JATU ni Mr Kuku mwingine, ni swala la muda tu

Naona na huyu ameanza Tena na watu wanapenda kabisa.



Huyu yupo Kama kawa. Wajinga ndio waliwao.
 
Hapa wachache watakuelewa. Mtu hajui hata IPO ni nn na utaratibi wake ukoje lkn anaishia kusema ulichoandika ni uongo.

Jatu hawezi kuwa mr kuku hata siku moja coz hata ikitokea akafilisika basi kuna utaratibu wa wanahisa kulipwa stahiki zao baada ya creditors kulipwa.

Ni kwamba tu liquidity ya DSE ni ndogo sana. Nikinunua hisa leo nikaja kutaka kuziuza ni mpaka nisubiri mnunuaji atokee, lkn kwa Exchanges kama nairobi kdg ziko fasta.
 
thank you chief....
 
Mwaka jana nilipitia mchakato wao wote, kuanzia kujiunga mpaka mwisho. Nikagundua hawa jamaa ni "wezi wajanja".

Nikisema "wezi wajanja" namaanisha kwamba wao wanakuibia kwa kukuongezea "gharama" za kilimo kuanzia kujiunga nao, kukukodishia shamba, kukulimia, kukutunzia yaani mchakato mzima halafu mazao wananunua wenyewe kwa bei ya kukupiga. Mwishoni unaletewa kafaida kiduchu sana.

Nikaamua kufanya utafiti wangu binafsi na kugundua kwamba ukilima mwenyewe unapata faida kubwa sana ili mradi tu uwe na muda na ufuate utaalamu wa kilimo.

Kilimo kinahitaji muda na close supervision. Kama unao muda wa kutosha kilimo kinalipa mbaya sana.

Sasa wanaopigwa na JATU ni wale watu ambao wanapesa za kuwekeza kwenye kilimo lakini hawana muda wa kusimamia mashamba. Hao ndiyo JATU inawalenga na wanapigwa kweli kweli siyo mchezo.

JATU hawakupigi mazima bali wanakuletea faida ndogo sana tena sana. Mwisho wa siku wao ndiyo wanafaidika zaidi.
Akili kumkichwa.
 
Kwa makampuni unayoona kabisa yanavutia kuleta profit muda mzuri wa kununua hisa ni muda wa IPO (Initial public offering) coz hapo bei ya hisa inakua fixed. Lakini kpnd cha IPO kikiisha then bei ya hisa itakua inabadilika kutokana na market perfomance yake(manunuzi zaidi ya hisa yatapandisha hisa mauzo yataishusha)

Pia baada ya kununua hisa kuna dividends ambazo huwa zinatolewa lwa wanahisa kila baada ya robo mwaka, dividends hizo zinategemea na faida iliotengenezwa na kampuni muda huo. Kwa makampuni yalio makini huwa yanatoa target dividends then investor anakua anajua anategemea faida ya sh ngp, sijajua kama JATU wanafanya hivyo.


Hivyo basi kama unaamini JATU watatengeneza profit baadae basi muda mzuri wa kununua hisa zao ni huu.

Ni bora kufuatilia financial statement zao kwa miaka iliopita au kuomba ushauri kwa wataalamu ili kujua kama JATU ni chaguo sahihi kwako.


~NOT A FINANCIAL ADVICE
 
Huyu sio kwamba seeikali ilichukua fedha?
Angekua kasajiliwa dse kama jatu pesa za watu zingerudi. Haya mambo yana utaratibu wake, sasa mr kuku aliamka na idea akaanza moja kwa moja bila kufuatilia utaratibu wa kisheria ukoje. Na watu wasioelewa wakaendelea kumfuata.

Ni lazima serikali iweke elimu ya uwekezaji mashuleni ili kupunguza matukio kama haya.
 
JATU siyo kama ni kampuni ya kitapeli moja kwa moja, hapana, ila uwizi wao uko kwenye kukubambikizia bei kubwa sana za gharama za kilimo na hata mazao wananunua kwa bei ya chini sana.

Itoshe tu kusema kwamba JATU ni kampuni ya "kinyonyaji" sana. Mkulima analetewa kafaida kiduchu sana ukilinganisha na akilima mwenyewe.

Kama mtu una akili kichwani ni bora ulime mwenyewe na siyo kuwategemea hawa "wahuni".
 
Sasa wizi wao upo wapi hapo?🤣
Unalimiwa, unasimamiwa, wao ndo wanakupa soko sasa ulikuwa unataka hayo yafanyike kwa gharama za nani?

Vitu vingine si kuibiwa ni kutokujiongeza. Sawa sawa na mkeo asiye na kazi na wewe hutoi fedha za matumizi ila kila siku mnakula kuku na maziwa halafu baadae ufanye uchunguzi kisha ushtuke mkeo anakusaliti.
 
Serikali ina wajibu wa kutoa msaada kwa watu wa aina yake si kuchukua mtaji. Wanasheria wa uma hizi pia ni kazi zao.
 

Wacha wapigwe, mwisho wa siku watamchangia hela mtu aendeleze anasa zake!

Ndugu pekee huwezi mpa pesa akakulimia sembuse huu upuuzi, wacha wapigwe tu Hakuna namna!

