Je, bustani ya Eden haipo Tanzania?

Je, bustani ya Eden haipo Tanzania?

Tanzania Nchi Yetu Sote

JF-Expert Member
Joined
Mar 12, 2017
Posts
505
Reaction score
872
Baada ya kusoma kwangu somo la historia ninashawishika kuamini kuwa bustani ya Eden ipo mkoani Arusha eneo la Olduvai gorge ambapo paligunduliwa fuvu la mtu wa kale duniani.

Sote tutakumbuka juu ya uvumbuzi uliofanywa na Dkt. Leakey na mkewe Mary Leakey wote hawa ni wazungu na uvumbuzi wao haujawahi kupingwa popote mpaka sasa. Kwa wao (wazungu) kuvumbua fuvu la mtu wa kale duniani kwangu mimi naona hilo ni fuvu la Adam kwani siamini kama kuna mtu wa kale zaidi ya Adam. Kutokana na kutopingwa kwa uvumbuzi wao na ukimya wa wazungu juu ya suala hilo ni dhahiri kuwa:

1. Ni kweli lile ni fuvu la mtu wa kale duniani.

2. Ni kweli lile ni fuvu la Adam.

3. Ni kweli kuwa bustani ya Eden ipo nchini Tanzania eneo.

lilipovumbuliwa fuvu la Adam.
Pamoja na maelezo katika kitabu cha Biblia juu ya Adam kufukuzwa bustanini baada ya kuasi lakini ni wazi kuwa kama bustanini ndipo Adam alipokuwa akijipatia riziki yake basi hawezi kuwa alikwenda kuishi mbali na bustani hata baada ya kufukuzwa.

Naomba tujadili ili tuupate ukweli na kuisimamisha historia ya kweli juu ya fuvu lililovumbuliwa Olduvai Gorge.
 
Baada ya kusoma kwangu somo la historia ninashawishika kuamini kuwa bustani ya Eden ipo mkoani Arusha eneo la Olduvai gorge ambapo paligunduliwa fuvu la mtu wa kale duniani.

Sote tutakumbuka juu ya uvumbuzi uliofanywa na Dkt. Leakey na mkewe Mary Leakey wote hawa ni wazungu na uvumbuzi wao haujawahi kupingwa popote mpaka sasa. Kwa wao (wazungu) kuvumbua fuvu la mtu wa kale duniani kwangu mimi naona hilo ni fuvu la Adam kwani siamini kama kuna mtu wa kale zaidi ya Adam. Kutokana na kutopingwa kwa uvumbuzi wao na ukimya wa wazungu juu ya suala hilo ni dhahiri kuwa:

1. Ni kweli lile ni fuvu la mtu wa kale duniani.

2. Ni kweli lile ni fuvu la Adam.

3. Ni kweli kuwa bustani ya Eden ipo nchini Tanzania eneo.

lilipovumbuliwa fuvu la Adam.
Pamoja na maelezo katika kitabu cha Biblia juu ya Adam kufukuzwa bustanini baada ya kuasi lakini ni wazi kuwa kama bustanini ndipo Adam alipokuwa akijipatia riziki yake basi hawezi kuwa alikwenda kuishi mbali na bustani hata baada ya kufukuzwa.

Naomba tujadili ili tuupate ukweli na kuisimamisha historia ya kweli juu ya fuvu lililovumbuliwa Olduvai Gorge.
Ipo turkey
 
Baada ya kusoma kwangu somo la historia ninashawishika kuamini kuwa bustani ya Eden ipo mkoani Arusha eneo la Olduvai gorge ambapo paligunduliwa fuvu la mtu wa kale duniani.

Sote tutakumbuka juu ya uvumbuzi uliofanywa na Dkt. Leakey na mkewe Mary Leakey wote hawa ni wazungu na uvumbuzi wao haujawahi kupingwa popote mpaka sasa. Kwa wao (wazungu) kuvumbua fuvu la mtu wa kale duniani kwangu mimi naona hilo ni fuvu la Adam kwani siamini kama kuna mtu wa kale zaidi ya Adam. Kutokana na kutopingwa kwa uvumbuzi wao na ukimya wa wazungu juu ya suala hilo ni dhahiri kuwa:

1. Ni kweli lile ni fuvu la mtu wa kale duniani.

2. Ni kweli lile ni fuvu la Adam.

3. Ni kweli kuwa bustani ya Eden ipo nchini Tanzania eneo.

lilipovumbuliwa fuvu la Adam.
Pamoja na maelezo katika kitabu cha Biblia juu ya Adam kufukuzwa bustanini baada ya kuasi lakini ni wazi kuwa kama bustanini ndipo Adam alipokuwa akijipatia riziki yake basi hawezi kuwa alikwenda kuishi mbali na bustani hata baada ya kufukuzwa.

