lakini hili sakata litaisha, ikishindikana basi tutaomba makao makuu watuongezee nguvu” alisema Honda.
“Japo naamini hujashindwa lakini ikifikia huko tutakuwa hatuna namna!” alisema Papi.
“mmh wale vijana wa kitengo cha usalama wapo wangapi vile!!” alihoji Honda huku dhahiri akionekana kuwa na hisia za kumbukumbu.
“wapo watatu Komredi!!” alijibu Papi.
“Basi jicho lako lianzie hapo Komredi” Honda alimwambia Mkurugenzi wake!
Papi akatikisa kichwa bila kutoa sauti na hilo lilimaanisha tayari uchunguzi dhidi yao umeanza.
“Ok naomba unifikishe ofisini kwa Balozi kuna kitu nahitaji kutazama.” Alipokwisha kusema hivyo tayari miguu yao ilianza kufanya harakati za kuondoka ndani ya kile chumba.
Dakika moja badae wote walikuwa wanatazama tundu la risasi lilokuwa limejenga nyufa kadhaa kwenye kioo.
“Mdunguaji!!” alijisemea Honda huku taratibu akisogea lilipokuwa dirisha.
“ina maana hili pazia lingekuwa limerudishiwa basi mdunguaji angekosa shabaha” alisema tena taratibu Honda huku akishika tundu la risasi ilipopita.
Moja ya sifa kubwa ya kubwa ya Honda ni kutambua ukubwa wa vipenyo vya risasi na aina za silaha.
Hata hapo alijua.
“Hii ni Lapua Magnum bila Shaka” alisema Honda huku akimgeukia papi.
“Yes!! Kitengo kimethibitisha aina hiyo ya risasi na silaha ilikotoka.” Papi alijibu swali la kijana wake.
“Lakini kwa nilivyoona siku ile kabla sijakamatwa hili pazia lilikuwa limerudishiwa makusudi kabisa na nadhani wewe ungechunguza pia aliefanya usafi siku hiyo Mkuu au!” Honda alitoa mawazo yake kwa mtindo wa kuhoji.
“Hilo pia litafanyiwa kazi na sikuwa nimeliwaza kabisa komredi” alisema Papi huku akigonga tano kuashiria amekubali mawazo ya kijana wake ambae tangu wajuane walifanya kazi kwa ukaribu kiasi wakajikuta ni kama wanalingana wadhifa.
“Kile chumba pale ghorofani kinaweza kunifikisha kwa muuaji wa Balozi” alisema Honda huku akinyooshea kidole upande wa pili kulikokuwa na ghorofa kubwa na ndefu.
Ukimya ukapita.
Naendela na majukumu komredi ila usiponiona siku tatu pale ndani kwa Bulembo kuna kipanya nimekihifadhi pale kakichukue kinaweza kukufikisha nilipoishia” alisema Honda huku akianza kutoka pale ofisini.
Kitu kimoja ambacho watu hawa hawakujua ni kuwa kulikuwa na mtu mwingine aliewasikia walichokua wanazungumza.
Lakini kwao ni kama kiza hakuna walichojua.
****
Sajini Kebu alikuwa ametulia kimya huku akiwaza namna alivyonusurika kusombwa na maji yaliokuwa yanapita chini ya daraja alilitupiwamo na Honda.
Kimoyomoyo alihusudu uwezo wa akili wa mtanzania yule.
Sajini kebu akageuza macho yake kushoto kwake akakutana na jicho la Kojo ambae waliunganishwa pamoja baada ya vijana wa Kebu kuadhibiwa na Honda; hivyo sasa alikuwa ameungana na kundi la Kizibo na Kojo.
Aliona jinsi uso wa Kojo ulivyopasuka bila mpangilio.
“Umesema hii kazi ya yule bwege sio!!” aliuliza Sajini Kebu.
Swali lile lilionekana kumkera Kojo ila hakujibu akabaki kutazama pembeni.
“Bwana yule ananitesea rafiki yangu aisee” alidakia Kizibo aliekuwa amekaa kwenye kiti cha dereva.
“Hebu nipelekeni nikapumzike kwa mrembo wangu nikitoka huko risasi za kichwa zitammaliza Honda!!” alisema Sajini Kebu huku akiegemea kiti cha abiria alichokuwa amekalia.
Gari ikawashwa na kuondoka kuelekea viunga vya mji wa Gombe pembeni kidogo ya mji wa Kinshasa.
Ni kwa kuwa hawakujua lijalo halijawahi kujulikana kamwe.
Na kama walidhani wanaenda kupumzika walikosea sana
*****
Shusha komenti yako tafadhali, usipite kimya
shukran shemela,japo natamani kujua mwisho wa solomonRIWAYA: MPANGO WA CONGO
SEHEMU YA 14
Zilipita dakika kadhaa ndipo alipohisi kuna hali ya tofauti kutoka pale alipokuwa amelala.
Mwili hakuwa na nguvu lakini alisikia joto jingi huku akianza kupaliwa na alipofumbua macho akakutana na wingu la moshi mzito.
Nyumba ilikuwa inaungua!!.
Akajaribu kuinuka ila hakuwa na nguvu,akajaribu tena akashindwa.
Akakata tamaa na tayari alisikia mmomonyoko wa mabati kutokea huko vyumbani.
Kifo kilinusa pua za Solomoni Bukaba.
****
“Yule boya kakuotea leo aisee” alisema bwana mmoja mrefu aliekuwa anaendesha gari kwa kasi kutoka lango lango huku akipishana na magari na baadhi ya raia waliokuwa wameanza kujazana barabarani kushangaa moto mkubwa uliokumba baadhi ya nyumba zilizokuwa zimepakana na nyumba ya Solomoni Bukaba.
“Ndio mana kitengo kina Helper hasa killer akishindwa” alisema binti.
“Wapi sasa” aliuliza yule bwana.
