Johnny Sack
JF-Expert Member
- Jan 21, 2017
- 8,984
- 19,288
Kabis yaan ni hiyo ngono movieBongo muvi ilianza kufa walipoanza kuamini kuwa kila msichana mwenye sura nzuri anaweza kuigiza,kilichofuata ni magwiji kama Monalisa,Johari,Waridi kupotea taratibu na kuwaachia 'ngonomuvi' kuongoza jahazi.
u deserve my like mkuu...Bongo muvi ilianza kufa walipoanza kuamini kuwa kila msichana mwenye sura nzuri anaweza kuigiza,kilichofuata ni magwiji kama Monalisa,Johari,Waridi kupotea taratibu na kuwaachia 'ngonomuvi' kuongoza jahazi.
Mkuu, usichanganye SIRI YA MTUNGI na huo upuuzi unaoitwa Bongo Movie. Siri ya mtungi ilitengenezwa na jamaa waliotengeneza "yellow card" na "Neria". Kama unazijua hizo movie utakuwa umenielewa.Bongo movie hakuna kitu kabisa ila nitoe pongezi kwa waliofanya SIRI YA MTUNGI walijitahidi sana mastaa wenye majina makubwa walikuwa wachache,story na ujumbe ulieleweka,sauti na picha ni HD kabisa walifanya vizuri.
Umetoa mchango mubashara kabisaBongo movie imekufa sababu haiwaangalii watu wenye vipaji asilia vya kuigiza, yaani watu wabunifu. Bongo movie ilianza kufa mlipoanza kuangalia matako, mahips na sura kama kigezo cha kuwa muigizaji bora na ndio maana Sanaa yenu kwa kipindi hiki imekuwa kimbilio la malaya, huku mkiwaacha waigizaji wenye vipaji vya ukweli kisa hawana mwonekano na sasa hivi upande wa wanaume wamejaa mashombeshombe na wauma lips kuigiza hawajui, sanaa mmeiuwa wenyewe. Mimi huwa najiuliza hivi mtu kama LUPITA NYONGO angezaliwa Tanzania kweli angepewa nafasi ya kuigiza ktk hizi movie zetu za bongo, sasa muangalie huko Hollywood LUPITA sasa hivi anavyokimbiza, badilikeni angalieni vipaji na si mwonekano la sivyo mtaendelea kufeli.