Je, Binadamu tuna free will (Hiari)?

Je, Binadamu tuna free will (Hiari)?

Kuna zawadi na adhabu kwa watakomfuata au kumpinga. Kitendo cha kuwepo tu adhabu nisipomfuata Mungu kinamaanisha sina hiari/free will katika maisha yangu hapa duniani, maana ningekuwa nayo ningekuwa na uhuru wa kufanya jambo lolote liwe jema au baya bila kuwa na consequences. Ni sawa na mtu akuwekee bunduki kichwani akuambie una uhuru wa kutaja au kutotaja password yako ya benki, ila usipotaja nakuua. Sasa hapo unao huo uhuru?
Kaka mkubwaa kuikataa freewill kwa kigezo cha kuwepo adhabu na zawadi sio sawa.

Kwa kuwa Mungu anajua hali yote iliyopo sasa hivi, na anajua matokeo yote ya hali zote aliamua kuweka mfumo.
Na kwa kuwa pia Mungu hana upendeleo, akimpangia huyu awe raisi na mwingine awe waziri mkuu atakuwa amempendelea mmoja. Bora hao, vipi yule atakayempangia awe mnyonge mlipakodi si ndo tutasema amemuonea kabisaaa!? Ujanja hapa ni kuweka mfumo tu.

Mfumo upo na option zote na matokeo yote ambayo mtu anayafikia kiotomati kutokana na machaguo yake. Mfano atakayesoma sana, akabeba majukumu kinamna hii atakuwa raisi mwishowe. Atakayeamua kutosoma na kufanya ufundi atakuwa mpigakura. Akijiongeza kiufundi akawa kampuni kubwa atamuongoza hadi huyo rais katika sera zake! So ni utashi huru hakuna anayewekewa maamuzi kichwani kwake ni yeye anacheza na option za mfumo na kujioatia matokeo kiotomati. Ngoja niandae kamfano.
 
We are determined, no free will at all! Can you choose to kill? I think you are determined to kill, may be devil is the one directing you to kill.
 
Mfano huyo mtu hapo katikati akiamua kwenda pointi D ndio lengo lake basi ataenda.
Lazima atatembea hadi pointi A.
Halafu akiamua kupitia B basi atafika mahala atavuka mto kwa daraja atafika D

lakini akiamua kupitia C basi matokeo yake ataogelea mtoni ndipo atafika D
Katika maamuzi ya kupita B au C ni yeye na matokeo ya kuvuka daraja au kuogelea ni yeye amepima akaona kipi kinafaa. Yeye ndo anayesema kichwani (kwanza nna jasho bora nipitie huku hata nikaoge na kuoga). Mungu au serikali ikimpangia akavuke daraja tuu ni kumuonea hata kama ni salama zaidi kwake. Yeye amependa kuogelea mamba atapambana nao kama vipi(kwanza haamini kama mamba wapo😄).

Lakini kwa utashi-huru wake anaweza kuutumia kuamua sitaki hata kwenda pointi D mimi ntaenda kufia T au W akanyooka hadi destination

Au akaenda tu na kumaliza alfabeti hadi Z akasema mimi nikifa nataka niishie hapo. Maisha ndo hayahaya, hakuna zaidi ya alfabeti naye akafa.

Mwingine akajiaminisha kuwa kuna zaidi ya alfabeti akaziishi akatumia na nyingine za kutohoa tu mfano hiyo AC hadi M-N-O akamaliza zote na kwa imani akaamini zipo nyingine akaishi na tumaini la kuziishi basi huyo ataishi milele maana hatazimalizaga pointi zote.

Bottomline ni kwamba Mungu kaweka mfumo na pointi zote zimo humo. Mtu binafsi anachagua anapotaka kwenda na matokeo anayapata sambamba na machaguo yake. Full stop.
20230114_180445.jpg
 
Bwana Yesu Asifiwe, dhambi nayo ilianzia Kwenye free will aliyozitaka Adam na Mkewe Hawa baada ibilisi kuwadanganya (Mwanzo 3:1-6),Shetani na free will zake aliasi ili awe sawa na Mungu.Tuepuka kumkufuru BWANA wetu.
Usije ukajiona kila kitu unaweza fanya debate Maandiko yote tunayoandika iwe kwa uzuri au ubaya wake yatalipwa kwa hesabu yake

Mungu anatupenda sana ndio Maana anataka tusikie sauti yake.Kusudio lake huko mbeleni ni kuja Kuuangamiza uovu wote na Watu wote tuishi bila dhambi,sasa kama sisi tukiendelea kuishikiria dhambi kipindi anaangimiza uovu automatic na sisi tutaangamia pia.
 
