econonist
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 20,189
- 29,663
Wanajamii kwa jinsi mambo yanavyoenda napata wasiwasi inaweza kuwa Hamas na Hizbullah waliingizwa kingi na Mossad kufanya mashambulizi ya October 7 na 8 2023.
Kwanini nasema hivi:
Inawezekaa pandikizi wa Mossad ndani ya Hamas walipanga hili Jambo. Wakawaset Hamas kupanga Hilo shambulio ili Israel ipate uhalali wa kuishambulia Gaza. Pia inawezekana Pandikizi la Mossad lilihusika kupanga mashambulizi ya Hizbullah kaskazini mwa Israel ili kupata uhalali wa kuishambulia Hizbullah. Yani pandikizi liliwapa wazi na mbinu ya kuishambulia Israel nao wakajaa.
Nasema hivi kwa sababu zifuatazo:
1. Kwanza, Israel ilipoanza mashambulizi dhidi ya Hamas na Hizbillah ni kama walikuwa na taarifa zote za wapi pa kushambulia. Hvyo kuwepo kwa taarifa hizi ni kama Israel alikuwa amejipanga mapema. Alijua jengo gani la kulipia na lipo sio la kulipia. Mpaka pagers za Hizbullah alizochakachua. Hivyo Israel aliwasoma Hamas na Hizbullah ndipo alawaingiza mkenge nao wakaingia mazima.
2. Pili, Israel imeua Viongozi wa juu wengi wa Hamas Hadi Yahaya Sinwar aliyeonekana ni invisible. Je ilikuwaje ghafla Israel wawalenge Viongozi wa Hamas na Kwa kujua maeneo walipo?. Sio kwamba walipanga Toka zamani wakawa wanasubiria Hamas aingie kingi. Israel alimfata Haniyeh kule kule Tehran Tena kwenye Kambi ya jeshi la Iran. Nadhani Israel alikuwa amepanga haya mambo mapema sana alisubiri uhalali wa kutekeleza.
3. Tatu, kwa Sasa Hamas na Hizbullah hawana nguvu Kama zamani. Israel imewabomoa Sana hasa Hamas. Hamas walichobakiza ni kushikilia mateka wa Israel kitu kinachoipa Israel nafasi ya kuendelea kukaa Gaza na kuchukua maeneo ya Gaza. Mtandao wa kifedha wa Hizbullah umeharibiwa, Miundo mbinu yao umeharibiwa na hata kiwanda chao kule Syria kimeharibiwa.
4. Nne, kuanguka kwa Assad. Je waasi waliandaliwa mapema wakisubiri Hizbullah aingie kingi kwa Israel ili adhoofishwe? Ili wao wapate nafasi ya kumpindua Assad?. Haingii akilini Hizbullah alipoingia kwenye ceasefire ndipo waasi wakaanza kazi.
Kwa Sasa Israel anaweza kumpiga Hizbollah bila kizuizi maana hawezi kupokea silaha kutoka Iran kupitia Syria na pia anajiongezea eneo Syria.
5. Tano, Israel imeua karibia Viongozi wote wa juu wa Hizbullah kuliko wakati wowote ule. Tena wakiwa ndani ya Beirut. Zamani Israel ilishambulia Sana Lebanon lakini haikuweza kugusa Viongozi wake kama Sasa hivi. Nani alijua kwamba Nasrallah atakufa? Alikuwa kiongozi invisible.
Mimi naamini kwa Asilimia kubwa Israel alimuungiza kingi Hamas na Hizbullah wawashambilie ili watekeleze mipango yao.
Kwanini nasema hivi:
Inawezekaa pandikizi wa Mossad ndani ya Hamas walipanga hili Jambo. Wakawaset Hamas kupanga Hilo shambulio ili Israel ipate uhalali wa kuishambulia Gaza. Pia inawezekana Pandikizi la Mossad lilihusika kupanga mashambulizi ya Hizbullah kaskazini mwa Israel ili kupata uhalali wa kuishambulia Hizbullah. Yani pandikizi liliwapa wazi na mbinu ya kuishambulia Israel nao wakajaa.
Nasema hivi kwa sababu zifuatazo:
1. Kwanza, Israel ilipoanza mashambulizi dhidi ya Hamas na Hizbillah ni kama walikuwa na taarifa zote za wapi pa kushambulia. Hvyo kuwepo kwa taarifa hizi ni kama Israel alikuwa amejipanga mapema. Alijua jengo gani la kulipia na lipo sio la kulipia. Mpaka pagers za Hizbullah alizochakachua. Hivyo Israel aliwasoma Hamas na Hizbullah ndipo alawaingiza mkenge nao wakaingia mazima.
2. Pili, Israel imeua Viongozi wa juu wengi wa Hamas Hadi Yahaya Sinwar aliyeonekana ni invisible. Je ilikuwaje ghafla Israel wawalenge Viongozi wa Hamas na Kwa kujua maeneo walipo?. Sio kwamba walipanga Toka zamani wakawa wanasubiria Hamas aingie kingi. Israel alimfata Haniyeh kule kule Tehran Tena kwenye Kambi ya jeshi la Iran. Nadhani Israel alikuwa amepanga haya mambo mapema sana alisubiri uhalali wa kutekeleza.
3. Tatu, kwa Sasa Hamas na Hizbullah hawana nguvu Kama zamani. Israel imewabomoa Sana hasa Hamas. Hamas walichobakiza ni kushikilia mateka wa Israel kitu kinachoipa Israel nafasi ya kuendelea kukaa Gaza na kuchukua maeneo ya Gaza. Mtandao wa kifedha wa Hizbullah umeharibiwa, Miundo mbinu yao umeharibiwa na hata kiwanda chao kule Syria kimeharibiwa.
4. Nne, kuanguka kwa Assad. Je waasi waliandaliwa mapema wakisubiri Hizbullah aingie kingi kwa Israel ili adhoofishwe? Ili wao wapate nafasi ya kumpindua Assad?. Haingii akilini Hizbullah alipoingia kwenye ceasefire ndipo waasi wakaanza kazi.
Kwa Sasa Israel anaweza kumpiga Hizbollah bila kizuizi maana hawezi kupokea silaha kutoka Iran kupitia Syria na pia anajiongezea eneo Syria.
5. Tano, Israel imeua karibia Viongozi wote wa juu wa Hizbullah kuliko wakati wowote ule. Tena wakiwa ndani ya Beirut. Zamani Israel ilishambulia Sana Lebanon lakini haikuweza kugusa Viongozi wake kama Sasa hivi. Nani alijua kwamba Nasrallah atakufa? Alikuwa kiongozi invisible.
Mimi naamini kwa Asilimia kubwa Israel alimuungiza kingi Hamas na Hizbullah wawashambilie ili watekeleze mipango yao.