Je, Evolution ni Ukweli au Nadharia tu?

Je, Evolution ni Ukweli au Nadharia tu?

Mcqueenen

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2019
Posts
6,843
Reaction score
11,702
Mwaka 1859 mwanabaiolojia Charles Darwin alichapisha kitabu chake kuhusu chanzo cha viumbe wote duniani chenye jina “On the origin of species” Kilichoelezea theory yake ya evolution. Darwin alisema kwamba hivi viumbe vyote tunavyoviona leo (Aina Zaidi ya million 8.6) vikizagaa kwenye uso wa dunia havikuwa hivyo milele tangu mwanzo, lakini vilitokana na mabadiliko ya muda mrefu yanayoitwa evolution.
Evolution ni mchakato ambao aina mbalimbali za viumbe husitawi kutoka maumbo ya awali (viumbe vya awali) wakati wa historia ya dunia.
Darwin alielezea kwa ndani jinsi viumbe vinabadilika kulingana na sababu mbalimbali na akaelezea mechanism inayosababisha viumbe kubadilika na kutengeneza viumbe wapya (specie formation)
Mechanism kuu ni mbili ambayo ni Natural selection/Uteuzi wa asili na Variation/Tofauti katika viumbe.
i. Variation: Viumbe havifanani, kutokana na randomness/unasibu wa uzazi (Watoto hawafanani 100% na wazazi) na pia kuna mutation (Mabadiliko katika gene za viumbe) husababisha viumbe wa aina moja wasifanane. Mfano unaweza kufuga kuku wekundu tu bandani lakini baada ya vizazi kadhaa unaweza kuona kuku wanazaliwa wenye rangi tofauti.
ii. Natural selection/Uteuzi wa asili : Mazingira husababisha viumbe wenye sifa nzuri kuishi na wale wenye sifa mbaya hupotea. Hivyo katika mfano hapo juu, ikitokea waganga wanapenda kuku wekundu basi wale kuku wekundu watapotea lakini wale wengine wenye rangi tofauti wataishi….Hivyo baada ya muda mrefu itaweza kutokea kuku wa aina tofauti na wale wa mwanzo na kuleta aina nyingine ya kuku...Hii process ikiendelea kwa muda mrefu inaweza kutokea aina ya viumbe kama kuku lakini wametofautiana sana na kuku mpaka wanashindwa kuzaliana na kuku wa kawaida (Hivyo kiumbe kipya kinakuwa kimepatikana)



Lakini leo ni May Mwaka 2022 AD (Takriban miaka 163 baadae) Bado watu wanabishana kama hii concept ya Evolution ya Darwin ni ukweli (Fact) au ni nadharia tu (Theory).
Kwenye huu uzi nataka nielezee kama hii evolution ni fact au ni theory tu, na nitajaribu kujibu baadhi ya maswali yanayowasha vichwa vya watu wengi kuhusu evolution, hivyo twende Pamoja.
Ikumbukwe kipindi Darwin anachapisha kitabu chake Nyanja mbalimbali za kisayansi kama Genetics, embryology, Anatomy zilikuwa hazijatanuka na kuwa kama leo. Hata fossils zilikuwa hazijagunduliwa kwa wingi kama leo, Hivyo Darwin alipingwa na watu wengi sana kwakuwa kipindi hicho watu wengi waliamini Dunia iliumbwa kwa mara moja miaka isiyozidi 6000 nyuma. Kwakuwa leo Nyanja hizo zimetanuka na tunajua mengi Zaidi basi tuyapitie hayo mengi kwa kifupi.
i. Anatomy;
Viumbe wengi wanafanana maumbile kuashiria kuwa wana chimbuko moja. Mfano Mifupa ya mikono na miguu ya paka inafanana na mifupa ya binadamu nk. Nk.Viumbe vingi kwenye kundi moja hufanana sana maumbo, Hivyo viumbe vingi huonesha kuwa vilitokana na wazazi walewale/Chimbuko moja.
ii. Genetics.;
Mendel (Mwaka 1865) aligundua kuwa viumbe vinarithishana sifa kwa njia ya kuzaa kupitia vinasaba (DNA). Kwa kutumia sayansi ya kisasa kuziangalia hizi DNA wanasayansi wamegundua kuwa Hivi vinasaba vya viumbe mbalimbali vinafanana. Viumbe wa kundi moja (mfano mamalia) huwa na vinasaba vinavyofanana sana kuliko wale wa makundi tofauti. Hivyo huonesha viumbe vina chimbuko moja.
iii. Fossils
Mabaki ya viumbe wa zamani yamekuwa yakipatikana chini ya dunia. Mabaki mengi yameonesha kuwa hapo kale kulikuwa na viumbe ambavyo leo havipo tena duniani na mabaki hayo pia yameonesha kwa kiwango kikubwa jinsi viumbe vya leo vina chimbuko moja. Mfano ugunduzi wa Alesi pale Kenya umeonesha kuwa Alesi alikuwa ni kiumbe mwenye sifa za binadamu na nyani, hivyo alikuwa ni babu yetu sisi binadamu na nyani.
iv. Embryology
Hapa tunaangalia viumbe vikiwa ndani ya tumbo/Yai kabla havijazaliwa..Viumbe vingi katika ngazi za mwanzoni huwa vinafanana, mfano mimba ya mwezi mmoja ya binadamu, kile kijusi kinafanana na kijusi cha nyani,mbwa,papa,Ng’ombe nk. Ni katika ngazi za mbele za ukuaji ndipo vijusi huanza kutofautiana Hivyo inaonesha kuwa viumbe vyote vina chimbuko moja.

