Je, hoja za Nyalandu zimejibiwa?

Je, hoja za Nyalandu zimejibiwa?

Elius W Ndabila

JF-Expert Member
Joined
Jul 17, 2019
Posts
324
Reaction score
649
JE, HOJA ZA MHE NYALANDU ZIMEJIBIWA?

Na Elius Ndabila
0768239284

Leo Mhe Nyalandu aliyewahi kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii amerudi CCM katika Mkutano mkuu maalum uliofanyika hapa Jakaya Kikwete Convention. Mhe Nyalandu anarudi CCM baada ya kujivua uwanachama wa CCM tarehe 30/10/2017.

Kama ilivyo kwa watu wengine wanapohama Chama kimoja kwenda kingine huwa wanakuwa na sababu lukuki zinazowafanya kuhama vyama vyao. Ndugai naye akiwa anaondoka na kujivua ukada wa CCM alielekeza shutuma kuwa Katiba ya nchi si rafiki. Alisema kuwa mihimili haijitegemei.

Maswali ya kujiuliza ni kuwa Mhe Nyalandu hoja zake alizokuwa akizisimamia zimefanyiwa kazi? Je, Nyalandu aliukimbia utawala wa hayati Magufuli au aliikimbia Katiba? Kama ni Katiba mbona bado ni ile ile aliyoikimbia? Je, Mhe Nyalandu anaamini katika utawala au katika Katiba?

Mhe Nyalandu, aliyewahi kuwa Waziri wa Mali Asili na Utalii wakati wa serikali ya awamu ya Tano wakati anatimukia CHADEMA alisema kupitia taarifa yake kwamba amejuzulu nyadhifa zake zote ndani ya chama cha mapinduzi CCM ikiwemo ubunge wake.

Nyalandu alisema amechukua uamuzi huo kutokana na kutokuridhishwa na mwendo wa siasa nchini Tanzania, ukiukwaji wa haki za kibinaadamu, ongezeko la vitendo vya kidhalimu dhidi ya raia na kutokuwepo kwa mipaka baina ya mihimili ya dola - Serikali, Bunge na Mahakama. Hizi zilikuwa ni tuhuma kubwa kutokea kutoka kwa mtu aliyekuwa ndani ya serikali ukimuondoa mzee Mrema.

Katika taarifa yake ya kujiuzulu aliyoiweka katika ukurasa wake wa Facebook ambayo hadi muda huu ninaandika hakuifuta, Nyalandu alisisitiza umuhimu wa nchi kupata katiba mpya.

Mhe Nyalandu alisema "Naamini kwamba bila Tanzania kupata Katiba Mpya Sasa, hakuna namna yeyote ya kuifanya mihimili ya dola isiingiliane na kuwepo kwa ukomo wa wazi na kujitegemea kwa dhahiri kwa mihimili ya Serikali,"

Kwa hoja hizi za kuondoka kwa Mhe Nyalandu na kurudi tena leo CCM ingali bado hoja yake ya Katiba mpya haipo, Basi inaonyesha namna Wanasiasa wengi tulivyo na ndimi mbili. Inaonyesha namna Wanasiasa tunavyotumia fursa za Siasa vibaya. Nyalandu sasa anaowajibu wa kuwaeleza Watanzania kuwa sababu iliyomkimbiza CCM haikuwa Katibu mpya kwa mwamvuri wa Mhimili kuto kuwa independent bali alikuwa na sababu nyingine.

Ni vema kama Taifa tukajenga siasa za ushindani bila uzushi na kutengenezeana ajali.
 
Nyalandu kama Mt zero walidhani wakienda Chadema watapata nafasi ya kugombania urais. Ni tabu sana kuona watu kama hawa wanaendeshwa na fursa

Anyways tusimlaumu sana, hawa ni wana siasa na kusema kweli nje ya ccm kwa sasa Tanzania hakuna mtu mwingine anafanya siasa. Wamepigwa pini maisha hayaendi, acha waende huko labda watapata nafasi ya kufanya siasa. Vyama vya upinzani kwa sasa ni kama vimekufa tu. Inatakiwa moyo wa kipekee kukomaa navyo. Ikiwa dhamira ni masalhi na ujiko huwezi dumu kwenye vyama vya upinzani sasa hivi.
 
