Je, biashara ya Bar ina laana?

Je, biashara ya Bar ina laana?

mwanyaluke

JF-Expert Member
Joined
Jan 22, 2015
Posts
704
Reaction score
2,435
Hivi ni kweli biashara ya bar na kumbi za starehe ina laana? Zamani nilikuwa na rafiki yangu mfanyabiashara aliyekuwa anaishi Chunya, Mbeya. Wakati huo, mimi nilikuwa katika biashara za magari, zote tukiwa tumerithi kutoka kwa wazazi wetu.

Katika mazungumzo yetu kuhusu maisha na biashara, nilimshauri kwamba, kwa kuwa alikuwa na fedha, angeweza kuanzisha sehemu ya starehe Chunya, kwani wakati huo hakukuwa na sehemu nzuri za starehe.

Alinijibu kwa urahisi na kusema, "Mwanangu, biashara ya bar ina laana. Chunguza familia ambazo ama baba, mama, au familia kwa ujumla wanamiliki biashara hiyo – wengi huishia kuharibikiwa, kufilisiwa, kuchoka, kufa na magonjwa ya aibu, au kupata ajali. Hakuna maisha marefu kwenye hiyo biashara, na usijaribu hata kufikiria."

Miaka ilipita, na rafiki yangu huyo aliaga dunia. Siku moja, nilikuwa kwenye sehemu ya starehe mjini Mbeya (City Pub), ambapo nilikutana na mfanyabiashara mwenzangu. Katika mazungumzo yetu, nilieleza kisa hicho kuhusu biashara za starehe. Naye alinipa ushauri mkubwa akisema kuwa biashara hiyo haina baraka, na hata alitoa mifano kutoka kwenye Biblia. Maneno yake yalinishtua na kuanza kujiuliza kama kweli biashara hii ina matatizo.

Nilichogundua ni kwamba:

  1. Biashara hii huvuma kwa muda mfupi na kisha hufa ndani ya miaka michache.
  2. Inahusisha dhuluma nyingi.
  3. Familia nyingi zimepoteana baada ya biashara hii kufilisika.
  4. Wengi huanza biashara hii, lakini wachache sana huweza kudumu.
  5. Ni vigumu kupata muda mwafaka wa kuendelea kuboresha biashara hiyo.
  6. Faida yake ni ndogo sana, na mtaji na faida havilingani.
  7. Matukio ya vifo vya wamiliki wake hufanana sana – iwe ni magonjwa, ajali, nk.
Nilipenda sana siku moja kuwa na sehemu ya starehe hapa Jombe, lakini haya niliyoyaona na kusikia yanazidi kunitia shaka. Siku moja rafiki yangu Mhindi alinishauri kuwa na mawazo tofauti ya biashara na kuepuka bar, akidai kuna matatizo. Aliendelea kusema nifikirie biashara kama mgahawa mzuri lakini sio kuuza vileo.

Nauliza kwenu: Biashara ya bar na kumbi za starehe huko kwenu imekaaje?
 
Hivi ni kweli biashara ya bar na kumbi za starehe ina laana? Zamani nilikuwa na rafiki yangu mfanyabiashara wa madini aitwaye Goodluck Sanga (mtoto wa mzee Itumbi), aliyekuwa anaishi Chunya, Mbeya. Wakati huo, mimi nilikuwa katika biashara za magari, zote tukiwa tumerithi kutoka kwa wazazi wetu.

Katika mazungumzo yetu kuhusu maisha na biashara, nilimshauri kwamba, kwa kuwa alikuwa na fedha, angeweza kuanzisha sehemu ya starehe Chunya, kwani wakati huo hakukuwa na sehemu nzuri za starehe.

Alinijibu kwa urahisi na kusema, "Mwanangu, biashara ya bar ina laana. Chunguza familia ambazo ama baba, mama, au familia kwa ujumla wanamiliki biashara hiyo – wengi huishia kuharibikiwa, kufilisiwa, kuchoka, kufa na magonjwa ya aibu, au kupata ajali. Hakuna maisha marefu kwenye hiyo biashara, na usijaribu hata kufikiria."

Miaka ilipita, na rafiki yangu huyo aliaga dunia. Siku moja, nilikuwa kwenye sehemu ya starehe mjini Mbeya (City Pub), ambapo nilikutana na mfanyabiashara mwenzangu. Katika mazungumzo yetu, nilieleza kisa hicho kuhusu biashara za starehe. Naye alinipa ushauri mkubwa akisema kuwa biashara hiyo haina baraka, na hata alitoa mifano kutoka kwenye Biblia. Maneno yake yalinishtua na kuanza kujiuliza kama kweli biashara hii ina matatizo.