“Club D nishushe pumzi” alijibu binti huku akiegemea kwenye kiti.
“mmh nadhani urudi nyumbani uoge” alishauri bwana dereva.
“ Haina shaka”
Gari ilichochewa moto.
****
..NCHINI CONGO..
Honda alihakikisha maelezo aliopewa na mateka wake yamemkaa sawia na hakutaka kuendelea kuhoji zaidi kwa wakati huo mana hakutaka kupoteza muda zaidi kwa kuwa alijua hapo ndipo ukomo wa ukweli kutoka kwa yule mateka na zaidi ya hapo ni kwa jasho na damu ndo ukweli atapata au kukosa kabisa.
Hakutaka kucheza bahati na sibu na muda.
Lazima amtafute X ambae kwa mujibu wa marehemu Bulembo ni Mtanzania na pia ni Club lakini kwa maelezo ya mateka; ndie aliewatuma wamkamate.
Akabaki na maswali kadhaa hivi.
Je X inahusu watu wangapi ama inahusu mtu mmoja?
Hakuwa na jibu.
Akajizoa zoa kutoka pale alipokuwa kisha akamsogelea mateka wake
“Kwanini mnamuita X?” aliuliza Honda Makubi.
Mateka akatoa cheko la kebehi kisha akajibu;
“Kwa sababu hafahamiki na hajulikani hata kwa sura!!”
“Duh!!” akaguna Honda kisha akaendelea kumsikiliza mateka wake.
“Kwa hiyo uliniona mjinga kukwambia tumetumwa na Mr X? au ulidhani ningemfahamu ninge….” Mateka hakumaliza kauli yake akajikuta anaelea hewani huku akishindwa kujitetea sababu ya kufungwa kamba ngumu kwenye kiti.
Mateka hakuwa na namna akasambaratika chini kama zigo la maharage mabichi.
Honda alijua kuna sababu za kuambiwa bila kukurukakara mwanzo na sababu aliipata na hakuwa tayari kuendelea kudhihakiwa hivyo akamtandika teke kali yule mateka lililomwacha akiwa hana msaada huko alikoangukia.
Honda akamwinua kisha akamshika kosi wa shati lake na kumvutia kwake wakawa wakitazamana kwa karibu.
“Nikirudi utanieleza aba,cha,da zote unazozijua Kimburu wewe” alichimba mkwara Honda kisha akamwachia na kukusanya vilivyo vyake na muhimu akavitia kwenye kwenye mkoba na kuuvaa kisha akatoka na kufunga milango yote vizuri na kuruka ukuta na kutokomea kuwahi pahali.
****
Kiza kilipoanza kuingia, Honda alikuwa nje ya ubalozi wa Tanzania nchini Congo.
Alikuwa amevaa kofia ya pama na suti matata iliomkaa vyema mwilini na kubadilisha mwonekano wake kwa kiasi kikubwa.
Wakati huu alivaa suti kwa sababu kwa waliomzoea kamwe hawakuwahi kumuona akiwa amevaa suti.
Mkononi alishika mkoba mweusi ambao alijua kabisa una uhumimu mkubwa licha ya kuhifadhi vitu asivyovifahamu maana yake.
Tayari wafanyakazi wengi walikuwa wameanza kurudi makwao.
Muda bado ulikuwa unaruhusu kwa watu wenye dharura kuingia na kutoka pale ubalozini kwa wakati huo.
Alijichanganya na watu hatimae alifanikiwa kuingia hadi mapokezi na bahati bado ilikuwa upande wake,mapokezi kulikuwa na watu kadhaa huku sehemu ya kupumzika kukiwa na watu wengine waliokuwa wakingoja huduma.
Akatumia nafasi ile kwa wafanyakazi kuwa bize akapita na kupanda juu kuelekea kwenye ofisi za Mkurugezni wa uhamiaji Papi Mndewa.
Alipofika karibu na mlango wa ofisi za Mkurugezi; Honda akasita kwenda zaidi akarudi nyuma kidogo akaangalia kushoto na kulia, hakuona mtu.
Kumbukumbu ya picha alioiona mezani kwa mhudumu wa mgahawa wa Tunde ikajijenga tena kichwani kwake.
Na hapo akajaribu kutazama tena ni wapi alipopigwa picha na mpigaji alipiga kwa kulenga kona akitokea upande gani!!
Hatimae macho yake yakatua kwenye kona iliotenganisha ofisi ya Balozi na chumba cha mawasiliano.
Konani pale kulikuwa kuna kamera ndogo mbili za usalama.
Macho yake akayahamishia tena kwenye kona iliotumika kutenganisha ofisi ya balozi na Mkurugenzi.
Tofauti na kona ya mwanzo yenye kamera mbili zilizofungwa pamoja, kona hii ilikuwa na kamera moja tu ambayo hata yeye alijua ilikuwepo na kona nyingine pia ilikuwa na kamera moja na ndivyo ilitakiwa iwe kila siku.
Alah!!!
Kamera ya pili ilitoka wapi na kwanini ilikuwa pale na ilikuwa na faida gani!!
Makubwa jama!!
Honda aliweka kituo kichwani kwake kumaanisha amefikia mwisho wa kufikiri wakati huo.
Wakati akitaka kufungua mlango wa mkurugenzi,mlango ukafunguliwa haraka akarudi nyuma.
Macho yao yakagongana.
Alikuwa ni mkurugenzi ambae alikuwa anataka kutoka kwenda kwake.
“Honda!!” aliita kwa kushangaa Mkurugenzi.
Honda akamwonyesha ishara warudi ofisini.
“Aisee nilijua nimeshakupoteza komredi” ndilo aliloweza kusema Mkurugenzi huku akimtizama Honda kama asieamini uwepo wake pale.
“Sio kunipoteza tu, hata uhai ningeupoteza na usingeniona kabisa” alisema Honda huku akikaa juu ya meza na kubaki wakitazamana kwa sekunde kadhaa.
