Je, ilichukua muda gani kuanza kupata faida katika biashara yako?

OMOYOGWANE

JF-Expert Member
Joined
Dec 30, 2016
Posts
4,701
Reaction score
11,920
Habari wakuu!

Kuendesha biashara inahitaji akili nyingi sana, huu uzi ni maalum kwa watu ambao wamewahi kuanzisha biashara na zikafanikiwa.

Katika biashara kuna mtaji (Fungu la pesa la kueendeshea biashara), matumizi (kodi ya fremu, umeme, ulinzi, usafirishaji n.k) pia kuna faida (Mauzo - mtaji)

Je, ilikuchukua muda gani kuanza kupata faida ktk biashara yako?
Je, ulianzaje anzaje mpaka ukafikia hapo ulipo?
 
1. Miaka 2-3 ya mwanzo ni migumu mno. Bila roho ya paka, utaacha biashara,ila ukivumilia utaanza kuiona faida.

2. Lazima uchague kuwa mtu wa Mungu kweli au uwe mshirikina, bila hivyo hutoboi.

3. Lazima uwe na usimamizi Mzuri au ujenge strong team
4. Nidhamu ni muhimu sana.

Ukijitahidi kufuata hizo rules utatoboa.
 
Wewe ilikuchukua muda gani na ulikuwa unafanya biashara gani mkuu.
 
Sawa mkuu asante kwa ushauri.
 
Wewe ilikuchukua muda gani na ulikuwa unafanya biashara gani mkuu

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
Mimi nilichelewa kufanikiwa kibiashara sababu sikutaka kuwa mshirikina na wala sikutaka kuwa kwa Mungu, niliamini kwenye elimu yangu na mtaji. Baadae ndio nikaja kutonywa na watu.

Nimeanza ku-breakeven 2.5 years, ila miaka 3 ndio nilianza kupata faida.
 
Nakazia hiyo namba 2 mkuu
 
Mkuu unafanya Fx nn, naona mambo ya breakeven[emoji1][emoji1]
 
Nakazia hiyo namba 2 mkuu
Mimi sikupenda kuchagua upande wa ushirikina, nikaamua kujiunga na vikundi vya maombezi, huwezi amini niliingia kwa hasira sana,maana nilishapata hasara sana.

Nilifunga mfungo wa masaa 12 kwa siku 30, kuna siku wakati nipo kwenye mfungo,nikaota usiku ninapambana na jitu la miraba mi4, mimi naomba na yeye anaomba kwa ishara kwa kuninyooshea mikono, baadae nikalidondosha chini, nikashtuka ndotoni. After one week ,biashara zikaanza kunyooka. Hii dunia ni zaidi ujuavyo.

Ila ukitaka kufuata kanuni hii, uwe na uhakika hutafanya madhambi Mungu anayochukia, ukifanya tu unafirisika to zero. Trust me haswa uzinzi.
Walokole wengi ni maskini sababu kubwa wanataka kufanikiwa kibiashara kupitia Mungu lakini wanafanya dhambi nyingi sirini.
 
Asante kwa kunifungua macho

Sent from my Infinix X652 using JamiiForums mobile app
 
Miezi 5 hakuna faida,natunza pesa inarud tena kwenye marekebisho,sikuwa kwa mungu wala kwa washirikina,ila baba yangu alkuwa kwa washirikina,biashara ilisumbua,baadae nkafanya ukarabati wa kuweka mashine vizuri ,nkaamua kutafuta maji ya baraka,biashara inaenda poa mpaka sasa na kanisani huwa siendi
 
Mkuu kuna siku nilitaka kuleta thread hapa ya kutaka kufahamu hili swala

Hivi ni kwa nini asilimia kubwa ya watu wakishafungua biashara,kunakuwepo na dhana ya kutafuta Ushirikina????..

ni kujikinga dhidi ya maadui?

Au ili biashara istawi???

Nina imani wewe si mtaalamu,ila naomba unidokezee kdg unayofahamu kuhusu haya.

“Trust me haswa uzinzi”..Na jee vipi hapa mkuu hili suala huwa linamaliza vipi nguvu ya mtu?

Ahsante.
 
Mkuu hiyo line yake ata mm imenitafkarisha sana natamani aiweke vizuri kwa kuiongezea nyama
 
Mkuu hiyo line yake ata mm imenitafkarisha sana natamani aiweke vizuri kwa kuiongezea nyama
sanaa mkuu
haya maneno huwa nayasikia sana kuwa asilimia kubwa ya wafanyabiashara wanatumia nguvu za giza,wachache sana ni nyota zao + nguvu za Mungu.
 
Mathayo 4:8-9, shetani akamchukua Yesu Akamuonyesha milki zote za ulimwengu na fahari zake.
Maana yake:
1.Milki inamaana ardhi, madini, majumba etc
2.Fahari inamaana vyeo,heshima, etc.(ndio maana sikushangaa kumsikia mbunge Msukuma akitamka bungeni kwamba 99% walienda kwa waganga ili kuwa wabunge,sababu vyeo vinatolewa na shetani au Mungu.)
Lakini kwa condition moja tu Yesu amuangukie na kumsujudu.
Hapa biblia inatupa siri kumbe kuna vitu shetani anavimiliki hapa duniani na huwezi kuvipata mpaka u-mfanye Mungu wako(ndio maana ya kumuangukia na kimsujudia).
Kiufupi hapa duniani Sisi wanadamu tuna-lease tu hizi assets, lakini wenye assets ni Mungu na Shetani.mpaka ufuate masharti yao ndio wakupe.
Ngoja nikupe mfano mrahisi, wewe ni mfanyabiashara wa kilimo. Unaweza kuwa na mtaji,ujuzi na man power na kufanya kilimo, lakini ardhi ambayo ni msingi mkuu wa kufanya biashara yako inamilikiwa na serikali.kwahiyo inabidi uombe Kibali cha serikali ili ikukodishie ardhi na siku ukizinguana na serikali wanachukua ardhi yao na ndio kifirisika kwako
 
Mathayo 6:24
 
Ukitaka kufanikiwa kwa njia za ki-Mungu ufuate kanuni zifuatazo.
1. Uanze kuishi maisha ya kumpendeza Mungu, kwa nje na sirini
2. Kosea vyote ila usizini.ukikosea mengine ukaomba toba, Mungu atakusamehe na biashara itaendelea.
Ila ukizini lazima ufirisike kwanza, uaibike na ndio adhabu yako.

Ndio uje uanze mwanzo tena
3. Usiibe hela au kumdhulumu mtu Mali yake au kuiibia serikali then uje uanze biashara ukategemea Mungu ataibariki,NEVER

3.
 
Yote 9 hapa "Ila ukitaka kufuata kanuni hii, uwe na uhakika hutafanya madhambi Mungu anayochukia, ukifanya tu unafirisika to zero. Trust me haswa uzinzi." Panachangamoto
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…