NB: Evolution imaonesha kuwa viumbe vyote duniani vina chimbuko moja, Yule kiumbe wa kwanza alitokanaje hilo ni swali na mada nyingine ambayo ni ya siku nyingine.

While Evolution haisapoti lakini pia haipingi uwepo wa Mungu (Unaweza kuamini kuwa Mungu aliumba kiumbe wa Kwanza ambaye aliendelea kuevolve na kuleta viumbe wote duniani)

Screenshot 2022-05-19 140636.png


58470467_C0025531_Human_baby_with_a_tail_SPL_xlarge.jpeg
 
Sasa kama hiyo evolution ina Ushahidi lukuki Kwanini bado inaitwa Theory of evolution?

Itambulike kuwa wanasayansi wanaposema ‘theory’ haimaanishi ni kitu kisicho na Ushahidi. Theory inaweza kuwa ya ukweli, mfano uwepo wa atom ni fact lakini maelezo ya atom ipoje ni theory (atomic theory) ambapo wanafizikia wote wanajua kuwa atomic theory ni ukweli mtupu.

Tukienda google maana ya Theory inasema: dhana au mfumo wa mawazo unaokusudiwa kueleza jambo fulani, hasa kwa kuzingatia kanuni za jumla zisizotegemea jambo litakaloelezwa.

Mfano watu wote sasa tunajua kuwa dunia inalizunguka jua lakini hakuna mtu aliyesimama umbali wa kuishuhudia dunia ikilizunguka jua. Hivyo maelezo ya jinsi dunia inazunguka jua ni theory ambayo ushahidi wake ni uwepo wa Seasons/Majira, Nyota tofauti kuonekana kwa majira tofauti.

Kwahiyo sio kila theory haina ushahidi na sio kwamba theory ikipata ushahidi inaacha kuitwa theory.

Evolution ni theory lakini ni UKWELI
 
Kujibu swali moja common kuhusu evolution kabla halijaja ‘’Kama tumetokana na nyani, kwanini nyani wa leo hawageuki kuwa watu?’’
1. Hakuna mtu aliyesema tumetokana na nyani, lakini ni kuwa Nyani na sisi binadamu tumetokana na kiumbe kimoja (Babu yetu). Hivyo wajukuu wa hiko kiumbe wengine tumekuwa binadamu wengine wamekuwa nyani na miaka ijayo huenda binadamu tukabadilika kuwa kitu kingine na nyani wakawa kitu kingine (Evolution haina direction/goal) kwamba lazima nyani wawe watu. (Inawezekana baada ya miaka laki 2 ijayo nyani wakawa na mapezi kwakuwa dunia ilijaa maji ikabidi wajifunze kuogelea).

