Je, herbal clinics zina ufanisi?

Je, herbal clinics zina ufanisi?

Kimbori

JF-Expert Member
Joined
Feb 21, 2012
Posts
6,112
Reaction score
4,540
Itifaki ikiwa imezingatiwa.

Kumekuwa na ongezeko kubwa la verbal clinics mijini, herbal clinics hizo zinanadiwa sana kuwa zina uwezo wa kutibu magonjwa lukuki. Je zina ufanisi? Changia uzoefu wako.
 
Nilijaribu herbal moja wanaita Eternal...nilitoa hela nyingi na sikupata nafuu yyt.
 
MATAPELI WALE!

Walinipiga 250k na sikupona.
nimekuja pona kwa 52k hospital
 
Kumbe ndio maana wanatumia nguvu kubwa kujinadi. Dah!
 
Niliwahi kutibiwa Kwa mjinga alikuwa anajiita Dr mwaka wakati sijamjua Hadi Huwa natamani nimtandike ngumi.

Mpuuzi sana huyo mtu na serikali nayo alikuwa inamwangalia tu anajitangaza kuwaaminisha watu.baada ya takataka zake kutokuniponesha nilitaka nionane Naye ana Kwa ana ili anieleze hizo takataka zake kama zinatibu kweli,lakini Kila ukienda unadanganywa na wasaidizi wake ameenda japani mara china ili tu uondoke.

Mwisho wa siku nikaachana Naye tu nikaenda mhimbili nikapona.

Na nilipojihakikishia kuwa huyo mwaka ni tapeli ni pale Dr hamisi kingwangala alipoteuliwa na magufuli kuwa waziri wa afya akafanya ziara ya kushtukiza Kwa kichaa(mganga wa jadi mwaka)kwenye ofizi zake za kutapeli pale ilala bungoni.na kukimbia kupitia dirishani na Toka hapo akaacha na huo uganga wake wa jadi.

Mjinga sana Huyu mtu kala Hela za watu Kwa kutapeli na kuharibu afya za watu Kwa kuwanyesha mitakataka ambayo haifuate taratibu za kiafya.
 
Niliwahi kutibiwa Kwa mjinga alikuwa anajiita Dr mwaka wakati sijamjua Hadi Huwa natamani nimtandike ngumi.mpuuzi sana huyo mtu na serikali nayo alikuwa inamwangalia tu anajitangaza kuwaaminisha watu.baada ya takataka zake kutokuniponesha nilitaka nionane Naye ana Kwa ana ili anieleze hizo takataka zake kama zinatibu kweli,lakini Kila ukienda unadanganywa na wasaidizi wake ameenda japani mara china ili tu uondoke.mwisho wa siku nikaachana Naye tu nikaenda mhimbili nikapona.Na nilipojihakikishia kuwa huyo mwaka ni tapeli ni pale Dr hamisi kingwangala alipoteuliwa na magufuli kuwa waziri wa afya akafanya ziara ya kushtukiza Kwa kichaa(mganga wa jadi mwaka)kwenye ofizi zake za kutapeli pale ilala bungoni.na kukimbia kupitia dirishani na Toka hapo akaacha na huo uganga wake wa jadi.Mjinga sana Huyu mtu.kala Hela za watu Kwa kutapeli na kuharibu afya za watu Kwa kuwanyesha mitakataka ambayo haifuate taratibu za kiafya.
Na sasa kuna akina Dr. Mwaka wengi wamesambaa mikoani, yaani wao wanatibu kila kitu. Nimwestuka ndio wazo la kupata shuhuda toka kwa wadau likanijia.
 
Swali lako liko too generously, ni sawa nakusema hospitali zinaufanisi? Ukweli ni kwamba inategemea zipo ambazo zinaufanisi wa Hali ya juu na nyingine wa kawaida inategemea na ugonjwa husika na taasisi yenyewe hasa.
 
Wizara ya afya imelala sana,Kuna madawa makali sana yanatolewa na haya ma-herbal clinic.
Ubaya wanasema wanatibu mpaka magonjwa makubwa kabisa,Tena wenye elimu hata ya Fundamental biology ya secondary nao wanadanganywa HIV,Sukari zinatibika .
 