‘Free will’ ipo mkuu ktk mfano huu maana kuwepo kwa ‘consequences’ hakumaanishi tendo hilo halikuwa na ‘Free will’ kwa maana hakuna mtu kaumbwa kama malaika kuwa hana chaguo ila kufanya mema tu, kila mtu yuko huru kuchagua, ‘with consequences’ lakini na kwa bahati mbaya hakuna kitu hakina ‘consequences’.
Kusema binadamu hana free will haimaanishi kuwa anafanya mema tu, anaweza akawa anafanya yote mema na mabaya lakini bila kuchagua mwenyewe, bali kwa pressure za mazingira,kemikali kwenye ubongo, script ya simulation,randomness, au mpango wa Mungu anayeijua kesho yako.
Ila umeachwa huru huku ukipewa taarifa kuwa ukiswali kuna zawadi ila kama hutaswali kuna adhabu kwa maneno mengine uko huru kuchagua aidha zawadi au adhabu, hulazimishwi.
Then sina uhuru 100% wa kufanya ninachotaka...Mtu akisema shule yetu ins uhuru mkubwa anamaanisha kuna uwezo wa kufanya mema na mabaya bila kuadhibiwa...Huwezi kusema kazini kwetu kuna uhuru ila ukichelewa sekunde mbili unakatwa mshahara,ukipoteza muda chooni unakatwa mshahara,usipokwenda kazini unafukuzwa,ukizidisha dakika 1 ya lunch huna kazi sasa hapo uhuru utakuwa wapi?
Halafu ukiachana na hiyo.... Mungu anajua kesho, kitendo cha yeye kuijua tu it means imeshaandikwa na wewe huna choice inabidi ufanye kama ililvyoandikwa
Hata mfano wa mwizi kukuwekea silaha akitaka utaje nywila ya benki bado uko huru kwa namna fulani, maana unaweza kuchagua
1. Kupigana nae
2. Kutaja nywila ukitumai atakuacha
3. Kukataa ili akuue kirahisi
(Sisi waislam kwenye hili tunaambiwa tuchague ya kwanza kwa maana Muumini mnyonge kamwe hawezi kuwa kwenye daraja sawa na Muumini mwenye nguvu)
Sasa kwa Mungu hiyo option ya kupigana nae huna maana yeye ni Mungu, akisema usipohiji unaenda motoni (mfano) hauna option ya kutohiji na kupambana usiende motoni...Kitendo cha kukosa hiyo option ndio ukosefu wa uhur wenyewe naozungumzia
Bado una ‘Free will’ mkuu, unaweza ongea tofauti ukitaka, ukavaa tofauti na ukaachana na tamaduni zako.
Mfano tu Tanzania tuna zaidi ya makabila 120 na kwa sasa watu wengi wanaacha kuzungumza kikabila na tunazungumza kiswahili, tufahamu kuwa hapo kabla makabila yao hayakujua kiswahili.
Sasa kwa huo mfano hauoni kuwa wasukuma wa sasa hawana choice maana mazingira yanawafosi kukijua kiswahili na kusahau kisukuma au kukiswahilisha?? unakuta mtu anaongea kisukuma kama kiswahili. Hakuna anayeweza kucontrol mazingira akulia sehemu hakuna muingiliano hatajua kiswahili na aliyekulia spain hatojua kisukuma..Kuongea kwetu kuko limited na mazingira ya jamii zinazotuzunguka..Hata ukisema hutaki kuvaa kama waswahili huwezi kuamua kutembea uchi kwa sababu mazingir yoyote hayakuruhusu kwakuwa hauna huo uhurukulingana na tamduni za binadamu

Tazama tunavyovyaa, sio sisi tuliokuwa tunavaa magome ya miti? Muziki tulikuwa tukipiga kwa ngoma? Na taarifa tuliitaka kwa mbiu?
Tazama vijana wetu mabarobaro wanavyopendeza kwa mavazi ya ki Magharibi, tazama Masheikh zetu kutwa kubadili kanzu za Dubai, unafikiri hatuna uhuru wa kuchagua?
Zamani walivaa magome ya miti lakini kuotokana na sababu zilizo nje ya uwezo wao,mazingira yalibadilika (maana hakuna mtu mmoja anayecontrol mazingira yote) utandawazi ukaja ikabidi wavae majoho,kanzu na suti. Na sasa kwa haya mazingira mapya hawawezi tena kuvaa magome ya miti
Leo hii ukiamua kuvaa magome ya miti hakuna wa kukukataza mkuu ni chaguo lako, Mpoto bado anaendeleza utamaduni wa kutembea peku na mavazi asili akiamua, yuko huru.
Trust me, hata mpoto kuna mazingira yaliyompelekea kuwa mtu wa kuvaa hivyo, angekuwa mtoto wa Bakhresa angevaa hivyo? Angekuwa ridhiwani je? Kwahyo ni mazingira fulani either alipokulia,shule alizosoma au marafiki na watu aliojuana nao ndio wamempelekea kufanya kuwa anavaa hivyo.
Kuhusu vyakula tunavyo vya asili yetu na historia inatuambia hata mahindi hatukuwa nayo hapa, yaliletwa toka ardhi ya mbali, leo hii tunachagua kula Pizza, Burger au Ugali mlenda, Uhuru wa kimaamuzi tunao.
Lakini hatuwezi kuchagua kuacha kula
Elimu haizuii uhuru wako, Elimu inakuongezea wigo wa uhuru wako, nilikwambia kila jambo lina ‘consequences’ hii haikwepeki abadan, ukisoma hata ngazi ya PhD bado unaweza kula chakula kilichochacha ukiamua, ukisoma dini bado unaweza zini ukiamua.
Uhuru upo pale pale ila elimu itakuongoza kufanya machaguo sahihi na si laIma uifuate ukiamua unaweza kuisigina.
Ni lini ulimkuta msomi wa PHd Kwa akili zake timamu anaokunywa maji ya lamboni? anakula mkate wa jalalani?? Huo uhuru umeshaondoshwa na elimu yake
Wewe ni Hakimu ukitaka unaweza kulewa na kushinda vijiwe vya kubeti, ukiamua unaweza ila hilo lina ‘consequences’ kama ambavyo umechagua kutoenda hilo pia lina ‘consequences’ ambayo ni unaona huna uhuru ilhali unao.
Hizo cnsequences ndio zinalimit uhuru wenyewe...maaana ukiwa na uhuru kamili hakuna consequences.
Tukienda kwa notion hiyo Basi hata wafungwa sasa tutasema wako huru ila wakiamua kuvuka getti kuna 'cosequemce ya kupigwa risasi. Wako huru kulala mpaka saa 3 asubuhi ila wakifanya hivyo kuna consequence ya virungu,,,,mkuu sidhani kama huo ni uhuru.
Mkuu unaweza hivi vyote ila hujaamua tu. Ukiamua unaweza acha kula ila kuna ‘consequences’ na unavyoamua kuendelea kula vilevile kuna ‘consequences’
‘Consequences’ hazikwepeki mkuu.