Naomba tujadili ili tuupate ukweli na kuisimamisha historia ya kweli juu ya fuvu lililovumbuliwa Olduvai Gorge.
Let me school you before I go to bed. .

Adam na Eva hawakuwa watu wa kwanza duniani hivyo duniani kulikuwa na watu wengine wengi tu ambao Mungu aliwaumba. Adamic period (kihistoria kaisome) ni kipindi ambacho Mungu aliamua kumuumba mwanaume na mwanamke ili awatolee mfano na kupitia hawa mataifa yawajue. Sasa bustani ya Eden ilizungukwa na mito mikubwa minne, ambayo haipo na haikuwepo Tanzania sasa kwa nini udhanie kuwa bustani hii ilikuwa Tanzania?

Nanukuu mito hii ilikuwa Pishoni, Gihoni, Hidekeli na Frati. Jina la kwanza ni Pishoni; ndio unaozunguka nchi yoye ya Havila, ambako kuna dhahabu ... Jina la mto wa pili ni Gihoni; ndio unaozunguka nchi yote ya Kushi. Jina la mto wa tatu ni Hidekeli; ndio unaopita mbele ya Ashuru. Na mto wa nne ni Frati. "Utambulisho halisi wa Mito ya Pishoni na Gihoni haujulikani, lakini Mito ya Hidekeli na Frati inajulikana.

Ukinionyesha mito hii Tanzania kwanza kisha tuanze mda yetu kuongea. .
 
Baada ya kusoma kwangu somo la historia ninashawishika kuamini kuwa bustani ya Eden ipo mkoani Arusha eneo la Olduvai gorge ambapo paligunduliwa fuvu la mtu wa kale duniani.

Sote tutakumbuka juu ya uvumbuzi uliofanywa na Dkt. Leakey na mkewe Mary Leakey wote hawa ni wazungu na uvumbuzi wao haujawahi kupingwa popote mpaka sasa. Kwa wao (wazungu) kuvumbua fuvu la mtu wa kale duniani kwangu mimi naona hilo ni fuvu la Adam kwani siamini kama kuna mtu wa kale zaidi ya Adam. Kutokana na kutopingwa kwa uvumbuzi wao na ukimya wa wazungu juu ya suala hilo ni dhahiri kuwa:

1. Ni kweli lile ni fuvu la mtu wa kale duniani.

2. Ni kweli lile ni fuvu la Adam.

3. Ni kweli kuwa bustani ya Eden ipo nchini Tanzania eneo.

lilipovumbuliwa fuvu la Adam.
Pamoja na maelezo katika kitabu cha Biblia juu ya Adam kufukuzwa bustanini baada ya kuasi lakini ni wazi kuwa kama bustanini ndipo Adam alipokuwa akijipatia riziki yake basi hawezi kuwa alikwenda kuishi mbali na bustani hata baada ya kufukuzwa.

Naomba tujadili ili tuupate ukweli na kuisimamisha historia ya kweli juu ya fuvu lililovumbuliwa Olduvai Gorge.
Fuvu lililogunduliwa olduvai Gorge na Dk Leakey ni la kale lakini sio kwamba ndio la kale zaidi kuliko yote duniani..Ethiopia mwaka jana kuligunduliwa fuvu la kale zaidi walilolipa jina la OMO 1..kwahiyo kwa nadharia zako tuhamishe mjadala tuseme sasa Eden ilikuwa Ethiopia maana ndipo kulipogunduliwa fuvu la kale zaid ya la Olduvai Gorge
 
Bila shaka fumbo liko kwenye kutofautisha kati ya mahali halisi(Place ) na mazingira (Enviroment) , eden ni mazingira ya uwepo wa Mungu unlike tunavyotaka kuwaza kuwa ni sehemu ambayo tunaweza kwenda kwa miguu. Na Kimsingi Biblia imejaa mafumbo matupu kwahiyo tunahitaji sana msaada wa Roho wa Mungu zaidi kuliko akili zetu kuelewa baadhi ya mambo
1Kor 2:10
 
Bila shaka fumbo liko kwenye kutofautisha kati ya mahali halisi(Place ) na mazingira (Enviroment) , eden ni mazingira ya uwepo wa Mungu unlike tunavyotaka kuwaza kuwa ni sehemu ambayo tunaweza kwenda kwa miguu. Na Kimsingi Biblia imejaa mafumbo matupu kwahiyo tunahitaji sana msaada wa Roho wa Mungu zaidi kuliko akili zetu kuelewa baadhi ya mambo
1Kor 2:10
Wanaosomea Theolojia huwa wanasoma nini kama inahitaji roho wa Mungu kutafsiri Biblia? Unafahamu kuwa Biblia ni mkusanyiko wa mila na desturi za jamii mbalimbali zilizoishi zama zao kwa jamii zao?
 
