Je, gari yenye engine capacity chini ya cc 1000 inafaa kwa safari ndefu?

Toyota cami cc650 inafika Mbeya bila shida from Dar
Kwa hiyo hata hizo cc990 zinaweza kutoboa vizri tu hakikisha gari imefanyiwa service kabla ya safari

Sent from my phone using JamiiForums mobile app
 
[emoji3] hapo kweli ushuru wa ma SUV ni noma, ndio maana watu tunajificha kwenye hivi vitoto vya gari[emoji1787]
 
Sawa, hapo umemaliza vyema kabisa[emoji1545]
 
Okey
 
[emoji3] hapo kweli ushuru wa ma SUV ni noma, ndio maana watu tunajificha kwenye hivi vitoto vya gari[emoji1787]
Mi naona ni heri kudunduliza miaka 4 upate hela ya kununua gari ya maana SUV kuliko mtu anapata let say 10_12 mil anakimbilia gari ndogo Tena la cc chini ya 1400 Kama ist, passo, vits, Bora hata Toyota succeed kuliko vits au ist. Kuna SUV Kama Subaru Forester, Nissan extrial ukiwa na 14 mil unapata gari toka Japan, mpaka unakabidhiwa mkononi kwa hyo 13_14 mil.
 
Mkuu kuna watu wananunua IST new model kwa more than 20M. Hizi babywalker zina raha yake, hasa hapa town, halafu utumiaji wa mafuta ndio factor kubwa sana, kwa mishe za Dar ukiweka mafuta ya 50k unatumia wiki nzima, kwa hizi gari ndogo.

Hata kama unauweza kuwa na SUV hizi ndogo nazo sio za kuzikosa. Sina msaada sana.
 
Safari za mbali unatoboa vizuri sana tu ili mradi unacheza na temp ya gari tu, mimi nilikuwa natoka Dar naenda mpaka Tanga mpakani Horiri naacha mzigo na nachukua mzigo naenda mpaka Namanga naacha mzigo napumzika Arusha mjini asubuhi nageuka Dar, na nilikuwa natumia Toyota Duet piston 3 ya cc 980 tu na sio mara moja
 
Sijajua mnabishana nn wakati kila siku zinashuka Mitsubishi pajero mini 650cc, terios kid 660cc, daihatsu Mira 660cc, Suzuki kei 660cc etc na zinapelekwa Malawi, Rwanda, Burundi, Zambia na hata Congo na wanaotembea huko barabarani mnajua madereva wa it wanavyotembea, mtu umemuahidi peleka rudia jingine alafu aweke kituo ili akose kazi, tena na abiria wanabeba ingawa tunawakataza, kiufupi hizo gari zinafika popote sema zinapoenda kwa speed kubwa hutumia mafuta mengi
 
Sema mkuu kiukweli ulikuwa unachoka sana
 
Mkuu umejibu kiweredi kabisa. Maana una ushuhuda juu. Asante sana
 
Umesema kweli, japo kwa uzoefu wangu wa kusafiri na hiz IT madereva huwa wanatembea taratibu mno. Kwanza kuhofia tochi, pili kutumia mafuta mengi. So jamaa huwa hawana haraka,

lakini pia kuna kwenye check points huwa wanatumia muda mwingi, ni kama wanapumzika tu, mfano wa check point ya misugusugu na iringa, wanakaa sana pale.
 
[emoji3] hapo kweli ushuru wa ma SUV ni noma, ndio maana watu tunajificha kwenye hivi vitoto vya gari[emoji1787]
SUV ni muundo wa gari tu kwa maana ya ground clearance. Mana naona ww unachanganya mambo, zipo Suv ambazo zina cc sawa na hizo ist, porte, vitz na n.k
 
Huwa nasafiri na IST Dar to Moshi, kituo kimoja tu Korogwe. Naondoka na level seat na mizigo zaidi ya 100kg natembea spidi hadi 140 sehemu nayoona mbele vizuri. Gari inatembea haswa haichemshi na siizimi mpk natia timu moshi milimani.

Sema wakati wa kurudi narudi na watu wawili tu na mizigo michache gari inatembea vizuri mno inakuwa na mbio zaidi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…