Ukitaka unaweza acha kulala ila vilevile kuna ‘consequences’
Hizo consequences ndio zinauziba uhuru wenyewe
Unaweza acha kujisaidia, unaweza jaribu kupaa, unaweza jaribu kubeba gari, unaweza jirefusha unaweza jifupisha, unaweza meza viwembe na unaweza piga bao 20 nini 10, haya yote ukiamua unayaweza vizuri sana ila hautakuwa tayari kubeba ‘consequences’ zake ila unaweza kuchagua.
Unawezaje kupiga bao 20? Halafu siongelei kujaribu naongelea kufanya
Kwenye kemikali asili za mwili bado tuko huru kuamua ukitaka utazipunguza au kuendelea nazo.
'Ukitaka' nani anayetaka? maana hizo kemikali ndio zinapelekea wewe kutaka au kutotaka kitu...Unaweza ukaamua kuacha mihadarati kisa dopamine inazidi,,,kumbe inayokuachisha hio ni oxytocin inayohusika na kukufanya uridhike na jambo fulan
Dopamine hizo hutokea kutuzawadia pale tendo la furaha tunapolifanya, hivyo ukiwa huitaki hiyo usifanye matendo yanayokupa furaha.
Hakuna binadamu ambaye hatafuti furaha kwa namna moja au nyingine labda huyo ni roboti...mkuu tunajadili uhalisia na binadamu wa kawaida sio AI
Bangi na cocaine vile vile ni hiyari yetu kuvitumia au la.
Bado tuna uhuru wa kufanya maamuzi ni vile hatuutumii makusudi tu.
ila unakubali ukivittumia vinakuendesha sio? sasa nilitumia kama mfano kuonesha jinsi kemikali extternal manmade zinakuendesha kuwa 'abnormal' basi hiyo inaprove kuwa hizi kemikali internal naural ndio zinakufanya kuwa 'normAL'
 
Pia wanasema kadri unavyoendelea kufanya jambo fulani na ndivyo sakiti hizo huzidi kujiunga, sasa hapo hulazimishwi kumbe maamuzi yako ndiyo huathiri sakiti hizo, basi kama hupendi vile zimeungwa badili maamuzi yako.
Ndiyo,mwanzoni ukitengeneza hizo sakitii inakuwa rahisi kubadili maamuzi, mfano ukijifunza leo umalaya, ni rahisi kuacha ila kwa mtu ambaye tokea azaliwe anakulia kwenye umalaya ni ngumu kuacha...ndomaana kuna msemo 'you cant turn a ho into a housewife' 'you cant teach an old dog new tricks'..Kuna stage zile circuit zinakuwa zimekomaa kiasi kwamba kuzibadili ni near impossible (kama extrovert kuwa introvert au vice versa)
(Naelewa si rahisi ila nasisitiza tu kuwa uhuru tunao, sisi si kama roboti)

‘as long as am concerned’ bado ninaamini tuna free will, maana siku nikiamka ninaamua leo niswali au nisiswali kwa uhuru kabisa.
Hii dhana ya ‘determinism’ Ninakubaliana nayo ila bado napata nayo ukakati ila ‘so far’ bado najihisi niko huru kufanya maamuzi yote maishani.
Wewe kujihisi uko huru haimaanishi uko huru, huko kujihisi huru kunaweza kuwa ni illusion ubongo wako unakutengenezea.
Hii sikubaliani nayo hata kidogo. Kila mmoja wetu anayo nafasi ya kuamua uelekeo wa maisha yake.