Fuvu lililogunduliwa olduvai Gorge na Dk Leakey ni la kale lakini sio kwamba ndio la kale zaidi kuliko yote duniani..Ethiopia mwaka jana kuligunduliwa fuvu la kale zaidi walilolipa jina la OMO 1..kwahiyo kwa nadharia zako tuhamishe mjadala tuseme sasa Eden ilikuwa Ethiopia maana ndipo kulipogunduliwa fuvu la kale zaid ya la Olduvai Gorge
Sasa walishindwa nini kusema ni la kale lakini si la kale zaidi ya yote na wakaishia tu kusema ni fuvu la kale?
 
Inasemekana ilikua hapo middle East Iraqi.
The location of Eden is described in the Book of Genesis as the source of four tributaries. Various suggestions have been made for its location:[3] at the head of the Persian Gulf, in southern Mesopotamia (now Iraq) where the Tigris and Euphrates rivers run into the sea;[4] and in Armenia.[5][6][7]
 
Sasa bustani ya Eden ilizungukwa na mito mikubwa minne, ambayo haipo na haikuwepo Tanzania sasa kwa nini udhanie kuwa bustani hii ilikuwa Tanzania?

Nanukuu mito hii ilikuwa Pishoni, Gihoni, Hidekeli na Frati. Jina la kwanza ni Pishoni; ndio unaozunguka nchi yoye ya Havila, ambako kuna dhahabu ... Jina la mto wa pili ni Gihoni; ndio unaozunguka nchi yote ya Kushi. Jina la mto wa tatu ni Hidekeli; ndio unaopita mbele ya Ashuru. Na mto wa nne ni Frati. "Utambulisho halisi wa Mito ya Pishoni na Gihoni haujulikani, lakini Mito ya Hidekeli na Frati inajulikana.

Ukinionyesha mito hii Tanzania kwanza kisha tuanze mda yetu kuongea. .
Mleta mada yuko sawa ila ana makosa kulitaja hilo fuvu, hata weye uko sawa, lk jua kwamba mito ya Pishoni na gihoni ni Mto Nile ya leo! nchi ya Havila ni zimbabwe yenye dhahabu wazungu wametuficha mengi !

na Biblia unayo soma leo imechezewa mnoo! Bustani ya edeni ilikuwa kuuubwa sana siyo sehemi ndogo tu km ilivo leo!
 
Mleta mada yuko sawa ila ana makosa kulitaja hilo fuvu, hata weye uko sawa, lk jua kwamba mito ya Pishoni na gihoni ni Mto Nile ya leo! nchi ya Havila ni zimbabwe yenye dhahabu wazungu wametuficha mengi !

na Biblia unayo soma leo imechezewa mnoo! Bustani ya edeni ilikuwa kuuubwa sana siyo sehemi ndogo tu km ilivo leo!
Nitajie hiyo mito minne iliyozunguka Eden. Tuanze hapo Ili nikueleweshe sawa. .
 
M
Nitajie hiyo mito minne iliyozunguka Eden. Tuanze hapo Ili nikueleweshe sawa. .
Mkuu yaani Naomba urudie kuyasoma ili twende sawa make nimeitaja kabisaaa!
 
Let me school you before I go to bed. .

Adam na Eva hawakuwa watu wa kwanza duniani hivyo duniani kulikuwa na watu wengine wengi tu ambao Mungu aliwaumba. Adamic period (kihistoria kaisome) ni kipindi ambacho Mungu aliamua kumuumba mwanaume na mwanamke ili awatolee mfano na kupitia hawa mataifa yawajue. Sasa bustani ya Eden ilizungukwa na mito mikubwa minne, ambayo haipo na haikuwepo Tanzania sasa kwa nini udhanie kuwa bustani hii ilikuwa Tanzania?

