Je, biashara 2 tofauti zinahitaji TIN number 2 tofauti?

Super Tuesday

JF-Expert Member
Joined
Apr 5, 2016
Posts
636
Reaction score
727
wadau naomba kuuliza. mimi nina biashara ya salon ya kiume 'barber shop' ambayo nina TIN number iliyoandikwa kwa jina langu na jina la hiyo salon, ila hivi sasa ninataka niongeze salon ya pili, kwa kufungua salon nyingine yenye jina lingine mahali pengine. Je, ninatakiwa kuomba TIN number nyingine TRA kwaajili ya salon hii mpya? nitashukuru sana kwa majibu yenu wadau.
 
Hapo salon una EFD machine? Maana hiyo machine inakuwa ina TIN yako, sasa ukifungua biashara nyingine sidhani kama TIN moja inaweza kuwa na EFD machine mbili.
 
Kama mumiliki ni yule yule huwezi kuwa Na TIN namba nyingine ndugu. Hapo utapata makadilio kwa tin ile ile Boss
 
Hapo salon una EFD machine? Maana hiyo machine inakuwa ina TIN yako, sasa ukifungua biashara nyingine sidhani kama TIN moja inaweza kuwa na EFD machine mbili.
yes, ninayo EFD machine.
 
Kama mumiliki ni yule yule huwezi kuwa Na TIN namba nyingine ndugu. Hapo utapata makadilio kwa tin ile ile Boss
Thats right.

TIN maana yake ni Taxpayer Identification Number.

Ni namba ya mlipakodi. Si namba ya biashara ya mlipakodi.

Hivyo, ili kuhakikisha kila mlipakodi faili lake halichanganyi akili, inabidi kila mlipakodi awe na TIN moja tu.
 
TIN huwa moja tu. We kafanye kadirio la biashara Mpya, kwa kupeleka tin yako ...then utakata leseni nyingine kama ni wilaya nyingine
 
Hakuna mtu anaweza kuwa na TIN mbili. Hapo unahitaji Branch TIN, nenda ofisi ya TRA iliyokaribu waambie unafungua biashara nyingine watakukadiria then watakupa Branch TIN(TIN yako hiyo hiyo inakuwa na tawi). Mtu kama Bakhresa biashara zoooote alizonazo TIN ni moja tuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…