Mathalan unataka kuwa hakimu, ni lazima ukasome sheria, na ili usome sheria ni lazima usome mpaka ngazi fulani, sijawahi ona mtu kawa hakimu kwa bahati mbaya, ‘and I think this idea of universe events occurring by chance is laughable and absurd’
Unaweza kuamua kuwa daktari halafu ile umemaliza kusoma diploma ya CO unataka kuapply degree, serikali ikasema udaktari lazima upite form 6, na kufaulu bado ni ishu ya bahati maana unaweza kusoma Organic chemistry mtihani ukatoka inorganic.

Na mwingine anaweza asipende kuwa mwalimu ila akashangaa mambo yalivyoenda mpaka akawa mwalimu (walimu wengi hawakupanga kuwa walimu)
‘free will’ tunayo mkuu, na tunaitumia kila siku kila saa kila dakika, bitu ambavyo havina ‘free will’ ni maroboti ambayo mienendo yao na tabia zao inakuwa tayari zimepangwa kwa ‘alogarithm’.
Wewe unajuaje kama haupo kwenye algorithm?? Roboti anajijuaje kuwa anafata algorithm??
Kuna experiment unaweza kuifanya kuprove kuwa huu ulimwengu sio simulation au sio scripted?
Nadhani vitu kama coincidence,karma,deja vu,destiny,prophesies nk. vinaprove huu ulimwengu ni scripted
Leo mwanaadamu akiendeaha lori kwa kasi mbele akakuta bi kizee na gari iliyobeba wanafunzi yuko huru kuchagua amgonge nani kati ya hao wawili kulingana na hisia zake na akili yake, nilimsikia mtaalam mmoja akizungumzia mustakabali wa ‘self driving cars’ akasema kwenye ‘situations’ kama hizo roboti itaamua kulingana na ‘Alogarithm’ yake ilivyoundwa na akatoa wito kuwa watu wa maadili wahusishwe kwenye uundaji wa ‘Alogarithm’ za magari hayo ili kuamua kimaadili nani afe katika ‘situation’ za namna hiyo.
Haya 'maadili' yanategemea vingi ikiwemo emotions (sio logic tu)nukiona mtoto wa primary kuna emotion unapata na ukiona bibi kizee kuna emotion unapata..maamuzi meng hufanywa kwa kufuata emotions kali zimeegemea upande upi.

Hizi emotions zinatengenezwa na kuwa controlled na sehemu ya ubongo inaitwa amygdala..Kwahyo Amygdala ndio inayokucontrol wewe na maadili yako...sio wewe.

By the way mkuu. Je, kuna experiment au kuna proof yoyote inayoweza kuelezea how hizi brains zetu zilizotengenezwa kwa neurones ambazo zimetengenezwa kwa atoms ambazo ni electrons, nucleons na protons tu, zimewezaje kuwa na free will?
 
Kaka mkubwaa kuikataa freewill kwa kigezo cha kuwepo adhabu na zawadi sio sawa.

Kwa kuwa Mungu anajua hali yote iliyopo sasa hivi, na anajua matokeo yote ya hali zote aliamua kuweka mfumo.
Na kwa kuwa pia Mungu hana upendeleo, akimpangia huyu awe raisi na mwingine awe waziri mkuu atakuwa amempendelea mmoja. Bora hao, vipi yule atakayempangia awe mnyonge mlipakodi si ndo tutasema amemuonea kabisaaa!? Ujanja hapa ni kuweka mfumo tu.

Mfumo upo na option zote na matokeo yote ambayo mtu anayafikia kiotomati kutokana na machaguo yake. Mfano atakayesoma sana, akabeba majukumu kinamna hii atakuwa raisi mwishowe. Atakayeamua kutosoma na kufanya ufundi atakuwa mpigakura. Akijiongeza kiufundi akawa kampuni kubwa atamuongoza hadi huyo rais katika sera zake! So ni utashi huru hakuna anayewekewa maamuzi kichwani kwake ni yeye anacheza na option za mfumo na kujioatia matokeo kiotomati. Ngoja niandae kamfano.
Mzee, sio rahisi kihivyo...wangapi wanaamua kutafuta hela na wangapi wanazipata? ukiangalia hizo numbers utajua kuwa matokeo hayapatikani kwa kuamua tu na kyufanya njia ili uyapate...ila kuna vitu vingi kama bahati,connections, vinaplay part.
 
Mfano huyo mtu hapo katikati akiamua kwenda pointi D ndio lengo lake basi ataenda.
Lazima atatembea hadi pointi A.
Halafu akiamua kupitia B basi atafika mahala atavuka mto kwa daraja atafika D

lakini akiamua kupitia C basi matokeo yake ataogelea mtoni ndipo atafika D
Katika maamuzi ya kupita B au C ni yeye na matokeo ya kuvuka daraja au kuogelea ni yeye amepima akaona kipi kinafaa. Yeye ndo anayesema kichwani (kwanza nna jasho bora nipitie huku hata nikaoge na kuoga). Mungu au serikali ikimpangia akavuke daraja tuu ni kumuonea hata kama ni salama zaidi kwake. Yeye amependa kuogelea mamba atapambana nao kama vipi(kwanza haamini kama mamba wapo😄).

Lakini kwa utashi-huru wake anaweza kuutumia kuamua sitaki hata kwenda pointi D mimi ntaenda kufia T au W akanyooka hadi destination

Au akaenda tu na kumaliza alfabeti hadi Z akasema mimi nikifa nataka niishie hapo. Maisha ndo hayahaya, hakuna zaidi ya alfabeti naye akafa.