Mi nanukuu tuuu kuna watu wanataka Uwaziri wa Maliasili na Utalii na Hakika wataupata tuu,Kuna watu wanataka kuwa Daraja fulani wengine wapite!hahaha hivi kumbe nilikuwa naota tena Ndoto ya Mchana?
 
JE, HOJA ZA MHE NYALANDU ZIMEJIBIWA?

Na Elius Ndabila
0768239284

Leo Mhe Nyalandu aliyewahi kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii amerudi CCM katika Mkutano mkuu maalum uliofanyika hapa Jakaya Kikwete Convention. Mhe Nyalandu anarudi CCM baada ya kujivua uwanachama wa CCM tarehe 30/10/2017.

Kama ilivyo kwa watu wengine wanapohama Chama kimoja kwenda kingine huwa wanakuwa na sababu lukuki zinazowafanya kuhama vyama vyao. Ndugai naye akiwa anaondoka na kujivua ukada wa CCM alielekeza shutuma kuwa Katiba ya nchi si rafiki. Alisema kuwa mihimili haijitegemei.

Maswali ya kujiuliza ni kuwa Mhe Nyalandu hoja zake alizokuwa akizisimamia zimefanyiwa kazi? Je, Nyalandu aliukimbia utawala wa hayati Magufuli au aliikimbia Katiba? Kama ni Katiba mbona bado ni ile ile aliyoikimbia? Je, Mhe Nyalandu anaamini katika utawala au katika Katiba?

Mhe Nyalandu, aliyewahi kuwa Waziri wa Mali Asili na Utalii wakati wa serikali ya awamu ya Tano wakati anatimukia CHADEMA alisema kupitia taarifa yake kwamba amejuzulu nyadhifa zake zote ndani ya chama cha mapinduzi CCM ikiwemo ubunge wake.

Nyalandu alisema amechukua uamuzi huo kutokana na kutokuridhishwa na mwendo wa siasa nchini Tanzania, ukiukwaji wa haki za kibinaadamu, ongezeko la vitendo vya kidhalimu dhidi ya raia na kutokuwepo kwa mipaka baina ya mihimili ya dola - Serikali, Bunge na Mahakama. Hizi zilikuwa ni tuhuma kubwa kutokea kutoka kwa mtu aliyekuwa ndani ya serikali ukimuondoa mzee Mrema.

Katika taarifa yake ya kujiuzulu aliyoiweka katika ukurasa wake wa Facebook ambayo hadi muda huu ninaandika hakuifuta, Nyalandu alisisitiza umuhimu wa nchi kupata katiba mpya.

Mhe Nyalandu alisema "Naamini kwamba bila Tanzania kupata Katiba Mpya Sasa, hakuna namna yeyote ya kuifanya mihimili ya dola isiingiliane na kuwepo kwa ukomo wa wazi na kujitegemea kwa dhahiri kwa mihimili ya Serikali,"

Kwa hoja hizi za kuondoka kwa Mhe Nyalandu na kurudi tena leo CCM ingali bado hoja yake ya Katiba mpya haipo, Basi inaonyesha namna Wanasiasa wengi tulivyo na ndimi mbili. Inaonyesha namna Wanasiasa tunavyotumia fursa za Siasa vibaya. Nyalandu sasa anaowajibu wa kuwaeleza Watanzania kuwa sababu iliyomkimbiza CCM haikuwa Katibu mpya kwa mwamvuri wa Mhimili kuto kuwa independent bali alikuwa na sababu nyingine.

