Je, Bagamoyo Port itakuja kuwa White Elephant Port?

Je, Bagamoyo Port itakuja kuwa White Elephant Port?

Huyo mwekezaji wa kichina atafaidi kila kitu kwa 100%, yaani ni kana kwamba hilo eneo tumewazawadia wachina wafanye uwekezaji wao, bwerere, waluguru wanasema chobwedaa.........

..binafsi napendekeza tuwe na shares at least 40% kama ni sisi na wachina.

..kama ni china na oman basi tuwe na 30% of shares.

..nakubaliana na wewe kwamba kumuachia mchina amiliki hiyo bandari kwa asilimia 100% siyo sahihi.
 
Hivyo viwanda vitakavyojengwa hapo navyo watafanya kazi wachina tu? Isitoshe huo mradi ni ushirikiano baina ya China na Oman. Kuna upotoshaji usio wa msingi, na sababu hasa ni serikali yetu kuficha mikataba.
Mkuu kama ni swala la PPP linaeleweka, lakini kwa experience ya zambia na kenya......haiwezekani tukawaamini hao wachina kirahisi hivi, mchina hata mmarekani amemshindwa, itakuwa sisi tuingie kichwakichwa......
 
Mkuu kama ni swala la PPP linaeleweka, lakini kwa experience ya zambia na kenya......haiwezekani tukawaamini hao wachina kirahisi hivi, mchina hata mmarekani amemshindwa, itakuwa sisi tuingie kichwakichwa......

Mradi sio wa mchina tu, nusu nusu ni baina ya China na Oman. Isitoshe ni kipi tunamficha mchina wakati miundombinu kibao hadi ya ulinzi katuwekea yeye? Hata sasa vikosi vyetu vingi vya jeshi vinapata mafunzo na vifaa toka China. Kama tayari wako mpaka kwenye vyombo vya ulinzi, majengo kibao ni wao wamejenga, watashindwa kuweka chip za kukusanya taarifa za intelijensia mpaka wasubiri ujenzi wa bandari?
 
Nadhani Huo Mkataba utafanyiwa variation. Kuna mambo mengi yameshabadilika. Bandari ya Dar es Salaam upanuzi umeshaanza au kukamilika, bandari ya Tanga kuna jambo linaendelea pale.

Kwamba tulikuwa tunauhitaji mradi huo hilo lilikuwa bayana. Tatizo lilikuwa ktk terms and coditions.

Hata Rais Magufuli alizungumzia uhitaji wa kurekebisha terms and conditions kwamba zikienda hivyo zilivyokuwa, maslahi kwetu yangekuwa madogo.

Mimi suala langu kubwa ni our Export Capacity Utilisation, Je, tumeanza kuchukua hatua kuweza kunufaika na bandari hiyo kwa ajili ya exports au itakuwa bandari ya kushushia Imports zaidi?

Lakini pia huenda tukahitaji ujenzi mkubwa wa dedicated Railways na Access and exit roads kwenda na kutoka bandari hiyo, ambazo hazitatumia conventional passages tulizo nazo. Sisi tumejipangaje kuliona na kulitekeleza hilo, hizo ndizo changamoto.

Tusije kujenga a White Elephant Port yenye capacity kubwa ambayo hatutaweza kuifikia kwa muda mrefu ujao.

Bandari ya Dar es Salaam kwa sasa ni ndogo sana kwa ustawi wa Uchumi hasa ukizingatia kuwa tumeshaingia uchumi wa kati, tunatakiwa kwenda juu zaidi. [emoji120][emoji120][emoji120]

Shida iko kwenye terms & conditions za mkataba huo. May be kwa kuwa hakuna ajuaye, tunasikia na kuambiwa tu na hawa tunaowaita "viongozi wetu"..

Kwa ishu ya umiliki wa ardhi kwa miaka 99, mimi hata sijali kwa sababu ardhi iko kwa ajili kutuzalishia na kutupa manufaa. Hata tukiamua tusiitoe, tukae nayo tu bila kuwa utilized kwa manufaa ya maisha ya sasa ya watu halafu dunia hii kesho kutwa ikaondolewa na mwenye nayo , bila shaka sisi wote (watanzania) tutaonekana kuwa ni wapumbavu sana....!