Mwingine akajiaminisha kuwa kuna zaidi ya alfabeti akaziishi akatumia na nyingine za kutohoa tu mfano hiyo AC hadi M-N-O akamaliza zote na kwa imani akaamini zipo nyingine akaishi na tumaini la kuziishi basi huyo ataishi milele maana hatazimalizaga pointi zote.

Bottomline ni kwamba Mungu kaweka mfumo na pointi zote zimo humo. Mtu binafsi anachagua anapotaka kwenda na matokeo anayapata sambamba na machaguo yake. Full stop.View attachment 2481105
kuna mwingine yupo hapo ila njia pekee anayoiona ni A, yani kutokana na sababu zilizo nje ya uweo wake haoni njia X, H,D nk. Yeye anaona njia moja tu A. Je huyo tutasema ana free will?

Watu wengi Tz wanaona njia moja tu ya kufanikiwa ni kusoma, wengine wachache wanaona ni biashara, ila kuna wengine kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wao kama kuzaliwa mtoto wa Kikwete wanaona njia nyingi zaidi kama kufanya siasa, kupewa cheo na baba, kupewa hisa za mzee, kusimamia biashara za familia, kupelekwa ughaibuni, Kuiba hela za serikali nk.

watoto wengi wa masikini hawana hizo njia.
 
Mzee, sio rahisi kihivyo...wangapi wanaamua kutafuta hela na wangapi wanazipata? ukiangalia hizo numbers utajua kuwa matokeo hayapatikani kwa kuamua tu na kyufanya njia ili uyapate...ila kuna vitu vingi kama bahati,connections, vinaplay part.
Ni kani zote zinahusika katika kuleta matokeo fulani. Ila
'Shit happens' is the worst philosophy to live with. 'Shit happens for a reason' is healthy, w...jpg
sehemu ya muhimu ni mtu binafsi na yeye.

Yeye ndiye anayeamua kushirikiana na hali au kupingana nayo, kutumia kanuni au kuachana nayo na matokeo halisi yanaathiriwa sana na chaguo zake. Bila kusahau kani na mambo yote na wahusika wote; We nake things happen
 
Kusema binadamu hana free will haimaanishi kuwa anafanya mema tu, anaweza akawa anafanya yote mema na mabaya lakini bila kuchagua mwenyewe, bali kwa pressure za mazingira,kemikali kwenye ubongo, script ya simulation,randomness, au mpango wa Mungu anayeijua kesho yako.

Then sina uhuru 100% wa kufanya ninachotaka...Mtu akisema shule yetu ins uhuru mkubwa anamaanisha kuna uwezo wa kufanya mema na mabaya bila kuadhibiwa...Huwezi kusema kazini kwetu kuna uhuru ila ukichelewa sekunde mbili unakatwa mshahara,ukipoteza muda chooni unakatwa mshahara,usipokwenda kazini unafukuzwa,ukizidisha dakika 1 ya lunch huna kazi sasa hapo uhuru utakuwa wapi?
Halafu ukiachana na hiyo.... Mungu anajua kesho, kitendo cha yeye kuijua tu it means imeshaandikwa na wewe huna choice inabidi ufanye kama ililvyoandikwa

Sasa kwa Mungu hiyo option ya kupigana nae huna maana yeye ni Mungu, akisema usipohiji unaenda motoni (mfano) hauna option ya kutohiji na kupambana usiende motoni...Kitendo cha kukosa hiyo option ndio ukosefu wa uhur wenyewe naozungumzia

Sasa kwa huo mfano hauoni kuwa wasukuma wa sasa hawana choice maana mazingira yanawafosi kukijua kiswahili na kusahau kisukuma au kukiswahilisha?? unakuta mtu anaongea kisukuma kama kiswahili. Hakuna anayeweza kucontrol mazingira akulia sehemu hakuna muingiliano hatajua kiswahili na aliyekulia spain hatojua kisukuma..Kuongea kwetu kuko limited na mazingira ya jamii zinazotuzunguka..Hata ukisema hutaki kuvaa kama waswahili huwezi kuamua kutembea uchi kwa sababu mazingir yoyote hayakuruhusu kwakuwa hauna huo uhurukulingana na tamduni za binadamu


Zamani walivaa magome ya miti lakini kuotokana na sababu zilizo nje ya uwezo wao,mazingira yalibadilika (maana hakuna mtu mmoja anayecontrol mazingira yote) utandawazi ukaja ikabidi wavae majoho,kanzu na suti. Na sasa kwa haya mazingira mapya hawawezi tena kuvaa magome ya miti

Trust me, hata mpoto kuna mazingira yaliyompelekea kuwa mtu wa kuvaa hivyo, angekuwa mtoto wa Bakhresa angevaa hivyo? Angekuwa ridhiwani je? Kwahyo ni mazingira fulani either alipokulia,shule alizosoma au marafiki na watu aliojuana nao ndio wamempelekea kufanya kuwa anavaa hivyo.

