Jay-Z, Rihanna na Lebron James watajwa kwenye orodha ya Forbes ya Mabilionea wa Dunia

na ukiwa na ndugu mabazazi hawataki hata kuona kaburi lako, wanakuchoma moto kisha majivu wanapeperusha.....ni ujinga tu kuwa na mabilioni ya pesa kiasi hicho na kuna watu jirani nawe wanateseka kwa njaa, hawana pa kulala wa mavazi.
💯💯💯💯 Hii ni kweli
 
Ohooo family money ni tamu sana ni kama kampuni ya chocolate ya koch family utaratibu wao ni mzuri sana duuh noma kwelikweli
 

Waliwahi kumweka jokate kwenye 30 under 36 kipindi anauza madaftari kariakoo.
 
Yale yale ya stori za vijiweni. Nimekwambia unitajie mmoja na kiasi anachomiliki unakuja maelezo meeengi. Nani kakwambia LVMH ni biashara ya familia? Utajiri wa Benard Arnault ni wake binafsi (personal fortune) sio utajiri wa LVMH. Unachanganya thamani ya Kampuni (market capitalization) na utajiri binafsi wa mtu ambaye ni Kiongozi wa hiyo kampuni.
 
Again, unachanganya utajiri wa eneo na utajiri wa watu binafsi. Kama ni hivyo basi hata Congo inapaswa kuwa na matajiri kwenye orodha ya dunia maana kuna raslimali nyingi sana za asili. Tafiti kwanza hizo tofauti kisha ndio uongee.
 
Wewe ndo unaleta story za vijiweni na unataka nikupe story za vijiweni, hao waarabu ni ngumu kujulikana ila effect ya hela yao inaonekana,

Sasa ukitaka nikutajie majina huoni unanilazimisha kukupa story za vijiweni?

Fuatilia Saudi National Bank imeinvest wapi ndo utaona effect ya hela za waarabu, hata elon musk alipotaka kuipeleka Tesla private mwaka 2018 alikua anapewa kiburi na funds za Saudi Arabia.

Hujui unachokiongelea af unaita story za kijiweni kisa huna information.

Benard Arnault percent kubwa ya utajiri wake ni share yake ya LVMH ambayo anaipata sababu ni kiongozi wa hio Family Business, sasa kama hata unakataa hilo ambalo google search ndg tu inakujibu basi naona napoteza tu mda wangu kukuquote. Na kwa taarifa yako watoto wake wanapigana vita balaa hadi media zinatangaza hilo ili mradi tu kuwa successor lkn jamaa kakomaa haachii kiti
 
Mkuu hujui hata unachoongea. Umedai kuna waarabu wana utajiri kuliko Forbes list. Nimekwambia unitajie unaanza kutaja benki, sasa benki ni mtu binafsi? Elon kutumia hela za waarabu sio kitu cha ajabu. Waarabu wamewekeza sana kwenye makampuni, masoko ya hisa na fedha Ulaya na US. Kitu ambacho kina-contradict point yako kwamba utajiri wa Europe na US sio halisi. Then kwa nini waarabu wanawekeza huko? Kwa nini wasinge-stick kwenye hayo mafuta yao?

Kama waarabu ni wagumu kujulikana utajiri wao uhakika kwamba wana utajiri kuliko waliotajwa na Forbes unaupata wapi?Kitu kingine ambacho inaelekea hujui ni kwamba kampuni zinazochimba mafuta kwenye nchi za kiarabu ni za Serikali na sio watu binafsi (mfano ARAMCO ya Saudi Arabia). Sasa hao matajiri wako wanatoka wapi hapo? Au ndio unahesabia utajiri wa ARAMCO ni utajiri wa mtu binafsi?

Narudia tena, LVMH SIO kampuni ya familia. Ni PLC (public liability company). Suala kwamba wanae Arnault wanagombania control ya LVMH haimaanishi ni kampuni binafsi. Inawezekana Arnault ana hisa nyingi (controlling shares) lakini hiyo haifanyi LVMH kuwa kampuni binafsi. Hata watoto wa Rupert Murdoch wanagombana kuhusu nani ataongoza Media Empire ya News Corp. Lakini News Corp sio kampuni ya familia ya Murdoch. Wana hisa nyingi tu humo.
 
Again, unachanganya utajiri wa eneo na utajiri wa watu binafsi. Kama ni hivyo basi hata Congo inapaswa kuwa na matajiri kwenye orodha ya dunia maana kuna raslimali nyingi sana za asili. Tafiti kwanza hizo tofauti kisha ndio uongee.
Nimesema vyanzo vya Utajiri wao sio maeneo ya utajiri wao.

Wewe unaniletea habari za Congo tena
 
Roc-boy and Roc-girl

"......How many billionaires come from the ROC Crib? I count 3, Me, Ye and Rih. Bron's a ROC boy so four Technically......" - JAY Z (from God Did)
Jay is very smart.... Yemwenyewe anasemaga from the pj to the pj, yan from the projects(marcy projects) to the private jet.... I am at the cap table, what the split is...

Me kwangu huwa ndio the best rapper alive... Ni vile tu jamaa yuko very lyrical kiasi kwamba hata mtu anaejua kingereza kikawaida hawezi elewa anasema nini ila wanaojua wanajua jay ni hatari sana... Kama God did wimbo umebebwa na yeye...
 
na ukiwa na ndugu mabazazi hawataki hata kuona kaburi lako, wanakuchoma moto kisha majivu wanapeperusha.....ni ujinga tu kuwa na mabilioni ya pesa kiasi hicho na kuna watu jirani nawe wanateseka kwa njaa, hawana pa kulala wa mavazi.
Hata waoteseka wameumbwa sawa tu na hao mabilionea isipokua vilema na wenye mapungufu mbalimbali

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Utajiri ni utajiri tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…