Ni vema kama Taifa tukajenga siasa za ushindani bila uzushi na kutengenezeana ajali.
Ni nyumbu tu atakayebaki chadema
 
CHADEMA wajifunze kupapatikia makapi ya CCM, la sivyo kitakuwa kinapiga hatua kumi na kurudi hatua 15 halafu wanajipongeza....

CHADEMA inawanachama waaminifu wengi Sana wenye uwezo wa kujitolea kwa jasho na damu..lakini ajabu wanawaacha na kubabaika na watu waliozoea kula kuku kwa mrija toka CCM.
 
CHADEMA wajifunze kupapatikia makapi ya CCM, la sivyo kitakuwa kinapiga hatua kumi na kurudi hatua 15 halafu wanajipongeza....

CHADEMA inawanachama waaminifu wengi Sana wenye uwezo wa kujitolea kwa jasho na damu..lakini ajabu wanawaacha na kubabaika na watu waliozoea kula kuku kwa mrija toka CCM.
CHADEMA kama chama hakipaswi kukataa wanachama kutoka vyama vingine lakini hakipaswi kuwaamini na kuwapa uongozi mpaka kwenye nafasi nyeti za kitaifa.
 
Haya mambo yangetokea wakati Magu akiwa hai (akiwa kamaliza muda wake wa Rais,akamwachia mwingine,,naamini asingekuwa mwanamama)... Nadhani Familia ya JPM inateseka kwa yanayotokea
 
JE, HOJA ZA MHE NYALANDU ZIMEJIBIWA?

Na Elius Ndabila
0768239284

Leo Mhe Nyalandu aliyewahi kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii amerudi CCM katika Mkutano mkuu maalum uliofanyika hapa Jakaya Kikwete Convention. Mhe Nyalandu anarudi CCM baada ya kujivua uwanachama wa CCM tarehe 30/10/2017.

Kama ilivyo kwa watu wengine wanapohama Chama kimoja kwenda kingine huwa wanakuwa na sababu lukuki zinazowafanya kuhama vyama vyao. Ndugai naye akiwa anaondoka na kujivua ukada wa CCM alielekeza shutuma kuwa Katiba ya nchi si rafiki. Alisema kuwa mihimili haijitegemei.

Maswali ya kujiuliza ni kuwa Mhe Nyalandu hoja zake alizokuwa akizisimamia zimefanyiwa kazi? Je, Nyalandu aliukimbia utawala wa hayati Magufuli au aliikimbia Katiba? Kama ni Katiba mbona bado ni ile ile aliyoikimbia? Je, Mhe Nyalandu anaamini katika utawala au katika Katiba?

Mhe Nyalandu, aliyewahi kuwa Waziri wa Mali Asili na Utalii wakati wa serikali ya awamu ya Tano wakati anatimukia CHADEMA alisema kupitia taarifa yake kwamba amejuzulu nyadhifa zake zote ndani ya chama cha mapinduzi CCM ikiwemo ubunge wake.

Nyalandu alisema amechukua uamuzi huo kutokana na kutokuridhishwa na mwendo wa siasa nchini Tanzania, ukiukwaji wa haki za kibinaadamu, ongezeko la vitendo vya kidhalimu dhidi ya raia na kutokuwepo kwa mipaka baina ya mihimili ya dola - Serikali, Bunge na Mahakama. Hizi zilikuwa ni tuhuma kubwa kutokea kutoka kwa mtu aliyekuwa ndani ya serikali ukimuondoa mzee Mrema.

Katika taarifa yake ya kujiuzulu aliyoiweka katika ukurasa wake wa Facebook ambayo hadi muda huu ninaandika hakuifuta, Nyalandu alisisitiza umuhimu wa nchi kupata katiba mpya.