Lakini hatuwezi kuchagua kuacha kula

Ni lini ulimkuta msomi wa PHd Kwa akili zake timamu anaokunywa maji ya lamboni? anakula mkate wa jalalani?? Huo uhuru umeshaondoshwa na elimu yake

Hizo cnsequences ndio zinalimit uhuru wenyewe...maaana ukiwa na uhuru kamili hakuna consequences.
Tukienda kwa notion hiyo Basi hata wafungwa sasa tutasema wako huru ila wakiamua kuvuka getti kuna 'cosequemce ya kupigwa risasi. Wako huru kulala mpaka saa 3 asubuhi ila wakifanya hivyo kuna consequence ya virungu,,,,mkuu sidhani kama huo ni uhuru.

Hizo consequences ndio zinauziba uhuru wenyewe

Unawezaje kupiga bao 20? Halafu siongelei kujaribu naongelea kufanya

'Ukitaka' nani anayetaka? maana hizo kemikali ndio zinapelekea wewe kutaka au kutotaka kitu...Unaweza ukaamua kuacha mihadarati kisa dopamine inazidi,,,kumbe inayokuachisha hio ni oxytocin inayohusika na kukufanya uridhike na jambo fulan

Hakuna binadamu ambaye hatafuti furaha kwa namna moja au nyingine labda huyo ni roboti...mkuu tunajadili uhalisia na binadamu wa kawaida sio AI

ila unakubali ukivittumia vinakuendesha sio? sasa nilitumia kama mfano kuonesha jinsi kemikali extternal manmade zinakuendesha kuwa 'abnormal' basi hiyo inaprove kuwa hizi kemikali internal naural ndio zinakufanya kuwa 'normAL'
Mkuu nadhani hoja rahisi ambayo una ‘miss’ ni kudhani kuwa kuwepo kwa ‘consequences’ kuna maanisha kukosekana kwa ‘Free will’

Sasa kiuhalisia hapa duniani HAKUNA JAMBO LOLOTE LILE AMBALO MTU ANAWEZA FANYA LIKAWA HALINA ‘CONSEQUENCES’, sijui kuhusu mbinguni.

Ukishaelewa hilo utajua kuwa kila kitu kinakupa chaguo, unavyosema mazingira yanakulazimu si kweli ni ‘excuse’ tu unaitumia kufanya au kukwepa jambo fulani.

Mathalan, Mwanafunzi anaekaa mbali na shule, kila siku anapoamka anakutana na ‘options’ mbili
1. Aende shule ila ‘consequences’ zake ni kuwa ataacha usingizi, atapigwa na baridi, ataloa umande na anaweza kusoma vizuri asifaulu au hata akifaulu asijeona matunda ya matendo yake.

2. Abaki alale ila ‘consequences’ ni kuwa jamii itamuona mzembe, atawaudhi wazazi, atafukuzwa shule, hatofaulu mitihani n.k na pia anaweza kutokwenda na akawa na mbadala wa kusoma na akafaulu

Kwahiyo japo mazingira yamekaa hivyo bado mwanaadamu ana chaguo la kufanya anachotaka yuko huru.

Umesema kuhusu Wasukuma na Mpoto kuwa mazingira yamewalazimisha, hapana sio kwa 100%, wakiamua wenyewe wanaweza fanya kinyume ila ‘consequences’ zipo pale pale.

Kuhusu kemikali wenzetu wanaobadili jinsia hufanya hivyo, au wale ambao husumbuliwa na ‘hormonal imbalances’ hufanya hivyo, hii inakuonesha kuwa tuko huru kujiamualia hayo mazingira ni ‘excuses’ tu (SITETEI LGBTQ LAKINI NI MZURI SANA KUONESHA UHURU TULIO NAO)
Mtu kazaliwa mwanaume akaoa na kuzaa watoto akiwa mwanaume, baada ya muda akajihisi hayuko ‘comfortable’ kuwa mwanaume anakwenda kwa wataalam kubadili jinsia na kuwa mwanamke…. Hapa ungesemq mazingira yamemlazimu kuwa ME ila hapana, ameamua kuyakabili na kuchagua anachotaka akiwa huru. Sijui unanielewa mkuu? Japo ‘consequences’ huwezi zikwepq ziko pale pale chochote utachoamua kukifanya.


Ila ukijenga hoja ati mazingira yanatulazimu tuwe watu fulani inakuwa hoja dhaifu sana, maana sidhani kamq tungefikia hatua hii ya maendeleo tuliyo nayo sasa… tungeendelea kula nyama mbichi, tukaishi mapangoni, pengine tungendelea kuishi utumwani lakini kwakuwa sisi ni viumbe huru tukaona hapana, tukaamua kuyakabili mazingira ‘against all odds’ tuautupilia mbali utumwa na kila siku tunabadili namna tunavyoishi sababu tunachagua kufanya hivyo


Ng’ombe alikuwa anakula majani tangu karne ya 1 na anaendelea kulq majani hayo mpaka leo karne ya 21, tazama wanaadamu tunavyobadili vyakula vyetu kila siku, ni kwa sababu tuna ‘free will’.

