Je!, adhabu aliyopewa refa Martin Sanya INAMTOSHA?

NGANU

JF-Expert Member
Joined
Oct 18, 2012
Posts
1,919
Reaction score
393
Wadau yule refa aliyechezesha mechi ya YANGA na COASTAL amefungiwa kuchezesha kwa muda wa mwaka 1, adhabu hii inatosha?
 
Yule wangemfuta kabisa,akafanye kazi nyingine
 
Inamtosha, ila wachukue na alvyopewa na aliowapa penalt ambayo hakuiona
 
Ningefurahi kama wangempoteza kwenye uwanja wa michezo ili labda ajaribu siasa ambako ubabaishaji ndo mwingi.
 
Soka la bongo ...hakuna mantiki ya kumfungia mwamuzi kwa kutoa maamuzi sahihi...it was clear mtu aliunawa mpira ndani ya 18...kama angewap penalt Yanga angefungiwa...?
 
wadau yule refa aliyechezesha mechi ya yanga na coastal amefungiwa kuchezesha kwa muda wa mwaka 1, adhabu hii inatosha?

yani kwa tff hii ya tenga, ingekuwa yanga kafungwa ile mechi huyu jamaa angefungiwa maisha!! Mpira wa bongo umejaa siasa bora tenga aondoke tuu ameharibu sana system ya soka, sijui hao waliomfungia saanya ni wasafi kiasi gani!!

Pia najiuliza sipati jibu labda wadau mtanisaidia, ile penati ingekuwa ndo yanga wamepewa ka dakika kama zile na wakasawazisha, je huyu jamaa angekutana na hii adhabu??
 
Na angepelekwa mahakamani kabisa afungwe miaka miwili kama rage, wanatwalibia soka hawa wahuni
 
Mwache akae kijiweni huo mwaka tuone kama atakula hzo pesa alizopewa na Bin Slum na Cmba
 
Ndio maana jamaa fulani anajiita Eddo Kumwembe alijitapa sana cku ya mechi kwa kuwa alijua timu lake lishatoa hongo.
 
maamuzi ya kijinga sana, maamuzi yamekaa kimahaba zaidi kuliko kimantiki
 
Hyu akiludi kucheza mechi za yanga hatuwezi endekeza mafisad wa soka
 
Mkuu Revocatus Kashaga hajafungiwa kwa ajili ya penati aliyotoa bali kushindwa kuumudu mchezo kwa muda wote.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Revocatus Kashaga hajafungiwa kwa ajili ya penati aliyotoa bali kushindwa kuumudu mchezo kwa muda wote.
 
Last edited by a moderator:
Kwanza mwandishi kichwa cha thread kimenipa utata,inaonesha wewe ni shabiki wa yanga,unaonaje kama hyo tittle labda ingekuwa katika muundo huu!"je adhabu aliyopewa mwamuzi Sanya ni sahihi?"

Mimi nitaanzia hapo kwenye hiyo tittle nilioipendekeza mwenyewe.Mwamuzi ni binadamu na makosa hayaepukiki katika utendaji wa majukumu yake ukizingatia tensheni kubwa ya mechi ilivyokuwa,sioni ni sabau gani TFF wameamua kumfungia mwamuzi Yule mwaka mmoja mbona waamuzi weng wa Tanzania ndio type zile zile,je watawafungia wangapi?najua hili limefanywa kwa kuwa victim wa mapungufu yale ni Yanga ambao ndio wanaihodhi TFF na hilo halina ubishi.
I feel sorry for the referees,soka la bongo kichefuchefu.....
 
Mwache akae kijiweni huo mwaka tuone kama atakula hzo pesa alizopewa na Bin Slum na Cmba

yule mwamuzi ni mwajiriwa wa jeshi la magereza hawez kufa njaa kwa kukosa hela mbuzi wanazopewa na TFF.
 
yule mwamuzi ni mwajiriwa wa jeshi la magereza hawez kufa njaa kwa kukosa hela mbuzi wanazopewa na TFF.

Kuchezesha mechi moja ni sh 240000 wakati mshahara wa askari ni sh zisizozidi 500000 take home kwa mwezi!
Adhabu ni sahihi ili liwe fundisho na kwa wengine lakini pia TFF waongeze dau walau iwe hata 1000000 ili kuwafanya marefa wasione tamaa ya kutaka kuhongwa maana watakuwa wanawaza wasije wakafungiwa na kuzikosa hizo 1M per mechi!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…