Je, herbal clinics zina ufanisi?

Je, herbal clinics zina ufanisi?

Wizara ya afya imelala sana,Kuna madawa makali sana yanatolewa na haya ma-herbal clinic.
Ubaya wanasema wanatibu mpaka magonjwa makubwa kabisa,Tena wenye elimu hata ya Fundamental biology ya secondary nao wanadanganywa HIV,Sukari zinatibika .
Ahsanteni sana wote, na wengine karibuni.

Kuna dogo alihitimu sek. 2015, akapata ufaulu 0. Alikuwa na bidii kwa kazi za mikono na nidhamu kuu.

Kufikia 2017 mwishoni nikamkuta mkoa mwingine ananadi dawa za mitishamba kwenye noa.

Yeye ndio mtangazaji, na anatiririka balaa, yaani ukimsikiliza kwa sekunde chache unalipia dawa.

Amekusanya kijiji, na kinagombania dawa.

Walipohitimisha biashara kwa siku hiyo akanifuata, na kusimulia mafanikio yake:

Nyumba 3 zilizokamilika, usafiri wa kawaida wa kutembelea, viwanja kadhaa.

Waliofaulu na kundelea na shule ndio wapo Six au mwaka wa 2 kwa ngazi ya cheti. Dah!
 
Kwa uzoefu wa miaka 10 Sasa kwenye hii huduma,herbal clinic nyingi hazina ufanisi.
Suala la mitishamba linahitaji utafiti wa kutosha ili kubaini ufanisi wa dawa Fulani katika kutibu changamoto Fulani,ni asilimia ndogo Sana ya watu wenye weledi na uwezo huo.
Mitishamba huhitaji uangalifu Sana katika uvunaji wake na mpaka ukaushaji wake ili kuepusha ile ingredients ya asili iliyomo ndani yake kupotea( ambayo Ndiyo dawa),mfano ni lazima kufahamu kuwa ni wakati gani mmea uvunwe majani,magome au mizizi yake.Si kila wakati unaweza kuvuna dawa katika mmea.Mathalani huwezi kuvuna dawa kwenye mizizi wakati wa jua Kali( hii ni kanuni ya kawaida ya fotosinthesis).
Wauzaji wengi wa dawa hawaadai wenyewe kulingana na changamoto ya upatikanaji wa mimea tiba.Wengi huuziwa dawa zilizoandaliwa na wao kuzipaki katika vifungashio vyao hata bila kujiridhisha Kama dawa hizo zina ubora,ilimradi tu amekalilishwa kuwa mti huo unatibu gonjwa Fulani.Kwa hiyo wengi wanauza makapi na Wala siyo dawa.Lakini Kama utapata mtu mtaalam anayeweza kuandaa dawa kwa vigezo na ufanisi,ni kweli mitishamba inasaidie Sana magonjwa mengi na watu wanapona.Shida ni pale mtu Yuko Dar anauza dawa ya unga wakati hata siku akikutana na huo mmea njiani hawezi kuutambua.
 
Kwa uzoefu wa miaka 10 Sasa kwenye hii huduma,herbal clinic nyingi hazina ufanisi.
Suala la mitishamba linahitaji utafiti wa kutosha ili kubaini ufanisi wa dawa Fulani katika kutibu changamoto Fulani,ni asilimia ndogo Sana ya watu wenye weledi na uwezo huo.
Mitishamba huhitaji uangalifu Sana katika uvunaji wake na mpaka ukaushaji wake ili kuepusha ile ingredients ya asili iliyomo ndani yake kupotea( ambayo Ndiyo dawa),mfano ni lazima kufahamu kuwa ni wakati gani mmea uvunwe majani,magome au mizizi yake.Si kila wakati unaweza kuvuna dawa katika mmea.Mathalani huwezi kuvuna dawa kwenye mizizi wakati wa jua Kali( hii ni kanuni ya kawaida ya fotosinthesis).
Wauzaji wengi wa dawa hawaadai wenyewe kulingana na changamoto ya upatikanaji wa mimea tiba.Wengi huuziwa dawa zilizoandaliwa na wao kuzipaki katika vifungashio vyao hata bila kujiridhisha Kama dawa hizo zina ubora,ilimradi tu amekalilishwa kuwa mti huo unatibu gonjwa Fulani.Kwa hiyo wengi wanauza makapi na Wala siyo dawa.Lakini Kama utapata mtu mtaalam anayeweza kuandaa dawa kwa vigezo na ufanisi,ni kweli mitishamba inasaidie Sana magonjwa mengi na watu wanapona.Shida ni pale mtu Yuko Dar anauza dawa ya unga wakati hata siku akikutana na huo mmea njiani hawezi kuutambua.
Nashukuru nimepata ABC za mitishamba.

Naomba kama itakupendeza uandae somo fupi namna bora ya kuvuna, kuandaa na kuhifadhi mitishamba kwa ujumla.

Kuna miti naitumia kutibu kuku, nataka kuongza ufanisi. Hizi kemikali zitatuua
 
Back
Top Bottom