Mhe Nyalandu alisema "Naamini kwamba bila Tanzania kupata Katiba Mpya Sasa, hakuna namna yeyote ya kuifanya mihimili ya dola isiingiliane na kuwepo kwa ukomo wa wazi na kujitegemea kwa dhahiri kwa mihimili ya Serikali,"

Kwa hoja hizi za kuondoka kwa Mhe Nyalandu na kurudi tena leo CCM ingali bado hoja yake ya Katiba mpya haipo, Basi inaonyesha namna Wanasiasa wengi tulivyo na ndimi mbili. Inaonyesha namna Wanasiasa tunavyotumia fursa za Siasa vibaya. Nyalandu sasa anaowajibu wa kuwaeleza Watanzania kuwa sababu iliyomkimbiza CCM haikuwa Katibu mpya kwa mwamvuri wa Mhimili kuto kuwa independent bali alikuwa na sababu nyingine.

Ni vema kama Taifa tukajenga siasa za ushindani bila uzushi na kutengenezeana ajali.

Jibu kila mwenye akili anajua Hayati Magufuli 😂 unafikiri angeweza kurudi Magu aliwepo?
 
Sio kila kitu cha mwanasiasa ni cha kuamini
 
Nyalandu kama Mt zero walidhani wakienda Chadema watapata nafasi ya kugombania urais. Ni tabu sana kuona watu kama hawa wanaendeshwa na fursa

Anyways tusimlaumu sana, hawa ni wana siasa na kusema kweli nje ya ccm kwa sasa Tanzania hakuna mtu mwingine anafanya siasa. Wamepigwa pini maisha hayaendi, acha waende huko labda watapata nafasi ya kufanya siasa. Vyama vya upinzani kwa sasa ni kama vimekufa tu. Inatakiwa moyo wa kipekee kukomaa navyo. Ikiwa dhamira ni masalhi na ujiko huwezi dumu kwenye vyama vya upinzani sasa hivi.

Umesema vyema. Na ukweli hasa ni kuwa CCM si chama cha siasa kama ilivyo CHADEMA. Bali CCM ndiyo serikali yenyewe (JMT + SMZ). Ni taasisi ya dola iliyoundwa kuhodhi nyenzo zote za dola kwa manufaa ya magenge ya watawala. Huu ni ukweli unaofumbiwa macho na wengi.

Ni mazingira ya kipekee sana ambapo chama makini cha siasa (CHADEMA) kinapambana na dola huku wananchi wakiaminishwa kwamba ni mapambano baina ya vyama vinavyolingana.

Wanasiasa waelewa wenye matamanio ya ukuu na ukwasi hata siku moja hawawezi kufanya “ujinga” wa kung’ang’ania CHADEMA. Huko ni kujitoa mhanga. Lengo lao ni hatimaye kukubalika serikalini (CCM) ili watimize matamanio yao.

Wasioweza kwenda CCM moja kwa moja huanzia CHADEMA kupata “credentials” za umahiri wa kisiasa ili waonwe na wakuu wa dola/CCM kisha “kushawishiwa” kujiunga na taasisi hiyo.

Huwa haishangazi kuona wakulu wa CCM/dola wakifurahia sana kumpata “firebrand” toka CHADEMA. Ingawa sijui kama wanaelewa kwa nini CHADEMA huwa haiathiriki na wahamaji bali hao ndio hupoteza makali yao wakisha kuwa ndani ya CCM. Ni wazi kuwa huko mahali ni wrong place kwa siasa makini.
 
Wanasiasa watawa pasueni vichwa teh teh teh

Ova
 
Ni mada dhaifu aiseee!

Hujamuuliza Frederick wala Edward, ya nini umrukie Nyalandu?

Nyalandu anakitu gani tofauti na hao wengine, si wote wanatafuta fursa, kama unavyotafuta wewe hapa, maana umejitambulisha kuwa ni mwanasiasa.

Nyinyi nyote ni wanasiasa njaa, msiokuwa na msimamo wowote mnaouamini isipokuwa matumbo yenu basi.

Hata ni aibu kabisa kuwaita nyinyi kuwa ni wanasiasa.
 
Back
Top Bottom