Zamani dawa hizi za asili walikua wakongwe ndo wanazitoa tena Kwa tahadhari sana,sasa hivi katoto kadogo ambako hata kujua rangi halisi ya mti wa muarobaini hakajui eti nako kanatoa dawa na kusifia ni Tiba ya uhakika 100%
 
Tatizo la Dawa za Asili ni kutokuwa na Research. Watu wanauza Dawa kisa Waliambiwa Mti fulani huwa unatibu na Babu yake au Bibi huko Nyuma

Wakati wenzetu wakisema Dawa Fulani inatibu wanakuwa wamefanya. research kwa Watu hata 1000 ndio wanaileta sokoni
 
Tatizo la Dawa za Asili ni kutokuwa na Research. Watu wanauza Dawa kisa Waliambiwa Mti fulani huwa unatibu na Babu yake au Bibi huko Nyuma

Wakati wenzetu wakisema Dawa Fulani inatibu wanakuwa wamefanya. research kwa Watu hata 1000 ndio wanaileta sokoni
Hawa jamaa wanatumia Matatizo/Changamoto za kiafya kama Fursa kwao kujipatia Fedha/Kipato. Wanajua ni lazima watu huugua na huhangaika sana kupata matibabu. Wanachafanya ni kutumia vifungashio vizuri, kuandika majina ya dawa kwa mwandiko mzuri wa rangi za kompyuta na kuorodhesha magonjwa yanayotibika kwa dawa iliyomo ndani ya kifungashio(chupa ya plastik). Mtumiaji Ukifungua ndani utakuta ni unga /powder ya mimea iliyochanganywa e.g. mashonanguo + Mkunde pori+ Mbegu ya parachichi + maganda ya chungwa. Kwa kweli vitu hivyo ni dawa kweli lakini isingekuwa kwa bei ghali hivyo. Unalipia container, leaflet ya maelezo ya matumizi iliyobandikwa nje ya kopo na ndani tena utachangia mishahara ya Wahudumu, kodi ya pango n.k. Aidha maduka yao huwa ni mijini. Huku vijijini hutoyakuta kwani huku vijijini tunajichimbia mizizi wenyewe na kutafuna majani fresh sio hayo yaliyokaushwa fasta-fasta kuwahi soko.
Hii sio sawa.
 
Nenda na ugonjwa wowote hukosi dawa, na dawa moja inatibu magonjwa 50 kidogo, ukinunua usipo pona ukirudi una ambiwa uongeze dozi.
 
Nenda na ugonjwa wowote hukosi dawa, na dawa moja inatibu magonjwa 50 kidogo, ukinunua usipo pona ukirudi una ambiwa uongeze dozi.
Hawana maabara za Utambuzi wa Tatizo - wao wanasikiliza maelezo kutoka kwa mgonjwa. Hawajui kwamba wagonjwa wengine kujieleza ni changamoto mojawapo. Ila wanajua fika kwamba dawa wanazouza haziwezi kumdhuru mtumiaji.
 
Herbel clinics hazuna tofauti na wanao uza maji ya upako. Wote ni wa ganga njaa wasio na huruma kwa watu wenye matatizo. Kama unaumwa nenda hospital usiende herbel clinic wala kuombewa kwa wachungaji.

Ni kweli kuna dawa za asili ambazo zinatibu lakini ni mpaka kwa wale wazee wanazozijua au kama mtu alifundishwa na wazee. Na hawa watu hawajitangazi bali unaweza kuwapata kwa word of mouth... Kupitia mtu anaye jua.

Ukiona mtu yeyote anauza na anajitangaza kuuza dawa za asili huyo ni mpigaji.

Kitu kingine cha kujua ni kwamba usinywe mitishamba kiholela. Maana haijafanyiwa utafiti na mingi ina sumu iliyopitiliza. Unaweza kupona lakini mwisho wa siku ikakuletea madhara kama kuharibu figo.

Ndugu.. nenda hospital. Achna na matapeli.
 
Back
Top Bottom