Nanukuu mito hii ilikuwa Pishoni, Gihoni, Hidekeli na Frati. Jina la kwanza ni Pishoni; ndio unaozunguka nchi yoye ya Havila, ambako kuna dhahabu ... Jina la mto wa pili ni Gihoni; ndio unaozunguka nchi yote ya Kushi. Jina la mto wa tatu ni Hidekeli; ndio unaopita mbele ya Ashuru. Na mto wa nne ni Frati. "Utambulisho halisi wa Mito ya Pishoni na Gihoni haujulikani, lakini Mito ya Hidekeli na Frati inajulikana.

Ukinionyesha mito hii Tanzania kwanza kisha tuanze mda yetu kuongea. .
Yaani iko hivi Bustani ina mito minne! lkn inajulikana miwili tu! miwili mingine imefichwaa maksudi tu! ili msijitambue nyie weusi!........ nchi ya Kush ni Ethiopia ya leo!! haikuwahi tawaliwa!
 
M

Mkuu yaani Naomba urudie kuyasoma ili twende sawa make nimeitaja kabisaaa!
Mito Tigris na Euphrates kutokana na historia iko huko Iraq na inamwaga maji kwenda kwa bahari na Armenia.

Tatizo kiswahili kigumu
Garden of Eden ilizungukwa na mito minne. Hiyo mito minne ambayo wewe unadai ni mto Nile pekee😬
Wewe msomi nionyeshe mito minne ambayo inaizunguka garden of Eden usiassume sijui Iko Zimbabwe
Biblia inajieleza kuwa Kuna mito minne.
Dunia nzima Kuna dhahabu, sio Zimbabwe tu. Hata marekani, hata ulaya, hata Arabs jagwan huko. Kila Kona Kuna dhahabu hakuna nchi ambayo Haina dhahabu chini
 
Yaani iko hivi Bustani ina mito minne! lkn inajulikana miwili tu! miwili mingine imefichwaa maksudi tu! ili msijitambue nyie weusi!........ nchi ya Kush ni Ethiopia ya leo!! haikuwahi tawaliwa!
Kwa hiyo Ethiopia peke yake haikuwah tawaliwa? Africa Kuna Liberia pia. Lakin Kuna nchi ambazo hazijawah tawaliwa kipindi hicho
Zimbabwe imetawaliawa ukumbuke
 
Biblia Iko clear kuwa garden of Eden ilizungukwa na mito Pishon, Gihon, Euphrates na Tigris.
Mito Pishon na Gihon bado location yake haijatambulika
Ila Euphrates na Tigris hii mito ipo mpaka Leo hii inatambulika. Na hii ni mito tokea ancient world mpaka Leo sasa uwepo wake sio coincidence

Cha kujiuliza hii mito mingine imepotele wapi. Lakini kingine hii bustani ilikuwa inaelea kulingana na historia. Japo ilikuwa dunian ilikuwa inaelea juu ya nchi.


Ukisema iko Zimbabwe au Tanzania au Ethiopia without showing four rivers ni Bure. Je mito mto Nile unahawanyika kuwa Pishon na Gihon? Tuonyeshe kwenye Raman unahawanyika wapi. Ili tufanye assumption 😬
 
Kwa hiyo Ethiopia peke yake haikuwah tawaliwa? Africa Kuna Liberia pia. Lakin Kuna nchi ambazo hazijawah tawaliwa kipindi hicho
Zimbabwe imetawaliawa ukumbuke
Yes nakubali Liberia haikuwahi tawaliwa ajili ya kurudishwa watumwa weusi lkn pia inasemekana Biashara ya utumwa ni changa la macho sababu weusi weengi asili yao ni America pia!

weusi wengi walitawala na kuishi Ulaya lkn hawasemwi! hata christopher columbus yasemekana ni mweusi! chunguza uone!

kuna tawala nyingi sana za weusi ziliishi na kutawala America! lkn zimezimwa km ilivyo zimwa Egypt pamoja na masanamu yanayoonyesha kabisa kuwa hao walikuwa waafrica lkn wengi hamuamini hayo !!

Kitu ambacho mzungu Mkoloni na muuza watumwa hakutaka kabisaa mweusi akipate ni Elimu!
 
Hilo fuvu la kale lenyewe unalojengea hoja lilibuniwa ili kupinga ishu ya Adam na Hawa...

Kitu ninachohuzunika sana ni hiki cha kusema bustani (hiyo waliyoipa jina la Eden) ilikuwa duniani ambapo kumesababisha kuibuka hoja nyingi na matusi ya waziwazi juu ya Adam na mkewe Hawa

Sent from my SM-G532F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom