Je, ajiunge na SACCOSS apate mkopo au achukue mkopo BANK?

rikiboy

JF-Expert Member
Joined
Feb 19, 2017
Posts
21,952
Reaction score
43,265
Kuna ndugu yangu anataka kuchukua mkopo. Sasa anaomba ushauri je, ajiunge na SACCOSS apate mkopo au achukue mkopo BANK? Ni mkopo kama milioni 5 hivi

Please ushuari wako muhimu sana

=======


========

 
Kwanza anataka mkopo wa kiasi gani kwa ajili ya nini na anategemea kuulipaje na kwa muda gani.
 
Amua mwenyewe.

SACCOS

- Siyo sehemu ya kupata mkopo haraka, maana utahitaji kuwa mwanachama na kujiwekea akiba.

- Sometimes, riba yao yaweza kuwa kubwa kidogo maana kuna SACCOS kibao zinakopa bank.

- Unaweza Kupata Mkopo Bila Dhamana. Akiba yako ndio dhamana yako ( Unaruhusiwa kukopa mara 3 ya akiba yako )

BANK

- Riba Nafuu
- Kukopa Ni Faster Kidogo Kama Umekidhi Vigezo Vyao Hususani Dhamana
 
Kupata mkopo bank ni process...! Sio rahisi namna hyo
Halaf imekaa kiwiz wiz kinomaaaaaa.Kiwizi vibyaaaa snaaaaaaa.
Kuna siku wife aliomba niongozane nae akachukue mkopo bancABC.

Nikaenda nae nika cheel pemben nawasikiliza wanavyompa michanganu pale weeee.wife hesabu kidogo sio kipaji.Wakamwambia rate yao ya interest kuwa ni 30% kama sijasahau. Sasa 30% ikaonekana kama fare tu na mm huku pemben nikabonyeza calculator yangu.

Nikauliza marjesho kwa mwezi nikauliza time frane ya marejesho nikawapigia mahesabu wale ma banker halaf yakafuata maswal.Nadhan hawakutarajia .Biashara yetu ikaishia pale.

Sina uzoef sana na mikopo ya kibiashara lakin hii mikopo ya wafanyakazi ni WIZI WA MACHO MACHO. Shida zinawaendesha vibaya sana masikin hasa watumishi wa umma linapokuna suala la kukopa bank.NMB pia wapo.

NB
toka siku hiyo nikashauri wife ajiunge vikoba zilizo stable na utaratibu mzuri wa utunzaji pesa kwa mikopo yake hii ya kawaida ya 3m kushuka chini.
 
rikiboy

SACCOS ni sehemu nzuri ya kukopa au mtu ambaye hana vigezo vya kukopa benki; wasichokijua wanachama wa SACCOS in kuwa hakuna mkopo ghali kama wa SACCOS.

Ili upate mkopo wa kiasi fulani lazima na wewe uwe na akiba mfano moja ya tatu ya mkopo unaomba; maana yake sehemu ya mkopo ni pesa yako mwenyewe na unailipia riba.

Ukikopa Shs 6,000,000 kwa riba ya 20% utalipa riba ya TZS 1,200,000
Ukikopa SACCOS TZS 6,000,000 kati ya hizo pesa TZS 2,000,000 itakuwa ni akiba yako hivyo kiuhalisia umekopeshwa TZS 4,000,000 ambazo utalipia riba ya TZS 1,200,000 sawa na 30%. Hivyo aliyekopa benki ana nafuu zaidi
 
watu wamebadilisha mfumo wa maisha wa asili wa kuweka akiba na sasa wamekuwa addicted na mikopo

1. Banki kakopa miaka 8

2. Viccoba kakomba

3.Salary advance kakomba

4. voda niwezeshe kashabamiza

5. Kadi ya benki kaiwekeza kwa mangi mkopeshaji ili chochote kinachoingia kwenye akaunti kiondoke

6. Yeye akisikia mkopo popote akiliinasisimka haulizi riba wala gharama za mkopo.

Mfumo sahihi ni kuweka akiba na katika hili mfumo wa ushirika wa kuweka na kukopa ndio sahihi maana hata ukikopa unalazimishwa kuweka akiba. Usiende kwenye saccos ukiwa na wazo unataka kukopa haraka haraka tuu bali nedha na wazo la kujiwekea akiba na kununua hisa nyingi iliupate gawio na akiba nyingi zikusaidie kwa baadaye lakini sio kila tatizo linatatuliwa kwa mikopo zaidi unaongeza gharama kwenye maisha yako mkopo hata wa riba ndogo unaumiza.
 
Akope popote penye unafuu na kwa wakati sahihi..
Mfano kwa upande wangu,niwe na shida ya haraka na inatakiwa itatulike ndani ya muda fulani na usipoitatua inaweza leta madhara zaidi, kwa upande wangu sitaangalia sana kwenye riba hata kama ni 100%. Bali nitaangalia ni wapi watakaonipatia kwa muda ule husika (thamani ya fedha kwa muda husika).
Kwa ushauri, kama hitaji lake la fedha si la haraka; anaweza kuringanisha urasimu uliopo saccos na kwenye mabank pamoja na riba zitolewazo,atakapoona penye unafuu ndipo achukue hatua.
 
Q Lakini ukimaliza mkopo si utaweza kopa tena???

Sent using Jamii Forums mobile app
 
QLakini ukimaliza mkopo si utaweza kopa tena???

Sent using Jamii Forums mobile app
Kupata million 6 SACCOS lazima udundulize au ukakope mahali million 2 ili uweze kukopesha mara tatu ya akiba yako. Ukipata million 6 lazima utoe ile 2 irudi ulikoitia hivyo kama ni mkopo wa biashara utaingizi million 4 kwenye biashara wakati unatakiwa kurejesha 7,200,000
 
ila pia uzuri wa saccoss hiza zako zinaongezeka kwa kulipwa gawio kila mwaka, japo huwa kidogo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Gawio si mpaka muwe na uongozi bora wenye uwezo wa kusimamia mikopo yote ikalipwa na mkapata faida!!!
saccos inaongozwa kwa sheria ambayo ipo wazi, pia mikopo unayokopa saccos lazima uache 1.5% ya mkopo inakuwa bima ya mkopo. Pesa ya saccoss yote inatunzwa benki na mkopo unapewa kupitia benki

N.b Saccoss sio Vicoba

Sent using Jamii Forums mobile app
 


Mie mwenyewe jana kuna mdada nimemit naye ( nimesoma naye o level) anafanya kazi Access bank...anajua mishe zangu ananing'angania nikakope had nimestuka ..haiwezekan kuna kitu...sema hatujui mahesabu yao ya compound interest hapo lazima tupigwe!
 
Mie mwenyewe jana kuna mdada nimemit naye ( nimesoma naye o level) anafanya kazi Access bank...anajua mishe zangu ananing'angania nikakope had nimestuka ..haiwezekan kuna kitu...sema hatujui mahesabu yao ya compound interest hapo lazima tupigwe!
Ni balaa..imagine someone close to me kakopa nmb m7 ila jumla ya marejesho ni 12m ..yan karibia interest ni karibia 100% in five years.
Hatar
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…