2. Evolution ni very slow process na inachukua miaka hata 50,000 mpaka mamilioni, kwahiyo kwa muda tuliokuwepo duniani mabadiliko kwa viumbe hutokea lakini katika nyanja ndogo sana (Mfano bacteria/virusi hubadilika kuzipinga dawa..ndiyomaana dawa nyingi hubadilika na muda). Hivyo ni ngumu kwa miaka 1000-6000 kuona nyani anabadilika kuwa mtu

Maisha yanabadilika sana, binadamu aliyeishi duniani miaka 2000 iliyopita sio sawa na binadamu wa leo. Leo binadamu anakula chakula kingi kwa wastani, anamulikwa na mwanga mwingi machoni (TV, Simu)..Kwahiyo binadamu anaweza kukua kiumbo kutokana na chakula(Binadamu wa siku hizi ni wakubwa kidogo tofauti na miaka ya 1700 kurudi nyuma) na pia anaweza kubadilika macho (Macho ya bluu kwa wazungu ni kitu cha hivi karibuni).
 
Evolution ni theory lakini ni UKWELI MTUPU.

Ahsante sana kwa Elimu hii. Nimeongeza kitu!
 
Ukweli au Nadharia inategemea unatazamaje swala hilo.

Kwanza kaisa unatakiwa uelewe kwamba wanadamu wanabadalika na viumbe vinabadilika.Hta viumbe vya aina moja vina utofauti na mfanano wa kiwango fulani.Katika hali kama hio huwezi kukataa uwezekano wa kuwa na uzao mmoja au chanzo kimoja ambacho kinabadilika kutokana na mazingira na hali tofauti.

Pili unapaswa uelewe kwamba ukweli juu ya evolution una mambo mengi sana ambayo kwa kiasi kikubwa yana ukweli kiasi fulani.Hata hivyo kuna baadhi ya mambo ambayo kwa kiasi ni ngumu ya kuyaelewa kulingana na kiwango cha taarifa na maarifa uliyonayo.Kwa mfano wengi husema kwamba iwapo mwanadamu aliwahi kuwa kama nyani ni kwa nini bado nyani wapo?Swali kama hilo ni swali dogo na jibu lake ni kwamba.Wanadamu ni baadhi ya nyani ambao kulingana na mazingita waliyokuwa walijikuta wakibadilika ili kuendana na mazingira na changamoto.SO UKWELI au NADHARIA katika Evolution unategemea unachagua kulitazamaje swala hilo.
 
i. Variation: Viumbe havifanani, kutokana na randomness/unasibu wa uzazi (Watoto hawafanani 100% na wazazi) na pia kuna mutation (Mabadiliko katika gene za viumbe) husababisha viumbe wa aina moja wasifanane. Mfano unaweza kufuga kuku wekundu tu bandani lakini baada ya vizazi kadhaa unaweza kuona kuku wanazaliwa wenye rangi tofauti.
ii. Natural selection/Uteuzi wa asili : Mazingira husababisha viumbe wenye sifa nzuri kuishi na wale wenye sifa mbaya hupotea.
Pamoja na kuwa naikubali evolution na mchango mkubwa wa natural selection na variation, kuna kitu naona hakipewi airtime Ila nacho kingetusaidia sana.

Kuna huyu mwamba Jean Baptiste Lamark's na nadharia yake ya ya evolution. Naipenda kwa sababu inaonesha viumbe nao wana mchango katika mabadiliko yao. Matakwa ya viumbe hayajaachwa hatutegemei randomness tu. Kwamba epigenetic changes inaongoza genetic changes pia. Sikatai accidental random genetic changes kutokea. La. Ila natetea kuwa mchango wa 'uamuzi' wa wanyama wenyewe upo na haujawakilishwa ipasavyo katika elimu.

Hivi kweli, are we not responsible whatsoever with anything that becomes of us, kweli!? Kwamba ni mazingira tuu, na forces na bahati? Aaah hapana.
 

Origin of life on earth (Mwanzo wa maisha hapa duniani)



Unaweza kufanya reference kupitia hiyo post nlitoa siku za nyuma ukaongeza maarifa zaidi
 
Both evolution na creation za religious ni uongo mkubwa.

Kisayansi haiwezekani uumbaji wa watu wawili waje wazae races na rangi tofaut tofauti bila ya kuwa na muingiliano wa mbegu ya utofauti ili kuja kuleta kiumbe cha race/rangi ya tofauti na hawa waliopo.

Sijui kwanni ktk sayansi na dini watu huogopa kuhoji haya maswali.