“Nilijua wale jamaa watakuwa si watu wazuri japo kuwaingilia kiharaka vile kungeleta mkanganyiko wa kidiplomasia!!” alisema kwa masikitiko Mkurugenzi Papi Mndewa huku akitupa gazeti mezani pale alipokuwa amekaa Honda.
Honda alilitizama gazeti lile kisha akatabasamu.
“Kwani limeshatoka?” akauliza Honda bila kujishugulisha kulichukua mana ukurasa wa mbele ulikuwa umepambwa picha yake.
Picha ile haikumstua mana alishaiona tangu akiwa Tunde.
“Kwani linatoka lini hili gazeti mbona limesambaa sana!!” akauliza Honda.
“Nimeletewa na mtu wetu alieko huko linakopikwa na linatoka kesho.” Alijibu Papi.
“Kwani ilikuwaje!!” aliuliza Papi.
“Ni hadithi ndefu kidogo komredi ila kifupi tunazungukwa na watu wenye akili na ujuzi pia lakini ni lazima tupambane, na mchawi wetu wa kwanza anaanzia hapa hapa,unaionaje hiyo picha hapo?” alimalizia kwa swali Honda.
“ulipigwa wakati ukiingia hapa ofisni. Nimefikiria sana kuhusu mtu aliepiga picha hii na..!” Papi hakumalizia kauli yake alikatishwa na Honda.
“Picha haijapigwa na kamera ya mtu ila imepigwa kamera ilioko humu, lakini swali la kujiuliza, imewekwa lini na nani alieiweka?” akauliza Honda na kuacha swali lile likiambaa kichwani mwa Papi Mndewa.
Ukapita ukimya kidogo!
“Hii hatari sasa!!” alisema Papi huku dhahiri akionekana kuzama kwenye tafakuri!!
“Komredi mmefikia wapi na nyie!” alisema Honda.
“kiukweli tumeshindwa kujua kilichosababisha mawasiliano kukatika wakati balozi aliposhambuliwa. Tumejaribu kupitia kamera na miundo yote ya usalama ili kuona ni wapi hujuma ilianzia,lakini kote kulikuwa shwari aisee na nimeagiza baada ya kumsafirisha Balozi basi tuanze uchunguzi upya mana kuna ukakasi pahali” alimaliza kueleza Papi.
Honda akazishusha pumzi kwa mkupuo.
“Hali ni tete, lakini hili sakata litaisha, ikishindikana basi tutaomba makao makuu watuongezee nguvu” alisema Honda.
“Japo naamini hujashindwa lakini ikifikia huko tutakuwa hatuna namna!” alisema Papi.
“mmh wale vijana wa kitengo cha usalama wapo wangapi vile!!” alihoji Honda huku dhahiri akionekana kuwa na hisia za kumbukumbu.
“wapo watatu Komredi!!” alijibu Papi.
“Basi jicho lako lianzie hapo Komredi” Honda alimwambia Mkurugenzi wake!
Papi akatikisa kichwa bila kutoa sauti na hilo lilimaanisha tayari uchunguzi dhidi yao umeanza.
“Ok naomba unifikishe ofisini kwa Balozi kuna kitu nahitaji kutazama.” Alipokwisha kusema hivyo tayari miguu yao ilianza kufanya harakati za kuondoka ndani ya kile chumba.
Dakika moja badae wote walikuwa wanatazama tundu la risasi lilokuwa limejenga nyufa kadhaa kwenye kioo.
“Mdunguaji!!” alijisemea Honda huku taratibu akisogea lilipokuwa dirisha.
“ina maana hili pazia lingekuwa limerudishiwa basi mdunguaji angekosa shabaha” alisema tena taratibu Honda huku akishika tundu la risasi ilipopita.
Moja ya sifa kubwa ya kubwa ya Honda ni kutambua ukubwa wa vipenyo vya risasi na aina za silaha.
Hata hapo alijua.
“Hii ni Lapua Magnum bila Shaka” alisema Honda huku akimgeukia papi.
“Yes!! Kitengo kimethibitisha aina hiyo ya risasi na silaha ilikotoka.” Papi alijibu swali la kijana wake.
“Lakini kwa nilivyoona siku ile kabla sijakamatwa hili pazia lilikuwa limerudishiwa makusudi kabisa na nadhani wewe ungechunguza pia aliefanya usafi siku hiyo Mkuu au!” Honda alitoa mawazo yake kwa mtindo wa kuhoji.
“Hilo pia litafanyiwa kazi na sikuwa nimeliwaza kabisa komredi” alisema Papi huku akigonga tano kuashiria amekubali mawazo ya kijana wake ambae tangu wajuane walifanya kazi kwa ukaribu kiasi wakajikuta ni kama wanalingana wadhifa.
“Kile chumba pale ghorofani kinaweza kunifikisha kwa muuaji wa Balozi” alisema Honda huku akinyooshea kidole upande wa pili kulikokuwa na ghorofa kubwa na ndefu.
Ukimya ukapita.
Naendela na majukumu komredi ila usiponiona siku tatu pale ndani kwa Bulembo kuna kipanya nimekihifadhi pale kakichukue kinaweza kukufikisha nilipoishia” alisema Honda huku akianza kutoka pale ofisini.
Kitu kimoja ambacho watu hawa hawakujua ni kuwa kulikuwa na mtu mwingine aliewasikia walichokua wanazungumza.
Lakini kwao ni kama kiza hakuna walichojua.
****
Sajini Kebu alikuwa ametulia kimya huku akiwaza namna alivyonusurika kusombwa na maji yaliokuwa yanapita chini ya daraja alilitupiwamo na Honda.
Kimoyomoyo alihusudu uwezo wa akili wa mtanzania yule.
