HABARINI! TOKA jana kwenye mitandao ya kijamii Mchekeshaji Erick Omond amejiwa juu na baadhi ya watu kwa kile Alicho Fanya na kuleta mvutano mkubwa sana katika Imani!
Mimi ni mkristo,Lakini sijaona Kosa kwa kile Alichokifanya Erick Omondi! kabla ya Kuja kumuhukumu Erick Omond .....Tujiulize Je Erick Omond ni nani na anafanya nini? ERICK ni Mchekeshaji na anafikisha ujumbe kwa njia ya kuchekesha na kuimba!
Sasa kile alichokifanya ni moja ya uigizaji wake na Lengo lake ni kufikisha ujumbe! Jumbe ulifika tatizo liko wapi? Tujiulize Je mtu akiigiza kama Rais ni kweli anakuwa Rais? au mtu akiigiza Ana maambukizi je kweli anakuwa mayo?
Moja ya watu walio Kuja juu ni baraka De prince Lakini mm sioni kama ni sawa kumuhukumu Eric kwa Alicho fanya
View attachment 442376
Sasa Tujiulize wote Je Alicho Fanya Eric ni Sahihi? Kwangu mimi yupo sahihi