MwanaFalsafa1
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 5,565
- 843
Atinga na kisu bungeni
Selemani Mpochi
Askari polisi mwenye namba E 5420 Hassan Ngoma, ambaye yupo katika kikosi cha Polisi Bunge, jana alinusurika kuchomwa kisu na kijana mmoja ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja.
Kwa mujibu wa askari huyo, kijana huyo aliwasili eneo la nje la uzio wa Bunge ambako kuna lango kuu la kuingilia magari ya viongozi saa 6:00 mchana na kuanza kupiga kelele huku akionyesha nia ya kufanya fujo eneo hilo.
"Baada ya kuona kuwa kijana huyo ataondoa utulivu uliopo eneo hilo, niliamua kwenda kumtuliza, ndipo alipochomoa kisu na kutaka kunichoma, nilikwepa kwa kurudi nyuma, lakini kijana huyo alizidi kunifuata hadi nilipofika lango la kuingilia magari," alisema askari huyo.
Alisema muda wote kijana huyo alikuwa ameshika kisu mkononi akitaka kuchoma mtu yeyote aliyekuwa mbele yake.
Alisema mbele ya lango hilo kuu, kulikuwa na askari wengine.
Wakati mkasa huo ukitokea, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alikuwa anakaribia kujibu hoja mbalimbali za wabunge waliokuwa wamechangia hotuba ya bajeti ya ofisi yake kwa mwaka wa fedha 2009/10, huku mawaziri wa nchi wa ofisi hiyo, wakijibu baadhi ya hoja za wabunge.
Kwa kawaida, lango hilo hulindwa na askari wa Usalama wa Taifa, Polisi na askari wa kampuni binafsi, lakini wote walitawanyika baada ya kijana kuibuka akiwa katika hali hiyo.
Kijana huyo alifanikiwa kupita kwenye lango hilo na kuelekea kwenye viwanja vya Bunge ndipo askari polisi Ngoma alikwenda kuchukua bunduki aina ya Sub Machine Gun (SMG) na kumfuata kabla hajafika kwenye lango linalotumiwa na wabunge kuingia ndani ya ukumbi wa Bunge.
Kabla hajafika mbali, askari wa Usalama Barabarani ambaye huongoza msafara wa Waziri Mkuu, Ali Ayoub, alimfuata kijana huyo na kumtuliza ili arudi getini.
Baada ya kuona anafuatwa na askari mwenye bunduki, ghafla alimzunguka zunguka askari huyo kwa nia ya kumfanya awe ngao yake endapo polisi mwenye bunduki angemfyatulia risasi.
Mtafaruku huo uliendelea kwa muda wa dakika 10 lakini polisi walifanikiwa kumdhibiti na kumuweka chini ya ulinzi.
Aliondolewa eneo hilo na kuingizwa ndani ya gari la polisi na kumpeleka kituo kikuu cha polisi mkoani hapa.
NIPASHE
Najua kijana huyu hakupaswa kufanya alicho fanya. lakini kukaa na kufikiri nikawa naona je hizi ni dalili ndogo ndogo kuwa wananchi wa kawaida wameshaanza kuchoshwa na uongozi wetu? Kama mwananchi wa kawaida kajitolea muhanga kufanya kitu kama hicho kwenye jengo analo jua viongozi wapo na kutakuwa kuna lindwa sana ni anajaribu kupaza sauti yake ambayo viongozi wetu hawataki kusikia? Mh tusipo angalia tunaenda kubaya. Anaweza tu kuwa mhuni wa kawaida lakini pia anaweza kuwa kiashiria cha dalili ya watu kuchoka.
Selemani Mpochi
Askari polisi mwenye namba E 5420 Hassan Ngoma, ambaye yupo katika kikosi cha Polisi Bunge, jana alinusurika kuchomwa kisu na kijana mmoja ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja.
Kwa mujibu wa askari huyo, kijana huyo aliwasili eneo la nje la uzio wa Bunge ambako kuna lango kuu la kuingilia magari ya viongozi saa 6:00 mchana na kuanza kupiga kelele huku akionyesha nia ya kufanya fujo eneo hilo.
"Baada ya kuona kuwa kijana huyo ataondoa utulivu uliopo eneo hilo, niliamua kwenda kumtuliza, ndipo alipochomoa kisu na kutaka kunichoma, nilikwepa kwa kurudi nyuma, lakini kijana huyo alizidi kunifuata hadi nilipofika lango la kuingilia magari," alisema askari huyo.
Alisema muda wote kijana huyo alikuwa ameshika kisu mkononi akitaka kuchoma mtu yeyote aliyekuwa mbele yake.
Alisema mbele ya lango hilo kuu, kulikuwa na askari wengine.
Wakati mkasa huo ukitokea, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alikuwa anakaribia kujibu hoja mbalimbali za wabunge waliokuwa wamechangia hotuba ya bajeti ya ofisi yake kwa mwaka wa fedha 2009/10, huku mawaziri wa nchi wa ofisi hiyo, wakijibu baadhi ya hoja za wabunge.
Kwa kawaida, lango hilo hulindwa na askari wa Usalama wa Taifa, Polisi na askari wa kampuni binafsi, lakini wote walitawanyika baada ya kijana kuibuka akiwa katika hali hiyo.
Kijana huyo alifanikiwa kupita kwenye lango hilo na kuelekea kwenye viwanja vya Bunge ndipo askari polisi Ngoma alikwenda kuchukua bunduki aina ya Sub Machine Gun (SMG) na kumfuata kabla hajafika kwenye lango linalotumiwa na wabunge kuingia ndani ya ukumbi wa Bunge.
Kabla hajafika mbali, askari wa Usalama Barabarani ambaye huongoza msafara wa Waziri Mkuu, Ali Ayoub, alimfuata kijana huyo na kumtuliza ili arudi getini.
Baada ya kuona anafuatwa na askari mwenye bunduki, ghafla alimzunguka zunguka askari huyo kwa nia ya kumfanya awe ngao yake endapo polisi mwenye bunduki angemfyatulia risasi.
Mtafaruku huo uliendelea kwa muda wa dakika 10 lakini polisi walifanikiwa kumdhibiti na kumuweka chini ya ulinzi.
Aliondolewa eneo hilo na kuingizwa ndani ya gari la polisi na kumpeleka kituo kikuu cha polisi mkoani hapa.
NIPASHE
Najua kijana huyu hakupaswa kufanya alicho fanya. lakini kukaa na kufikiri nikawa naona je hizi ni dalili ndogo ndogo kuwa wananchi wa kawaida wameshaanza kuchoshwa na uongozi wetu? Kama mwananchi wa kawaida kajitolea muhanga kufanya kitu kama hicho kwenye jengo analo jua viongozi wapo na kutakuwa kuna lindwa sana ni anajaribu kupaza sauti yake ambayo viongozi wetu hawataki kusikia? Mh tusipo angalia tunaenda kubaya. Anaweza tu kuwa mhuni wa kawaida lakini pia anaweza kuwa kiashiria cha dalili ya watu kuchoka.