Kuna ile dhana ya kiuongozi ambapo mtu anajitoa au ana declare interest kwenye jambo linalomhusu ili kusiwe na upendeleo nitatoa mifano ifuatayo.
1. MAHAKAMA
Majaji huwa wanajitoa kwenye kesi aidha zinazowahusu au ambazo wao ni washtakiwa.
2. NECTA
Baraza la mitihani huwa haliruhusu mwalimu kusahihisha au kusimamia shule anayofundisha au ambayo aliisimamia mitihani ndani ya miaka minne.
Swali.
Kwanini serikali ya ccm inasimamia chaguzi wakati na yenyewe ni mshindani? Je hii ni sawa?
Kama unadhani umenijibu kwa akili sana subiri wababe waje utajibiwa sawia.Hapa una tatizo moja, nadhani ni Msaliti au sana sana ni CHADEMA. Kuna Muhimili mitatu: Bunge. Mahakama, na Rais - collectively huitwa SERKALI au DOLA. Mkuu wa Dola ni Rais. Akimteua Chancellor wa SUA au Jaji Mkuu, au CEO wa TANESCO, huyo atakuwa mteule wa DOLA, si wa CCM. Unakosea sana kusema Time ya Uchaguzi huchaguliwa na CCM. Kazi ya Serkali (I mean Rais, Bunge na Mahakama) ni kulinda amani kwa kuhakikisha Kanuni na Taratibu zinafuatwa. Hiyo ndiyo hali halisi, iko hivo hivo I doa, Ufaransa, USA na Uingreza. Unakosea sana kudhani Rais ni CCM.