Mimi nadhani (kama ni kweli), tatizo liko kwenye mamlaka ya mapato ya Tanzania (TRA) kutokusanya mapato ya bandari hiyo na kisha kuyagawa kwa wabia sawa sawa na mkataba...

Hili linazungumzika na likakubalika na pande zote...

Je, ni inaweza kuwa a white elephant port...?

No, sidhani. Kwa sababu naamini kabisa utafiti wa kisayansi wa kutosha ulifanyika hata kufikia maamuzi haya ya ujenzi...

Tukumbuke kuwa, serikali ya Tanzania haiingizi hata senti moja ktk mradi huu. Fedha zote za kugharamia mradi huu ni juu ya mwekezaji mwenyewe. Serikali ya Tanzania gharama yake ni kutoa ardhi tu na kulipa fidia kwa wananch watakaoachia ardhi yao kwa ajili yq mradi huo....

Mwekezaji hawezi kuja kuwekeza dola bilioni kumi (10bn) huku akijua kabisa hakuna faida yoyote kwenye project hiyo...

Mradi uendelee kutekelezwa kwa sababu una faida nyingi na kubwa sana kwa nchi na wananchi kuliko hasara...
 
Wakuu, Tutakapoanza bulk products hasa za Chuma na mkaa wa mawe, na project za Primary industries machinery, bandari ya Dar haitatosha. Pana ufinyu wa maneuvrebility. Kuna mtaalamu ambaye tuliwahi kufanya naye Tume ya Rais ya Kurekebisha mashirika ya Umma, kama Utilities Advisor akiwa Mtaalamu mwelekezi kutoka Uingereza, Barbara Harris, mwajiriwa wa DfID (wakati huo 1999-2006), yupo ktk mradi huo wa bandari ya Bagamoyo katika jopo la Washauri Elekezi. Ni mtu straight, hawezi kufanya mradi wenye utata.

Jambo moja nililojifunza ambalo naweza kusema ndilo udhaifu wetu kama nchi katika miradi ya kimataifa k(wa uzoefu wangu) ni katika masuala ya mikataba, We seriously lack competence in negotiation skills.

Kuna maeneo ambayo tupende tusipende, tunatakiwa kujenga capacity ya negotiation skills. Na hili haliji ndani ya miaka mitano au kumi. Linatakiwa kuwa eneo la kujengea uwezo constantly hata miaka 20 au 30 mfululizo.

Tumeanza miradi ya Oil and gas kitambo. Tumeweza kujenga uwezo wa wataalamu wa kufanya kazi katika miradi hiyo kwa ngazi ya ufundi lakini hata tukianzisha degree programmes za Legal Aspects of Oil and Gas bado haitatufanya tuwe experts katika maeneo hayo.

Tunatakiwa kuwapeleka wasomi hao kwenye attachments katika nchi kama za Ghuba, Urusi, Venezuela na Afrika Magharibi pamoja na Angola ili waone changamoto zinazopatikana huko na zinavyoshughulikiwa.

Then tutakuwa na uzoefu thabiti wa kuhandle masuala kama hayo.

Katika eneo la masuala ya bandari, pale PSRC tuliwahi kupata ushauri wa wataalamu mahiri kutoka Rotterdam Marine Group (RMG). Rotterdam ni mji-Bandari. Ndilo eneo linaloaminika duniani kote sababu kuna vyuo vya uendelezaji na uboreshaji huduma za bandari chenye kutambulika kimataifa.

Kampuni kubwa kama za kuhudumia Bandari kubwa zaidi duniani kama Hutchinson Wampoa inayoendesha huduma katika bandari kubwa za Hong Kong, Malaysia, Phillipines, Singapore na za Ulaya, wataalamu wake husoma hapo Rotterdam.

Hapa kwetu bado hatuna wataalamu wengi waliosoma kule. Pia tunahitaji kupeleka wataalamu wakasome na kufanya kazi pale na kwingineko kupata uzoefu unaoitwa Intermational Best Practice. Tunalikosa hili katika maeneo mengi yakiwemo maeneo ya uchimbaji na biashara ya madini mbalimbali yakiwemo ya dhahabu, chuma, nickel, cobalt na vito, ambayo tunayo.

Ukisoma LLB ukapata LLM na hata PhD havikufanyi kuwa best negotiator for your country on these technical fronts.

Katika urekebishaji na ubinafsishaji wa Mashirika ya Umma, tuliajiri Mtaalamu MwelekeI Kiongozi (Lead Adviser) Mwingereza mwenye asili ya Jamaica, Prof. Cesley Sampson. Prof. Sampson alianzisha mpango wa Local Experts Capacity Building in international transactions ambapo kwa kila mradi uliohitaji mtaalamu mwelekezi wa kimataifa, alitakiwa kuajiri local law firm.

Ndivyo jinsi kampuni za IIMMA advocate, Mkono Advocates, Sinare-Mwandambo Advocates na nyinginezo zilivyojenga uwezo wa utaalamu wa mikataba ya kimataifa na kuendelea nayo hata baada ya PSRC kumaliza shughuli zake.

Yatupasa kama taifa kuhakikisha kuwa katika kila sekta muhimu kama madini, oil and gas, railway, port development nk tunakuwa na Mradi unaoajiri timu ya Wataalamu Elekezi ambao wanakuwa wanaajiriwa kwa muda tu kupitia miradi hiyo. Hao watasaidia kutujulisha vipaumbele vya msingi katika Capacity building kwa watu wetu.

Lakini wakati tunajenga hiyo capacity, wataserve kama Proxy Negotiators kwa miradi ambayo inaanza au kuendelea. Itatupuguzia kesi za mikataba ya kimataifa.... [emoji120] I stand to be corrected
 
Hata ikiwa White elephant siyo hasara kwa serikali, kwasababu kwenye huo mradi serikali haichangii hata 100
Kwa mkataba huu serikali ishirikiane na wawekezaji kujenga bandari hii iwe na jicho lake hata kama kwa 10%umma na by 90% sekta binafsi i.e wachina, oman na wazalendo km Bahresa/mabenki yetu nk kwa utaratibu wa PPP hapo mimi sitakuwa na hofu na masharti baadhi yaangaliwe upya.
 
1.Usiendeleze bandari yoyote
2.Usijenge barabara hata za kusini
3.Umiliki wa ardhi miaka 99
3.Usihoji kuhusu matumizi ya Ardhi
4.Marufuku TRA kufika Bagamoyo
5.Gawio la mapato ya bandari litaamriwa na mwekezaji atakapopenda.
.
.
.
Nikasema waliokubali mkataba kama huu ni uzao wa Mangungo.
Hizo terms za mkataba umeziona?

Au na wewe ni kilaza wa magufuli?
 
..mimi nimemuelewa tofauti kidogo.

..hebu tuangalie mifano hii miwili.

A: chukulia mfano wa hasara ya ATCL ambapo zimewekezwa fedha za walipa kodi wa Tz.

B: linganisha na hasara ya kampuni ya ndege kama Precision Airline ambayo 100% ni fedha za muwekezaji.

..kati ya hasara hizo mbili wewe unaona ipi ina afadhali?

..ukipata jibu sasa lihamishie kwenye bandari ya Bwagamoyo.

Cc Mkaruka
Kwa nchi zilizoendelea hata makampuni binafsi yanapata ruzuku toka serikalini yakiyumba.

Precision ikiyumba ni hasara kubwa kwa taifa kuliko isipoyumba. Ndo maana mashirika kama haya yanapewa ruzuku.
 
Katika projects kubwa dunia, mwekezaji hawezi kuwa moja. Hata siku. Ofcourse conglomerate ni makumpuni zaidi ya moja na kutoka zaidi ya nchi moja. Je, hao wote ni majambazi?
 
Back
Top Bottom