Kuhusu kila kitu kupangwa mbinguni wewe binafsi unajua umepangiwa nini?
Ni dhahiri hujui, sasa unawezaje kusema kila unachofanya ni vile vile ulivyopangiwa?
Kikawaida huwezi leta madai hayo, kwakuwa hatujui ila tunaambiwa tu bado ninaamini mimi na wengine wote, hata wale walio utumwani tuna ‘free will’.

NB: kuwepo kwa ‘consequences’ haina maana kukosekana kwa ‘free will’ hili ni muhimu sana usisahau.
 
Ndiyo,mwanzoni ukitengeneza hizo sakitii inakuwa rahisi kubadili maamuzi, mfano ukijifunza leo umalaya, ni rahisi kuacha ila kwa mtu ambaye tokea azaliwe anakulia kwenye umalaya ni ngumu kuacha...ndomaana kuna msemo 'you cant turn a ho into a housewife' 'you cant teach an old dog new tricks'..Kuna stage zile circuit zinakuwa zimekomaa kiasi kwamba kuzibadili ni near impossible (kama extrovert kuwa introvert au vice versa)
Ni ngumu ila haina maana haiwezekani, mkuu malaya anaweza kuwa mke mzuri tu nazungumza hii nikimaanisha. Leo mtu kuwa A haina maana hawezi kuwa B.
‘Introvert’ kuwa ‘Extrovert’ inawezekana kabisa japo ni ngumu ila haimaniishi haiwezekani, mkuu usitafsiri ugumu wa kufanya jambo kuwa ni kukosa uhuru wa kulifanya, la.

Mtu yeyote akifanya jitihada sahihi anaweza kuwa yoyote.
Wewe kujihisi uko huru haimaanishi uko huru, huko kujihisi huru kunaweza kuwa ni illusion ubongo wako unakutengenezea.
Ni kweli.
Unaweza kuamua kuwa daktari halafu ile umemaliza kusoma diploma ya CO unataka kuapply degree, serikali ikasema udaktari lazima upite form 6, na kufaulu bado ni ishu ya bahati maana unaweza kusoma Organic chemistry mtihani ukatoka inorganic.
Ikiwa kweli unataka kuwa daktari basi unaweza kwenda nchi nyingine kukamilisha ndoto zako.

Kuwepo kwa ugumu haina maana mtu kakosa uhuru.
Na mwingine anaweza asipende kuwa mwalimu ila akashangaa mambo yalivyoenda mpaka akawa mwalimu (walimu wengi hawakupanga kuwa walimu)
Sasa huyu mtu ni kwamba KAAMUA KWA MOYO WAKE kuwa mwalimu lakini sababu ndiyo hutofautiana, ila ANGEAMUA KWA MOYO wake kuwa anachotaka nina hakika asingekuwa mwalimu.

Tusitumie mazingira kama ‘excuse’ ya kutofanya jambo fulani kiasi tukasema hatuna ‘free will’

Leo tungesingizia mazingira kuwa sisi hatuwezi kupaa sidhani kama kuna mtu angegundua ndege, MAZINGIRA NI YETU KUYAKABILI ILI TUWE TUNACHOTAKA.

Nioneshe harakati moja ambayo ilikuwa ni rahisi kupata matokea, tazama Uhuru wa kitaifa, Fikra za kikomunisti na Kiliberali, Ufeministi, Udini n.k hawa wote wangesingizia mazingira kamwe tusingekuwa na hivyo vitu.

Yesu (AS) angesingizia ufinyu wa fursa kwenye utawala wa Roma kamwe asingeweza hubiri amani ungesema “mtu akihubiri anatundikwa msalabani” ile ni ‘consequences’ ambayo yesu (as) alichagua maana angeweza kukaa kimya ila akaona hapana, ana wajibu wa kusema ukweli na matokeo yake dunia karibia yote inafuata mafundisho yake.

Vile vile kwa Muhammad (pbuh) mazingira hayakuruhusu ahubiri uislam lakini tazama alivyoyakabili, Vile vile kwa Mussa (as), Remus na kaka yake wasingeyakabili mazingira Himaya ya Roma ingetoka wapi, Osman na Orhan nao wangesingizia mazingira Ottoman ingetoka wapi?, Xenophon angesingizia mazingira wangerudi hai? Wagiriki wangesingizia mazingira wangewezaje kulikabili jeshi lenye nguvu la Uajemi?
Wewe unajuaje kama haupo kwenye algorithm??
Kwa sababu mimi ni mwanaadamu, mimi ndiye ninaetengeneza hiyo algorithm.
Roboti anajijuaje kuwa anafata algorithm??
Sijui mkuu, Hili swali tuyaulize maroboti, tena tupate bahati kuyauliza yenye akili za kutosha kulijua hilo.
Kuna experiment unaweza kuifanya kuprove kuwa huu ulimwengu sio simulation au sio scripted?
Vizuri sana, kuna ‘experiment’ unaweza fanya kuthibitisha kuwa hii dunia ni ‘scripted’ au ‘simulation’?

Nina uhakika huwezi na mimi siwezi, hayo maswali yanalenga kuvuruga mada kwa kupandikiza mashaka na hofu kwa kila kitu hapa duniani.
Nadhani vitu kama coincidence,karma,deja vu,destiny,prophesies nk. vinaprove huu ulimwengu ni scripted
Unadhani, unaweza thibitisha kwa ushahidi jadidi mkuu?

