matunduizi
JF-Expert Member
- Aug 20, 2018
- 7,968
- 19,368
Wakuu kwema?
Niwe mkweli, siku hizi kiwango cha uaminifu kimeongezeka sana hasa kwenye pesa. Sijajua sababu.
Unaweza kukutana na mtu hamjuani ukamuachia pesa nyingi bila maandishi na kazi akafanya tena kwa wakati.
Mifano
Kuna dogo nilimpa 4M simjui anifanyie kazi, bila maandishi, jamaa yangu ananiambia umepigwa, mimi namwambia hakuna nchi imebadilika. Yule dogo kakamilisha kaleta tena kwa wakati. Baadae ananionyesha anapewa kazi na kutumiwa cash mil 20, 5, 8, 3 na kazi zinafanyika bila shida.
Pia soma: Utajiri wako uko kwenye uaminifu, kujituma, na kuweka aibu pembeni
Kwenye bidhaa za kuagiza kwa usiowajua huko ndio raha sana. Jamaa wengi mitandaoni ni waaminifu sana. Nimenunua vitu vingi tena kwa kuletewa nilipo na kitu kinakuja kilekile.
Mfano mtu mmoja alituma bidhaa ambazo kama ningempotezea zingeoza, lakini alituma tena bila hata kumshawishi sana.
Kwa ufupi, kuna mabadiliko sana ya kiwango cha uaminifu katika jamii. Watu wengi wanatumia kama mtaji maana wanajua wakizingua watalala njaa.
Huwa naamini hadi mtu unatapeliwa, huwa kuna viashiria uliviona ukavipotezea. Ila ukiwa mzingativu matapeli ni wachache na ni rahisi kuwagundua ukiwa makini.
Unadhani kwa nini hali imekuwa hivyo?
Niwe mkweli, siku hizi kiwango cha uaminifu kimeongezeka sana hasa kwenye pesa. Sijajua sababu.
Unaweza kukutana na mtu hamjuani ukamuachia pesa nyingi bila maandishi na kazi akafanya tena kwa wakati.
Mifano
Kuna dogo nilimpa 4M simjui anifanyie kazi, bila maandishi, jamaa yangu ananiambia umepigwa, mimi namwambia hakuna nchi imebadilika. Yule dogo kakamilisha kaleta tena kwa wakati. Baadae ananionyesha anapewa kazi na kutumiwa cash mil 20, 5, 8, 3 na kazi zinafanyika bila shida.
Pia soma: Utajiri wako uko kwenye uaminifu, kujituma, na kuweka aibu pembeni
Kwenye bidhaa za kuagiza kwa usiowajua huko ndio raha sana. Jamaa wengi mitandaoni ni waaminifu sana. Nimenunua vitu vingi tena kwa kuletewa nilipo na kitu kinakuja kilekile.
Mfano mtu mmoja alituma bidhaa ambazo kama ningempotezea zingeoza, lakini alituma tena bila hata kumshawishi sana.
Kwa ufupi, kuna mabadiliko sana ya kiwango cha uaminifu katika jamii. Watu wengi wanatumia kama mtaji maana wanajua wakizingua watalala njaa.
Huwa naamini hadi mtu unatapeliwa, huwa kuna viashiria uliviona ukavipotezea. Ila ukiwa mzingativu matapeli ni wachache na ni rahisi kuwagundua ukiwa makini.
Unadhani kwa nini hali imekuwa hivyo?