Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 301,577
- 754,412
Msanii mkongwe muigizaji wa Bongo movie Jacob Steven JB, ametoa sababu ya bongo movie kudorora kwa sasa. Amedai bado haijafa ila inapitia kipindi cha mpito, na kinachoifanya ikafifia ni kutokana na kufanya movie zinazofanana kila mara na watazamaji kuzizoea na kuona haina jipya.
Ametolea mfano kipindi cha uchekeshaji cha Komedi kilivyoanza na watu wakawa wanajazana kwenye TV kutazama lakini baada ya kuzoeleka wakaipotezea na hata Nigeria movie zao zilikuwa zinapendwa sana lakini nao wana tatizo kama la Bongo
Amedai haitakufa ila watakuja wasanii wapya na kiufanya tofauiti.
Maneno ya kujifariji
Iko wapi taarab
Iko wapi reggae ya kibongo
Iko wapi rap ya kibongo
Uko wapi muziki wa dance
Hii ni enzi ya bongo fleva nayo itaondoka
Bongo movie itarudi lakini sio sasa bado sana na itarudi kivingine kabisa na watu wengine kabisa