Hivi hawa jamaa wana Kiwanga na madawa nini? Mbona watu wanafanganywa kirahisi sana?
 
Udogo na ukubwa wa faida unaupima kwa vigezo vipi? Ukinipa m100 yako nikawekeze shambani kwa gharama zangu kisha nikakurudishia m101 na mm nikachukua m29 ya faida unapimaje kuwa ni unyonyaji iwapo huna ushiriki katika utendaji?
 
Serikali ina wajibu wa kutoa msaada kwa watu wa aina yake si kuchukua mtaji. Wanasheria wa uma hizi pia ni kazi zao.
Kisheria hio haipo mkuu, kama sheria ikifuatwa basi hao member wa mr kuku ilibidi wawe jela coz hairuhusiwi raia yyt kushiriki kwenye michezo hii ya pyramid schemes, refer vitu kama PONZI

Kumbuka tu "Kutoijua sheria hakukupi guarantee yyt kuivunja"

Serikali inachoweza kufanya ni kutoa elimu kwa wananchi ili wajue uwekezaji upi ni sahihi na upi sio sahihi na pia kuwahi kuzifungia hizi taasisi zinazoelekea kuwa pyramid schemes kabla hazijaumiza wananchi zaidi ya hapo tutalaumu watu bure kwa kutojua kwetu.
 
Mwamba amerudi kwa Kasi mno baada ya Mwendazake.

Na anakula vichwa mbaya huko insta.

Watz huwa hatujifunzi kabisa.
Kama watu wanabeti na kuliwa na wanabeti tu na makampuni ya kubeti yote hayakosi wateja hata huyu kukumtu asilaumiwe.
 
Huyu kuku anafanya pyramid schemes au unanunua kuku anawagharamia na kuwauza kwa niaba?

Mm nikajua yeye amewekeza kwenye mabanda ya kisasa. Wewe mwanajamii nunua kuku yeye anafuga na kutafuta masoko

Pesa ikawa ya kutosha benki serikali ikatafuta sababu ikaipata kwenye sheria kuwa hizi pesa zinazowekwa ni nn?

Kama ni mauzo umelipa kodi? Kama ni mitaji wewe ni public company?

Pamoja na mapungufu ya kisheria serikali ilipaswa kumwonyesha njia sahihi ya kupita na si kuchukua mtaji kwa kisingizio cha sheria.
 
Huyu kuku anafanya pyramid schemes au unanunua kuku anawagharamia na kuwauza kwa niaba yako?
Iwe pyramid scheme au sio lakini kisheria masoko yote ya mitaji yapo regulated na taasisi maalum, wewe ukienda kinyume na sheria zilizopo kuhusu masoko ya mitaji inabidi uchukuliwe hatua.

Kwa mr kuku mtaji ni hao kuku wanaonunuliwa coz yy ndio business cycle yake inaanzia hapo. Inakuja kuonekana kama pyramid scheme kwenye namna wanayotumia kuongeza wanachama. Kuna utaratibu maalum inabidi ufuatwe na ndio maana masoko ya hisa yanakua na brokers. Kwa utaratibu wa mr kuku ya zamani inaonesha walioingia mwanzo ndio wanakua na profit kubwa kwa kuwaingiza wengine hapo ndio pyramid inapotokea
 
Naheshimu mawazo yako juu ya JATU, ila sikubaliani nayo! JATU analenga katika kukamilisha dhana ya kukusanya mtaji au mitaji ili awekeze, pamoja na hao wenye fedha zao, kwenye kilimo au eneo jingine lolote analodhani au watakalodhani, hao wachangiaji kuna TIJA. JATU anatafuta nguvu ya wengi ili kuondokana kwenye umasikini wa kipato (income poverty). Kwa siku za karibuni, dhana hiyo inatumiwa ma wale jamaa wa VANILLA VILLAGE wa Njombe. Umewasikia?
 
Kipigo kiko pale pale, wacha nikamate fuko la popcorns. Hamna hela nyepesi kmmmk

It is unfortunate kwamba watu wanategeka kwavile JATU wako listed kwenye DSE!!! Unaponunua hisa ni muhimu sana kuwachunguza management ya hiyo kampuni inayouza hizo hisa!!! DSE as is currently constituted haina watu wenye weledi wa kutosha kuzichunguza kampuni zinazoingia kwenye soko lao kuwa kweli wana vigezo vya kuweza kuwafaidisha wanahisa wao!!! Sidhani hata kama wanaweledi wa kuthibiti INSIDE TRADING kwenye soko lao!!!! Hapo ndio maana watu wanapigika kwani viongozi wa DSE wanapasisha PONZI schemes kama acceptable investors!!
 
Wewe ukienda kinyume na sheria zilizopo kuhusu masoko ya mitaji inabidi uchukuliwe hatua.
Hiyo ndo akili yaaani.

Unamuacha mtu anakusanya pesa za watu zikijaa ndo unagundua kuwa hajafata taratibu sheria ichukue mkondo wake unamchukulia hatua kwa kuchukua mtaji bila kuwarudishia wenye mtaji. Busara ya hali ya juu hiyo.
Wajinga ndo waliwao ila kama kuku ni tapeli basi yupo na ushirikiano na tapeli mwingine mkubwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…