Sajini kebu akageuza macho yake kushoto kwake akakutana na jicho la Kojo ambae waliunganishwa pamoja baada ya vijana wa Kebu kuadhibiwa na Honda; hivyo sasa alikuwa ameungana na kundi la Kizibo na Kojo.
Aliona jinsi uso wa Kojo ulivyopasuka bila mpangilio.
“Umesema hii kazi ya yule bwege sio!!” aliuliza Sajini Kebu.
Swali lile lilionekana kumkera Kojo ila hakujibu akabaki kutazama pembeni.
“Bwana yule ananitesea rafiki yangu aisee” alidakia Kizibo aliekuwa amekaa kwenye kiti cha dereva.
“Hebu nipelekeni nikapumzike kwa mrembo wangu nikitoka huko risasi za kichwa zitammaliza Honda!!” alisema Sajini Kebu huku akiegemea kiti cha abiria alichokuwa amekalia.
Gari ikawashwa na kuondoka kuelekea viunga vya mji wa Gombe pembeni kidogo ya mji wa Kinshasa.
Ni kwa kuwa hawakujua lijalo halijawahi kujulikana kamwe.
Na kama walidhani wanaenda kupumzika walikosea sana
*****
Shusha komenti yako tafadhali, usipite kimya
RIWAYA: MPANGO WA CONGO
SEHEMU YA 14
Zilipita dakika kadhaa ndipo alipohisi kuna hali ya tofauti kutoka pale alipokuwa amelala.
Mwili hakuwa na nguvu lakini alisikia joto jingi huku akianza kupaliwa na alipofumbua macho akakutana na wingu la moshi mzito.
Nyumba ilikuwa inaungua!!.
Akajaribu kuinuka ila hakuwa na nguvu,akajaribu tena akashindwa.
Akakata tamaa na tayari alisikia mmomonyoko wa mabati kutokea huko vyumbani.
Kifo kilinusa pua za Solomoni Bukaba.
****
“Yule boya kakuotea leo aisee” alisema bwana mmoja mrefu aliekuwa anaendesha gari kwa kasi kutoka lango lango huku akipishana na magari na baadhi ya raia waliokuwa wameanza kujazana barabarani kushangaa moto mkubwa uliokumba baadhi ya nyumba zilizokuwa zimepakana na nyumba ya Solomoni Bukaba.
“Ndio mana kitengo kina Helper hasa killer akishindwa” alisema binti.
“Wapi sasa” aliuliza yule bwana.
“Club D nishushe pumzi” alijibu binti huku akiegemea kwenye kiti.
“mmh nadhani urudi nyumbani uoge” alishauri bwana dereva.
“ Haina shaka”
Gari ilichochewa moto.
****
..NCHINI CONGO..
Honda alihakikisha maelezo aliopewa na mateka wake yamemkaa sawia na hakutaka kuendelea kuhoji zaidi kwa wakati huo mana hakutaka kupoteza muda zaidi kwa kuwa alijua hapo ndipo ukomo wa ukweli kutoka kwa yule mateka na zaidi ya hapo ni kwa jasho na damu ndo ukweli atapata au kukosa kabisa.
Hakutaka kucheza bahati na sibu na muda.
Lazima amtafute X ambae kwa mujibu wa marehemu Bulembo ni Mtanzania na pia ni Club lakini kwa maelezo ya mateka; ndie aliewatuma wamkamate.
Akabaki na maswali kadhaa hivi.
Je X inahusu watu wangapi ama inahusu mtu mmoja?
Hakuwa na jibu.
Akajizoa zoa kutoka pale alipokuwa kisha akamsogelea mateka wake
“Kwanini mnamuita X?” aliuliza Honda Makubi.
Mateka akatoa cheko la kebehi kisha akajibu;
“Kwa sababu hafahamiki na hajulikani hata kwa sura!!”
“Duh!!” akaguna Honda kisha akaendelea kumsikiliza mateka wake.
“Kwa hiyo uliniona mjinga kukwambia tumetumwa na Mr X? au ulidhani ningemfahamu ninge….” Mateka hakumaliza kauli yake akajikuta anaelea hewani huku akishindwa kujitetea sababu ya kufungwa kamba ngumu kwenye kiti.
Mateka hakuwa na namna akasambaratika chini kama zigo la maharage mabichi.
Honda alijua kuna sababu za kuambiwa bila kukurukakara mwanzo na sababu aliipata na hakuwa tayari kuendelea kudhihakiwa hivyo akamtandika teke kali yule mateka lililomwacha akiwa hana msaada huko alikoangukia.
Honda akamwinua kisha akamshika kosi wa shati lake na kumvutia kwake wakawa wakitazamana kwa karibu.
“Nikirudi utanieleza aba,cha,da zote unazozijua Kimburu wewe” alichimba mkwara Honda kisha akamwachia na kukusanya vilivyo vyake na muhimu akavitia kwenye kwenye mkoba na kuuvaa kisha akatoka na kufunga milango yote vizuri na kuruka ukuta na kutokomea kuwahi pahali.
****
Kiza kilipoanza kuingia, Honda alikuwa nje ya ubalozi wa Tanzania nchini Congo.
Alikuwa amevaa kofia ya pama na suti matata iliomkaa vyema mwilini na kubadilisha mwonekano wake kwa kiasi kikubwa.
Wakati huu alivaa suti kwa sababu kwa waliomzoea kamwe hawakuwahi kumuona akiwa amevaa suti.
Mkononi alishika mkoba mweusi ambao alijua kabisa una uhumimu mkubwa licha ya kuhifadhi vitu asivyovifahamu maana yake.
Tayari wafanyakazi wengi walikuwa wameanza kurudi makwao.
Muda bado ulikuwa unaruhusu kwa watu wenye dharura kuingia na kutoka pale ubalozini kwa wakati huo.
Alijichanganya na watu hatimae alifanikiwa kuingia hadi mapokezi na bahati bado ilikuwa upande wake,mapokezi kulikuwa na watu kadhaa huku sehemu ya kupumzika kukiwa na watu wengine waliokuwa wakingoja huduma.