Eti mtu wa mwanzo alikuwa nyani and then why not now hao nyani hawabadiriki?

Kama huyo eva na adam walikuwa wazungu je hawa races zingine za waafrika/indians, chinese, walitokea vipi? Hakuna muujiza wa mtu kuzaliwa na race tofaut na ya mzazi wake pasipokuwa na muunganiko wa races mbili tofaut ili kuleta huo uchotara.

Upuuzi mwingine ni kuforce tuamni races za watu weupe zilitokea baada ya watu weusi kwenda maeneo ya baridi na kupelekea ngozi zao kubadirika na kuwa weupe, je wale watumwa wa kiafrika waliochukuliwa mateka miaka400 iliyopita kwanini hawajabadirika mpka leo wapo vile vile weusi?

Sayansi na Dini hizi zote ni takataka na propaganda zilizotungwa na wahuni ili kufichwa ukweli wa asili ya maisha ya dunia na kweli hii huwezi ipata kwa kusoma hizo takataka za vitabu vya dini ama vitabu vya kisayansi vilivyobase kwenye nadharia za wahuni wa Propaganda za Evolution..
 
Sasa kama hiyo evolution ina Ushahidi lukuki Kwanini bado inaitwa Theory of evolution?

Itambulike kuwa wanasayansi wanaposema ‘theory’ haimaanishi ni kitu kisicho na Ushahidi. Theory inaweza kuwa ya ukweli, mfano uwepo wa atom ni fact lakini maelezo ya atom ipoje ni theory (atomic theory) ambapo wanafizikia wote wanajua kuwa atomic theory ni ukweli mtupu.

Tukienda google maana ya Theory inasema: dhana au mfumo wa mawazo unaokusudiwa kueleza jambo fulani, hasa kwa kuzingatia kanuni za jumla zisizotegemea jambo litakaloelezwa.

Mfano watu wote sasa tunajua kuwa dunia inalizunguka jua lakini hakuna mtu aliyesimama umbali wa kuishuhudia dunia ikilizunguka jua. Hivyo maelezo ya jinsi dunia inazunguka jua ni theory ambayo ushahidi wake ni uwepo wa Seasons/Majira, Nyota tofauti kuonekana kwa majira tofauti.

Kwahiyo sio kila theory haina ushahidi na sio kwamba theory ikipata ushahidi inaacha kuitwa theory.

Evolution ni theory lakini ni UKWELI
. Dumas the terrible vipi hapo Annuanak hapo wapo wapi???
 
Pamoja na kuwa naikubali evolution na mchango mkubwa wa natural selection na variation, kuna kitu naona hakipewi airtime Ila nacho kingetusaidia sana.

Kuna huyu mwamba Jean Baptiste Lamark's na nadharia yake ya ya evolution. Naipenda kwa sababu inaonesha viumbe nao wana mchango katika mabadiliko yao. Matakwa ya viumbe hayajaachwa hatutegemei randomness tu. Kwamba epigenetic changes inaongoza genetic changes pia. Sikatai accidental random genetic changes kutokea. La. Ila natetea kuwa mchango wa 'uamuzi' wa wanyama wenyewe upo na haujawakilishwa ipasavyo katika elimu.

Hivi kweli, are we not responsible whatsoever with anything that becomes of us, kweli!? Kwamba ni mazingira tuu, na forces na bahati? Aaah hapana.
Yes nakubali kuwa kuna mchango wa individuals katika evolution
Mfano: Roughly miaka milioni 1.8 iliyopita inaaminika ndiyo moto uligundulika, hii ilisababisha homo erectus kuanza kuutumia kwa ajili ya kupika (behaviour) kwasababu ubongo unahitaji calories nyingi sana ili kuoperate (Ubongo una uzito wa 2% tu ya mwili lakini unatumia 20% ya chakula unachokula) Na chakula kilichopikwa huwa kina calories nyingi sana kuliko raw food, hii ilipelekea Homo erectus waweze kumaintain/Kusustain/Kuulisha ubongo mkubwa, Hivyo wale individuals wenye ubongo mkubwa waliweza kusurvive na wakaweza kupass zile traits kwa watoto wao, Hence Homo erectus wakakuza ubongo wao almost mara mbili ya size..Hii ikapelekea sehemu kama Neurocortex kudevelop na kuform complex structures leading to complex behaviours..Na hii ndo ikawa njia ya evolution kutuleta sisi binadamu.
Hivyo hapo kuna mchango mkubwa wa behaviour ambayo ni Diet
Lakini bado ni ngumu ku'argue kuwa hizi day to day behaviours zinaweza kuleta mabadiliko ambayo yanaweza kuwa inherited, na ndiyo maana Lamarck alipingwa..
However hii mada bado mbichi maana modern scientists bado wanafuatilia uwezekano wa non-DNA inheritence na epigenetics Lakini unfortunately hatuna Data za kutosha kusema ni ukweli au ni uongo..Hivyo this is an ongoing study
 