Nilichogundua ni kwamba:

  1. Biashara hii huvuma kwa muda mfupi na kisha hufa ndani ya miaka michache.
  2. Inahusisha dhuluma nyingi.
  3. Familia nyingi zimepoteana baada ya biashara hii kufilisika.
  4. Wengi huanza biashara hii, lakini wachache sana huweza kudumu.
  5. Ni vigumu kupata muda mwafaka wa kuendelea kuboresha biashara hiyo.
  6. Faida yake ni ndogo sana, na mtaji na faida havilingani.
  7. Matukio ya vifo vya wamiliki wake hufanana sana – iwe ni magonjwa, ajali, nk.
Nilipenda sana siku moja kuwa na sehemu ya starehe hapa Jombe, lakini haya niliyoyaona na kusikia yanazidi kunitia shaka. Siku moja rafiki yangu Mhindi alinishauri kuwa na mawazo tofauti ya biashara na kuepuka bar, akidai kuna matatizo. Aliendelea kusema nifikirie biashara kama mgahawa mzuri lakini sio kuuza vileo.

Nauliza kwenu: Biashara ya bar na kumbi za starehe huko kwenu imekaaje?
Ukiondoa point na. 2, zingine zote zina-apply kwa biashara nyingi tu mbali na za bar.

Dhulma dhidi ya watu au dhidi ya mamlaka (TRA, Halmashauri) lazima ziwepo kwenye biashara yoyote.
 
Uko sahihi uwekezaji na kinachopatikana, ukitoa gharama za uendeshaji ni stress tupu!
Na mbaya zaidi biashara ikishakuwa na jina kubwa unaanza kugawana faida na mamlaka, vikwazo vinakuwa haviishi!
 
Ni biashara yenye profit margin ndogo sana, kwa maana hiyo kama unataka faida kubwa lazima uwe na traffic au volume kubwa ya wateja.

Siamini kwamba kuna laana ila ni kwamba aina ya biashara kama hiyo inayotegemea volume ya wateja, ikitokea pakadoda yaani pasiwike basi biashara inakufia hapo hapo.

Kwa wajanja wa mjini, biashara ya bar hutumika kama kichochezi au geresha kuficha biashara nyingine ambazo ndo zina pesa mingi i.e. madawa ya kulevya, madanguro, money laundering, uuzaji wa silaha n.k

So usije kweli ukajichanganya kufungua bar ilihali hujui faida itapita mlango upi, lazima ukwame
 
Hivi ni kweli biashara ya bar na kumbi za starehe ina laana? Zamani nilikuwa na rafiki yangu mfanyabiashara wa madini aitwaye Goodluck Sanga (mtoto wa mzee Itumbi), aliyekuwa anaishi Chunya, Mbeya. Wakati huo, mimi nilikuwa katika biashara za magari, zote tukiwa tumerithi kutoka kwa wazazi wetu.

Katika mazungumzo yetu kuhusu maisha na biashara, nilimshauri kwamba, kwa kuwa alikuwa na fedha, angeweza kuanzisha sehemu ya starehe Chunya, kwani wakati huo hakukuwa na sehemu nzuri za starehe.

Alinijibu kwa urahisi na kusema, "Mwanangu, biashara ya bar ina laana. Chunguza familia ambazo ama baba, mama, au familia kwa ujumla wanamiliki biashara hiyo – wengi huishia kuharibikiwa, kufilisiwa, kuchoka, kufa na magonjwa ya aibu, au kupata ajali. Hakuna maisha marefu kwenye hiyo biashara, na usijaribu hata kufikiria."

Miaka ilipita, na rafiki yangu huyo aliaga dunia. Siku moja, nilikuwa kwenye sehemu ya starehe mjini Mbeya (City Pub), ambapo nilikutana na mfanyabiashara mwenzangu. Katika mazungumzo yetu, nilieleza kisa hicho kuhusu biashara za starehe. Naye alinipa ushauri mkubwa akisema kuwa biashara hiyo haina baraka, na hata alitoa mifano kutoka kwenye Biblia. Maneno yake yalinishtua na kuanza kujiuliza kama kweli biashara hii ina matatizo.

Nilichogundua ni kwamba:

  1. Biashara hii huvuma kwa muda mfupi na kisha hufa ndani ya miaka michache.
  2. Inahusisha dhuluma nyingi.
  3. Familia nyingi zimepoteana baada ya biashara hii kufilisika.
  4. Wengi huanza biashara hii, lakini wachache sana huweza kudumu.
  5. Ni vigumu kupata muda mwafaka wa kuendelea kuboresha biashara hiyo.
  6. Faida yake ni ndogo sana, na mtaji na faida havilingani.
  7. Matukio ya vifo vya wamiliki wake hufanana sana – iwe ni magonjwa, ajali, nk.
Nilipenda sana siku moja kuwa na sehemu ya starehe hapa Jombe, lakini haya niliyoyaona na kusikia yanazidi kunitia shaka. Siku moja rafiki yangu Mhindi alinishauri kuwa na mawazo tofauti ya biashara na kuepuka bar, akidai kuna matatizo. Aliendelea kusema nifikirie biashara kama mgahawa mzuri lakini sio kuuza vileo.

Nauliza kwenu: Biashara ya bar na kumbi za starehe huko kwenu imekaaje?
Kama hauna akili hiyo biasharaxachana nayo ...
 
Back
Top Bottom