Akatumia nafasi ile kwa wafanyakazi kuwa bize akapita na kupanda juu kuelekea kwenye ofisi za Mkurugezni wa uhamiaji Papi Mndewa.
Alipofika karibu na mlango wa ofisi za Mkurugezi; Honda akasita kwenda zaidi akarudi nyuma kidogo akaangalia kushoto na kulia, hakuona mtu.
Kumbukumbu ya picha alioiona mezani kwa mhudumu wa mgahawa wa Tunde ikajijenga tena kichwani kwake.
Na hapo akajaribu kutazama tena ni wapi alipopigwa picha na mpigaji alipiga kwa kulenga kona akitokea upande gani!!
Hatimae macho yake yakatua kwenye kona iliotenganisha ofisi ya Balozi na chumba cha mawasiliano.
Konani pale kulikuwa kuna kamera ndogo mbili za usalama.
Macho yake akayahamishia tena kwenye kona iliotumika kutenganisha ofisi ya balozi na Mkurugenzi.
Tofauti na kona ya mwanzo yenye kamera mbili zilizofungwa pamoja, kona hii ilikuwa na kamera moja tu ambayo hata yeye alijua ilikuwepo na kona nyingine pia ilikuwa na kamera moja na ndivyo ilitakiwa iwe kila siku.
Alah!!!
Kamera ya pili ilitoka wapi na kwanini ilikuwa pale na ilikuwa na faida gani!!
Makubwa jama!!
Honda aliweka kituo kichwani kwake kumaanisha amefikia mwisho wa kufikiri wakati huo.
Wakati akitaka kufungua mlango wa mkurugenzi,mlango ukafunguliwa haraka akarudi nyuma.
Macho yao yakagongana.
Alikuwa ni mkurugenzi ambae alikuwa anataka kutoka kwenda kwake.
“Honda!!” aliita kwa kushangaa Mkurugenzi.
Honda akamwonyesha ishara warudi ofisini.
“Aisee nilijua nimeshakupoteza komredi” ndilo aliloweza kusema Mkurugenzi huku akimtizama Honda kama asieamini uwepo wake pale.
“Sio kunipoteza tu, hata uhai ningeupoteza na usingeniona kabisa” alisema Honda huku akikaa juu ya meza na kubaki wakitazamana kwa sekunde kadhaa.
“Nilijua wale jamaa watakuwa si watu wazuri japo kuwaingilia kiharaka vile kungeleta mkanganyiko wa kidiplomasia!!” alisema kwa masikitiko Mkurugenzi Papi Mndewa huku akitupa gazeti mezani pale alipokuwa amekaa Honda.
Honda alilitizama gazeti lile kisha akatabasamu.
“Kwani limeshatoka?” akauliza Honda bila kujishugulisha kulichukua mana ukurasa wa mbele ulikuwa umepambwa picha yake.
Picha ile haikumstua mana alishaiona tangu akiwa Tunde.
“Kwani linatoka lini hili gazeti mbona limesambaa sana!!” akauliza Honda.
“Nimeletewa na mtu wetu alieko huko linakopikwa na linatoka kesho.” Alijibu Papi.
“Kwani ilikuwaje!!” aliuliza Papi.
“Ni hadithi ndefu kidogo komredi ila kifupi tunazungukwa na watu wenye akili na ujuzi pia lakini ni lazima tupambane, na mchawi wetu wa kwanza anaanzia hapa hapa,unaionaje hiyo picha hapo?” alimalizia kwa swali Honda.
“ulipigwa wakati ukiingia hapa ofisni. Nimefikiria sana kuhusu mtu aliepiga picha hii na..!” Papi hakumalizia kauli yake alikatishwa na Honda.
“Picha haijapigwa na kamera ya mtu ila imepigwa kamera ilioko humu, lakini swali la kujiuliza, imewekwa lini na nani alieiweka?” akauliza Honda na kuacha swali lile likiambaa kichwani mwa Papi Mndewa.
Ukapita ukimya kidogo!
“Hii hatari sasa!!” alisema Papi huku dhahiri akionekana kuzama kwenye tafakuri!!
“Komredi mmefikia wapi na nyie!” alisema Honda.
“kiukweli tumeshindwa kujua kilichosababisha mawasiliano kukatika wakati balozi aliposhambuliwa. Tumejaribu kupitia kamera na miundo yote ya usalama ili kuona ni wapi hujuma ilianzia,lakini kote kulikuwa shwari aisee na nimeagiza baada ya kumsafirisha Balozi basi tuanze uchunguzi upya mana kuna ukakasi pahali” alimaliza kueleza Papi.
Honda akazishusha pumzi kwa mkupuo.
“Hali ni tete, lakini hili sakata litaisha, ikishindikana basi tutaomba makao makuu watuongezee nguvu” alisema Honda.
“Japo naamini hujashindwa lakini ikifikia huko tutakuwa hatuna namna!” alisema Papi.
“mmh wale vijana wa kitengo cha usalama wapo wangapi vile!!” alihoji Honda huku dhahiri akionekana kuwa na hisia za kumbukumbu.
“wapo watatu Komredi!!” alijibu Papi.
“Basi jicho lako lianzie hapo Komredi” Honda alimwambia Mkurugenzi wake!
Papi akatikisa kichwa bila kutoa sauti na hilo lilimaanisha tayari uchunguzi dhidi yao umeanza.
“Ok naomba unifikishe ofisini kwa Balozi kuna kitu nahitaji kutazama.” Alipokwisha kusema hivyo tayari miguu yao ilianza kufanya harakati za kuondoka ndani ya kile chumba.
Dakika moja badae wote walikuwa wanatazama tundu la risasi lilokuwa limejenga nyufa kadhaa kwenye kioo.