Maana hata mimi naeza kudhani chochote kile. Mf. Naweza kudhani wewe ni muongo.
Haya 'maadili' yanategemea vingi ikiwemo emotions (sio logic tu)nukiona mtoto wa primary kuna emotion unapata na ukiona bibi kizee kuna emotion unapata..maamuzi meng hufanywa kwa kufuata emotions kali zimeegemea upande upi.
Hapana, Maadili hayahusiani na hisia binafsi.
Jambo haliwi sahihi kimaadili kwa sababu kuna mtu ana’feel’ kitu fulani, japo ni lazima nikubali kuwa hakuna ‘consensus’ kwenye hili ila ni mada pana ambayo haina mwisho.

Ukisema hisia kila mtu ana namna anavyohisi kuhusu jambo fulani, Hitler alihisi wayahudi hawafai kuishi, je alikuwa sahihi?
Ndiyo, alikuwa sahihi kwa upande wake lakini vipi kuhusu wayahudi wenyewe?

Wapo wazungu walihisi watu weusi si wanaadamu bali ni wanyama, je walikuwa sahihi?

Maadaili kamwe huwezi yanasibisha na hisia.
Hizi emotions zinatengenezwa na kuwa controlled na sehemu ya ubongo inaitwa amygdala..Kwahyo Amygdala ndio inayokucontrol wewe na maadili yako...sio wewe
Mkuu unajua kuwa hii njia uliyoichagua inakwenda shimoni?
Haya ukisema “wewe” unamaanisha MIMI, nakuuliza MIMI ni nani? (Usinitajie jina, nataka nione ni kwa namna gani unaweza nitenganisha mimi na ubongo wangu)
By the way mkuu...je, kuna experiment au kuna proof yoyote inayoweza kuelezea how hizi brains zetu zilizotengenezwa kwa neurones ambazo zimetengenezwa kwa atoms ambazo ni electrons,nucleons na protons tu...zimewezaje kuwa na free will??
Mpaka sasa sijakutana na ripoti kuhusu jaribio lolote ulilotaja, ila naweza kukwambia kwa uhakika ktk kila jambo unalotaka kufanya ni lazima akili yako ikupe ‘options’, na wewe aidha kwa kujua au kutojua (na kutojua mara nyingi ni kutotaka kufikiri) utachagua mojawapo ya ‘option’ iwe utatumia hisia kuchagua ama ‘reasoning’ hiyo ni juu yako lakini kila kitu kinakupa nafasi ya kuchagua.

Hata ukisoma maneno haya una nafasi ya kuchagua aidha kubonyeza ‘Like’ ama kuacha au kujibu ama kupuuza.

UKO HURU MKUU CHAGUA CHOCHOTE UTAKACHO ILA JUA KINA ‘consequences’ hili USISAHAU.
 
We are determined, no free will at all! Can you choose to kill? I think you are determined to kill, may be devil is the one directing you to kill.
Huu ni uvivu wa kufikiri, ‘You can kill if you want, but you will spend the rest of your life in jail IF you are convicted’

Bado una uhuru aidha uue au usiue, ila sisi watu wa maadili tunatumia maisha yetu kukushawishi usiuue.
 
Mfano huyo mtu hapo katikati akiamua kwenda pointi D ndio lengo lake basi ataenda.
Lazima atatembea hadi pointi A.
Halafu akiamua kupitia B basi atafika mahala atavuka mto kwa daraja atafika D

lakini akiamua kupitia C basi matokeo yake ataogelea mtoni ndipo atafika D
Katika maamuzi ya kupita B au C ni yeye na matokeo ya kuvuka daraja au kuogelea ni yeye amepima akaona kipi kinafaa. Yeye ndo anayesema kichwani (kwanza nna jasho bora nipitie huku hata nikaoge na kuoga). Mungu au serikali ikimpangia akavuke daraja tuu ni kumuonea hata kama ni salama zaidi kwake. Yeye amependa kuogelea mamba atapambana nao kama vipi(kwanza haamini kama mamba wapo😄).

Lakini kwa utashi-huru wake anaweza kuutumia kuamua sitaki hata kwenda pointi D mimi ntaenda kufia T au W akanyooka hadi destination

Au akaenda tu na kumaliza alfabeti hadi Z akasema mimi nikifa nataka niishie hapo. Maisha ndo hayahaya, hakuna zaidi ya alfabeti naye akafa.

Mwingine akajiaminisha kuwa kuna zaidi ya alfabeti akaziishi akatumia na nyingine za kutohoa tu mfano hiyo AC hadi M-N-O akamaliza zote na kwa imani akaamini zipo nyingine akaishi na tumaini la kuziishi basi huyo ataishi milele maana hatazimalizaga pointi zote.

Bottomline ni kwamba Mungu kaweka mfumo na pointi zote zimo humo. Mtu binafsi anachagua anapotaka kwenda na matokeo anayapata sambamba na machaguo yake. Full stop.View attachment 2481105
Safi sana mkuu👏
 
Back
Top Bottom