Both evolution na creation za religious ni uongo mkubwa.

Kisayansi haiwezekani uumbaji wa watu wawili waje wazae races na rangi tofaut tofauti bila ya kuwa na muingiliano wa mbegu ya utofauti ili kuja kuleta kiumbe cha race/rangi ya tofauti na hawa waliopo.

Sijui kwanni ktk sayansi na dini watu huogopa kuhoji haya maswali.

Eti mtu wa mwanzo alikuwa nyani and then why not now hao nyani hawabadiriki?

Kama huyo eva na adam walikuwa wazungu je hawa races zingine za waafrika/indians, chinese, walitokea vipi? Hakuna muujiza wa mtu kuzaliwa na race tofaut na ya mzazi wake pasipokuwa na muunganiko wa races mbili tofaut ili kuleta huo uchotara.

Upuuzi mwingine ni kuforce tuamni races za watu weupe zilitokea baada ya watu weusi kwenda maeneo ya baridi na kupelekea ngozi zao kubadirika na kuwa weupe, je wale watumwa wa kiafrika waliochukuliwa mateka miaka400 iliyopita kwanini hawajabadirika mpka leo wapo vile vile weusi?

Sayansi na Dini hizi zote ni takataka na propaganda zilizotungwa na wahuni ili kufichwa ukweli wa asili ya maisha ya dunia na kweli hii huwezi ipata kwa kusoma hizo takataka za vitabu vya dini ama vitabu vya kisayansi vilivyobase kwenye nadharia za wahuni wa Propaganda za Evolution..
Umesoma yote?? Maswali yako mengi yameshajibiwa huko juu

Eti mtu wa mwanzo alikuwa nyani and then why not now hao nyani hawabadiriki?
Kujibu swali moja common kuhusu evolution kabla halijaja ‘’Kama tumetokana na nyani, kwanini nyani wa leo hawageuki kuwa watu?’’
1. Hakuna mtu aliyesema tumetokana na nyani, lakini ni kuwa Nyani na sisi binadamu tumetokana na kiumbe kimoja (Babu yetu). Hivyo wajukuu wa hiko kiumbe wengine tumekuwa binadamu wengine wamekuwa nyani na miaka ijayo huenda binadamu tukabadilika kuwa kitu kingine na nyani wakawa kitu kingine (Evolution haina direction/goal) kwamba lazima nyani wawe watu. (Inawezekana baada ya miaka laki 2 ijayo nyani wakawa na mapezi kwakuwa dunia ilijaa maji ikabidi wajifunze kuogelea).

2. Evolution ni very slow process na inachukua miaka hata 50,000 mpaka mamilioni, kwahiyo kwa muda tuliokuwepo duniani mabadiliko kwa viumbe hutokea lakini katika nyanja ndogo sana (Mfano bacteria/virusi hubadilika kuzipinga dawa..ndiyomaana dawa nyingi hubadilika na muda). Hivyo ni ngumu kwa miaka 1000-6000 kuona nyani anabadilika kuwa mtu

Maisha yanabadilika sana, binadamu aliyeishi duniani miaka 2000 iliyopita sio sawa na binadamu wa leo. Leo binadamu anakula chakula kingi kwa wastani, anamulikwa na mwanga mwingi machoni (TV, Simu)..Kwahiyo binadamu anaweza kukua kiumbo kutokana na chakula(Binadamu wa siku hizi ni wakubwa kidogo tofauti na miaka ya 1700 kurudi nyuma) na pia anaweza kubadilika macho (Macho ya bluu kwa wazungu ni kitu cha hivi karibuni).
 
Back
Top Bottom