“Mdunguaji!!” alijisemea Honda huku taratibu akisogea lilipokuwa dirisha.
“ina maana hili pazia lingekuwa limerudishiwa basi mdunguaji angekosa shabaha” alisema tena taratibu Honda huku akishika tundu la risasi ilipopita.
Moja ya sifa kubwa ya kubwa ya Honda ni kutambua ukubwa wa vipenyo vya risasi na aina za silaha.
Hata hapo alijua.
“Hii ni Lapua Magnum bila Shaka” alisema Honda huku akimgeukia papi.
“Yes!! Kitengo kimethibitisha aina hiyo ya risasi na silaha ilikotoka.” Papi alijibu swali la kijana wake.
“Lakini kwa nilivyoona siku ile kabla sijakamatwa hili pazia lilikuwa limerudishiwa makusudi kabisa na nadhani wewe ungechunguza pia aliefanya usafi siku hiyo Mkuu au!” Honda alitoa mawazo yake kwa mtindo wa kuhoji.
“Hilo pia litafanyiwa kazi na sikuwa nimeliwaza kabisa komredi” alisema Papi huku akigonga tano kuashiria amekubali mawazo ya kijana wake ambae tangu wajuane walifanya kazi kwa ukaribu kiasi wakajikuta ni kama wanalingana wadhifa.
“Kile chumba pale ghorofani kinaweza kunifikisha kwa muuaji wa Balozi” alisema Honda huku akinyooshea kidole upande wa pili kulikokuwa na ghorofa kubwa na ndefu.
Ukimya ukapita.
Naendela na majukumu komredi ila usiponiona siku tatu pale ndani kwa Bulembo kuna kipanya nimekihifadhi pale kakichukue kinaweza kukufikisha nilipoishia” alisema Honda huku akianza kutoka pale ofisini.
Kitu kimoja ambacho watu hawa hawakujua ni kuwa kulikuwa na mtu mwingine aliewasikia walichokua wanazungumza.
Lakini kwao ni kama kiza hakuna walichojua.
****
Sajini Kebu alikuwa ametulia kimya huku akiwaza namna alivyonusurika kusombwa na maji yaliokuwa yanapita chini ya daraja alilitupiwamo na Honda.
Kimoyomoyo alihusudu uwezo wa akili wa mtanzania yule.
Sajini kebu akageuza macho yake kushoto kwake akakutana na jicho la Kojo ambae waliunganishwa pamoja baada ya vijana wa Kebu kuadhibiwa na Honda; hivyo sasa alikuwa ameungana na kundi la Kizibo na Kojo.
Aliona jinsi uso wa Kojo ulivyopasuka bila mpangilio.
“Umesema hii kazi ya yule bwege sio!!” aliuliza Sajini Kebu.
Swali lile lilionekana kumkera Kojo ila hakujibu akabaki kutazama pembeni.
“Bwana yule ananitesea rafiki yangu aisee” alidakia Kizibo aliekuwa amekaa kwenye kiti cha dereva.
“Hebu nipelekeni nikapumzike kwa mrembo wangu nikitoka huko risasi za kichwa zitammaliza Honda!!” alisema Sajini Kebu huku akiegemea kiti cha abiria alichokuwa amekalia.
Gari ikawashwa na kuondoka kuelekea viunga vya mji wa Gombe pembeni kidogo ya mji wa Kinshasa.
Ni kwa kuwa hawakujua lijalo halijawahi kujulikana kamwe.
Na kama walidhani wanaenda kupumzika walikosea sana
*****
Shusha komenti yako tafadhali, usipite kimya
RIWAYA: MPANGO WA CONGO
SEHEMU YA 14
Zilipita dakika kadhaa ndipo alipohisi kuna hali ya tofauti kutoka pale alipokuwa amelala.
Mwili hakuwa na nguvu lakini alisikia joto jingi huku akianza kupaliwa na alipofumbua macho akakutana na wingu la moshi mzito.
Nyumba ilikuwa inaungua!!.
Akajaribu kuinuka ila hakuwa na nguvu,akajaribu tena akashindwa.
Akakata tamaa na tayari alisikia mmomonyoko wa mabati kutokea huko vyumbani.
Kifo kilinusa pua za Solomoni Bukaba.
****
“Yule boya kakuotea leo aisee” alisema bwana mmoja mrefu aliekuwa anaendesha gari kwa kasi kutoka lango lango huku akipishana na magari na baadhi ya raia waliokuwa wameanza kujazana barabarani kushangaa moto mkubwa uliokumba baadhi ya nyumba zilizokuwa zimepakana na nyumba ya Solomoni Bukaba.
“Ndio mana kitengo kina Helper hasa killer akishindwa” alisema binti.
“Wapi sasa” aliuliza yule bwana.
“Club D nishushe pumzi” alijibu binti huku akiegemea kwenye kiti.
“mmh nadhani urudi nyumbani uoge” alishauri bwana dereva.
“ Haina shaka”
Gari ilichochewa moto.
****
..NCHINI CONGO..
Honda alihakikisha maelezo aliopewa na mateka wake yamemkaa sawia na hakutaka kuendelea kuhoji zaidi kwa wakati huo mana hakutaka kupoteza muda zaidi kwa kuwa alijua hapo ndipo ukomo wa ukweli kutoka kwa yule mateka na zaidi ya hapo ni kwa jasho na damu ndo ukweli atapata au kukosa kabisa.
Hakutaka kucheza bahati na sibu na muda.
Lazima amtafute X ambae kwa mujibu wa marehemu Bulembo ni Mtanzania na pia ni Club lakini kwa maelezo ya mateka; ndie aliewatuma wamkamate.
Akabaki na maswali kadhaa hivi.
Je X inahusu watu wangapi ama inahusu mtu mmoja?
Hakuwa na jibu.
Akajizoa zoa kutoka pale alipokuwa kisha akamsogelea mateka wake
“Kwanini mnamuita X?” aliuliza Honda Makubi.
