Je, Awamu ya 4 ibebe Lawama kwa mambo ya muungano yaliyoondolewa kinyemela na kupewa Zanzibar? Karibu tujadili kwa facts

Je, Awamu ya 4 ibebe Lawama kwa mambo ya muungano yaliyoondolewa kinyemela na kupewa Zanzibar? Karibu tujadili kwa facts

Shalom,

Tuunduiz Lissua myopia hawazungumzii haya mazito

Nasikitika kusema kwamba mambo ya muungano yalikuwa 22 na hakuna kikao halali cha Bunge la muungano kimeondoa baadhi ya mambo ya muungano. Cha ajabu Baraza la wawikilishi Zanzibar limefanya mabadilliko mengi yaliyoipa Zanzibar uhuru na haki ambazo hazitambuliki katika katiba ya muungano.

Ni hatari sana aliye ruhusu hayo kufanyika ni nyakati za awamu ya nne ikiwemo katiba ya Zanzibar ya 2010 imepoka madaraka ya Rais wa muungano. Tanzania imebaki ni kituko katiba ya muungano inasema hivi wakati katiba ya Zanzibar inasema vile.

Ni hatari sana na ndugu kipepeo mdomo ama chamdomo Tuunduiz Lissua haongei mambo ya msingi kama hayo anadonyoa anazotaka yeye.

CCM wamelala , Tanzania imelala, walishavunja muungano wakija kustuka Zanzibar itapeleka shauri lake UN la kutaka kujitegemea kama nchi.

Katiba ya Zanzibar ni sumu kwenye muungano ndiomana bandari za Zanzibar hazijaguswa kwenye saga la DP World kumbe Rais wa muungano hana mamlaka yoyote Zanzibar.

Chokochoko za wazanzibar wanajua katiba inawabeba ni mziki mnene Tanzania haina muungano tumebaki na katiba vuvuzela.

Watu wanacheka cheka sasa endelea kuchekelea vibes za wazanzibar mkistuka mshakuwa vibogoyo.

Kwa sasa koti la muungano jepesi kwa wazanzibar.

Imeze kama ilivyo ukitaka vielelezo tafuta katiba ya Zanzibar, Rais wa Zanzibar anapigiwa mizinga 21, Rais wa muungano hagawi mikoa, wilaya wala chochote Zanzibar, Zanzibar ni nchi, Baraza la wawikilishi Lina nguvu kuliko Bunge la muungano.

Tafuta hizo katiba mbili mjionee huo uchuro. Muungano umelegea vibaya.

Tubishane njooni
Hapa ilifaa kuwa na serikali moja tu inayotawala Bara na visiwani
 
Kwa kifupi tu, Zanzibar ioneshwe mlango wa kutokea kabla haijajitoa yenyewe kijeuri, maana ina hamu sana ya kusimama yenyewe kama taifa huru. Ya Nyerere yakiwatokea watajuta wenyewe huko na visiwa vyao
Zanzibar ilishajiandaa Musa mrefu kujisimamia yenyewe. Ina sheria zake, mahakama, majeshi yake, bendera, Huku Kuna TRA kule Kuna ZRA, nk
 
Zanzibar ilishajiandaa Musa mrefu kujisimamia yenyewe. Ina sheria zake, mahakama, majeshi yake, bendera, Huku Kuna TRA kule Kuna ZRA, nk
Na wanaendelea kujizatiti wawe na mambo yote halafu aje atokee mtu wa kusema muungano basi. Uanachama wa mashirika ya kimataifa wanautaka sana tu, OIC, FIFA bado wanalilia wapewe uanachama. Ni suala la muda tu Zanzibar ndio itavunja muungano kijeuri
 
Back
Top Bottom