Mateka akatoa cheko la kebehi kisha akajibu;
“Kwa sababu hafahamiki na hajulikani hata kwa sura!!”
“Duh!!” akaguna Honda kisha akaendelea kumsikiliza mateka wake.
“Kwa hiyo uliniona mjinga kukwambia tumetumwa na Mr X? au ulidhani ningemfahamu ninge….” Mateka hakumaliza kauli yake akajikuta anaelea hewani huku akishindwa kujitetea sababu ya kufungwa kamba ngumu kwenye kiti.
Mateka hakuwa na namna akasambaratika chini kama zigo la maharage mabichi.
Honda alijua kuna sababu za kuambiwa bila kukurukakara mwanzo na sababu aliipata na hakuwa tayari kuendelea kudhihakiwa hivyo akamtandika teke kali yule mateka lililomwacha akiwa hana msaada huko alikoangukia.
Honda akamwinua kisha akamshika kosi wa shati lake na kumvutia kwake wakawa wakitazamana kwa karibu.
“Nikirudi utanieleza aba,cha,da zote unazozijua Kimburu wewe” alichimba mkwara Honda kisha akamwachia na kukusanya vilivyo vyake na muhimu akavitia kwenye kwenye mkoba na kuuvaa kisha akatoka na kufunga milango yote vizuri na kuruka ukuta na kutokomea kuwahi pahali.
****
Kiza kilipoanza kuingia, Honda alikuwa nje ya ubalozi wa Tanzania nchini Congo.
Alikuwa amevaa kofia ya pama na suti matata iliomkaa vyema mwilini na kubadilisha mwonekano wake kwa kiasi kikubwa.
Wakati huu alivaa suti kwa sababu kwa waliomzoea kamwe hawakuwahi kumuona akiwa amevaa suti.
Mkononi alishika mkoba mweusi ambao alijua kabisa una uhumimu mkubwa licha ya kuhifadhi vitu asivyovifahamu maana yake.
Tayari wafanyakazi wengi walikuwa wameanza kurudi makwao.
Muda bado ulikuwa unaruhusu kwa watu wenye dharura kuingia na kutoka pale ubalozini kwa wakati huo.
Alijichanganya na watu hatimae alifanikiwa kuingia hadi mapokezi na bahati bado ilikuwa upande wake,mapokezi kulikuwa na watu kadhaa huku sehemu ya kupumzika kukiwa na watu wengine waliokuwa wakingoja huduma.
Akatumia nafasi ile kwa wafanyakazi kuwa bize akapita na kupanda juu kuelekea kwenye ofisi za Mkurugezni wa uhamiaji Papi Mndewa.
Alipofika karibu na mlango wa ofisi za Mkurugezi; Honda akasita kwenda zaidi akarudi nyuma kidogo akaangalia kushoto na kulia, hakuona mtu.
Kumbukumbu ya picha alioiona mezani kwa mhudumu wa mgahawa wa Tunde ikajijenga tena kichwani kwake.
Na hapo akajaribu kutazama tena ni wapi alipopigwa picha na mpigaji alipiga kwa kulenga kona akitokea upande gani!!
Hatimae macho yake yakatua kwenye kona iliotenganisha ofisi ya Balozi na chumba cha mawasiliano.
Konani pale kulikuwa kuna kamera ndogo mbili za usalama.
Macho yake akayahamishia tena kwenye kona iliotumika kutenganisha ofisi ya balozi na Mkurugenzi.
Tofauti na kona ya mwanzo yenye kamera mbili zilizofungwa pamoja, kona hii ilikuwa na kamera moja tu ambayo hata yeye alijua ilikuwepo na kona nyingine pia ilikuwa na kamera moja na ndivyo ilitakiwa iwe kila siku.
Alah!!!
Kamera ya pili ilitoka wapi na kwanini ilikuwa pale na ilikuwa na faida gani!!
Makubwa jama!!
Honda aliweka kituo kichwani kwake kumaanisha amefikia mwisho wa kufikiri wakati huo.
Wakati akitaka kufungua mlango wa mkurugenzi,mlango ukafunguliwa haraka akarudi nyuma.
Macho yao yakagongana.
Alikuwa ni mkurugenzi ambae alikuwa anataka kutoka kwenda kwake.
“Honda!!” aliita kwa kushangaa Mkurugenzi.
Honda akamwonyesha ishara warudi ofisini.
“Aisee nilijua nimeshakupoteza komredi” ndilo aliloweza kusema Mkurugenzi huku akimtizama Honda kama asieamini uwepo wake pale.
“Sio kunipoteza tu, hata uhai ningeupoteza na usingeniona kabisa” alisema Honda huku akikaa juu ya meza na kubaki wakitazamana kwa sekunde kadhaa.
“Nilijua wale jamaa watakuwa si watu wazuri japo kuwaingilia kiharaka vile kungeleta mkanganyiko wa kidiplomasia!!” alisema kwa masikitiko Mkurugenzi Papi Mndewa huku akitupa gazeti mezani pale alipokuwa amekaa Honda.
Honda alilitizama gazeti lile kisha akatabasamu.
“Kwani limeshatoka?” akauliza Honda bila kujishugulisha kulichukua mana ukurasa wa mbele ulikuwa umepambwa picha yake.
Picha ile haikumstua mana alishaiona tangu akiwa Tunde.
“Kwani linatoka lini hili gazeti mbona limesambaa sana!!” akauliza Honda.
“Nimeletewa na mtu wetu alieko huko linakopikwa na linatoka kesho.” Alijibu Papi.
“Kwani ilikuwaje!!” aliuliza Papi.
“Ni hadithi ndefu kidogo komredi ila kifupi tunazungukwa na watu wenye akili na ujuzi pia lakini ni lazima tupambane, na mchawi wetu wa kwanza anaanzia hapa hapa,unaionaje hiyo picha hapo?” alimalizia kwa swali Honda.
“ulipigwa wakati ukiingia hapa ofisni. Nimefikiria sana kuhusu mtu aliepiga picha hii na..!” Papi hakumalizia kauli yake alikatishwa na Honda.
“Picha haijapigwa na kamera ya mtu ila imepigwa kamera ilioko humu, lakini swali la kujiuliza, imewekwa lini na nani alieiweka?” akauliza Honda na kuacha swali lile likiambaa kichwani mwa Papi Mndewa.
Ukapita ukimya kidogo!
“Hii hatari sasa!!” alisema Papi huku dhahiri akionekana kuzama kwenye tafakuri!!
“Komredi mmefikia wapi na nyie!” alisema Honda.
“kiukweli tumeshindwa kujua kilichosababisha mawasiliano kukatika wakati balozi aliposhambuliwa. Tumejaribu kupitia kamera na miundo yote ya usalama ili kuona ni wapi hujuma ilianzia,lakini kote kulikuwa shwari aisee na nimeagiza baada ya kumsafirisha Balozi basi tuanze uchunguzi upya mana kuna ukakasi pahali” alimaliza kueleza Papi.
Honda akazishusha pumzi kwa mkupuo.
“Hali ni tete, lakini hili sakata litaisha, ikishindikana basi tutaomba makao makuu watuongezee nguvu” alisema Honda.
“Japo naamini hujashindwa lakini ikifikia huko tutakuwa hatuna namna!” alisema Papi.
“mmh wale vijana wa kitengo cha usalama wapo wangapi vile!!” alihoji Honda huku dhahiri akionekana kuwa na hisia za kumbukumbu.
“wapo watatu Komredi!!” alijibu Papi.
“Basi jicho lako lianzie hapo Komredi” Honda alimwambia Mkurugenzi wake!
Papi akatikisa kichwa bila kutoa sauti na hilo lilimaanisha tayari uchunguzi dhidi yao umeanza.
“Ok naomba unifikishe ofisini kwa Balozi kuna kitu nahitaji kutazama.” Alipokwisha kusema hivyo tayari miguu yao ilianza kufanya harakati za kuondoka ndani ya kile chumba.
Dakika moja badae wote walikuwa wanatazama tundu la risasi lilokuwa limejenga nyufa kadhaa kwenye kioo.
“Mdunguaji!!” alijisemea Honda huku taratibu akisogea lilipokuwa dirisha.
“ina maana hili pazia lingekuwa limerudishiwa basi mdunguaji angekosa shabaha” alisema tena taratibu Honda huku akishika tundu la risasi ilipopita.
Moja ya sifa kubwa ya kubwa ya Honda ni kutambua ukubwa wa vipenyo vya risasi na aina za silaha.
Hata hapo alijua.
“Hii ni Lapua Magnum bila Shaka” alisema Honda huku akimgeukia papi.
“Yes!! Kitengo kimethibitisha aina hiyo ya risasi na silaha ilikotoka.” Papi alijibu swali la kijana wake.
“Lakini kwa nilivyoona siku ile kabla sijakamatwa hili pazia lilikuwa limerudishiwa makusudi kabisa na nadhani wewe ungechunguza pia aliefanya usafi siku hiyo Mkuu au!” Honda alitoa mawazo yake kwa mtindo wa kuhoji.
“Hilo pia litafanyiwa kazi na sikuwa nimeliwaza kabisa komredi” alisema Papi huku akigonga tano kuashiria amekubali mawazo ya kijana wake ambae tangu wajuane walifanya kazi kwa ukaribu kiasi wakajikuta ni kama wanalingana wadhifa.
“Kile chumba pale ghorofani kinaweza kunifikisha kwa muuaji wa Balozi” alisema Honda huku akinyooshea kidole upande wa pili kulikokuwa na ghorofa kubwa na ndefu.
Ukimya ukapita.
Naendela na majukumu komredi ila usiponiona siku tatu pale ndani kwa Bulembo kuna kipanya nimekihifadhi pale kakichukue kinaweza kukufikisha nilipoishia” alisema Honda huku akianza kutoka pale ofisini.
Kitu kimoja ambacho watu hawa hawakujua ni kuwa kulikuwa na mtu mwingine aliewasikia walichokua wanazungumza.
Lakini kwao ni kama kiza hakuna walichojua.
****
Sajini Kebu alikuwa ametulia kimya huku akiwaza namna alivyonusurika kusombwa na maji yaliokuwa yanapita chini ya daraja alilitupiwamo na Honda.
Kimoyomoyo alihusudu uwezo wa akili wa mtanzania yule.
Sajini kebu akageuza macho yake kushoto kwake akakutana na jicho la Kojo ambae waliunganishwa pamoja baada ya vijana wa Kebu kuadhibiwa na Honda; hivyo sasa alikuwa ameungana na kundi la Kizibo na Kojo.
Aliona jinsi uso wa Kojo ulivyopasuka bila mpangilio.
“Umesema hii kazi ya yule bwege sio!!” aliuliza Sajini Kebu.
Swali lile lilionekana kumkera Kojo ila hakujibu akabaki kutazama pembeni.
“Bwana yule ananitesea rafiki yangu aisee” alidakia Kizibo aliekuwa amekaa kwenye kiti cha dereva.
“Hebu nipelekeni nikapumzike kwa mrembo wangu nikitoka huko risasi za kichwa zitammaliza Honda!!” alisema Sajini Kebu huku akiegemea kiti cha abiria alichokuwa amekalia.
Gari ikawashwa na kuondoka kuelekea viunga vya mji wa Gombe pembeni kidogo ya mji wa Kinshasa.
Ni kwa kuwa hawakujua lijalo halijawahi kujulikana kamwe.
Na kama walidhani wanaenda kupumzika walikosea sana
*****
Shusha komenti yako tafadhali, usipite kimya