Je, inawezekana mfanyakazi bank akaomba mkopo Kwa kutumia taarifa za mteja?

Je, inawezekana mfanyakazi bank akaomba mkopo Kwa kutumia taarifa za mteja?

monde arabe

JF-Expert Member
Joined
Oct 22, 2017
Posts
8,781
Reaction score
13,444
Habar za Leo ndugu wanajukwaa,

Siku chache zilizopita nilienda kwenye tawi la bank Moja maarufu hapa nchini kwaajili ya ku-process mkopo kutoka kwenye bank hiyo.Afisa mikopo alinipigia mahesabu na ikaonekana kuwa naweza kupata kiasi cha zaidi ya milioni tisa za Kitanzania.Leo nikampigia cm Afisa yuleyule kuhitaji kiasi kilekile na kwa muda uleule (muda wa kurejesha mkopo)

Nilishangaa sana!!!! jamaa ananiambia kuwa naweza kupata kiasi cha shilingi milioni Moja na laki tatu tu (1,300,000/=) nikikopa kiasi kilekile,na nikirejesha Kwa muda uleule.Nikahisi kuwa huenda huyu mtu mwanzo nilipoenda wiki mbili zilizopita anaweza kuwa alikopa kwa kutumia taarifa zangu course anazifahamu hatakama sikumpatia mimi bado aweza kuwasiliana na Afisa utumishi na kuzipata.

Wenye elimu ya kutosha kuhusiana na masuala ya kibenki,mikopo,fedha na uchumi naombeni mnipe elimu ndugu yenu...kutoka kupata milioni tisa Hadi milioni moja na laki tatu siyo poa.Pia,nitawezaje kujua kama alikopa kwa kutumia taarifa zangu?

Na ikitokea nimejua kuwa huyu Afisa mikopo alikopa kwa kutumia taarifa zangu je,nifuatilie kwa kutumia utaratibu gani?

Naomba kuwasilisha!
 
Kuna jamaa kwa Sasa atakuwa na miaka 35 ya kuzaliwa. Yupo bank moja Dar es Salaam. Hata miaka mitano hajafikisha. Jamaa ana nyumba nyingi aisee..

Hostel na frame za biashara Kigamboni. Nyumba kwa ajili ya apartment. Jamaa hana cheo wala nini. Kazini alikuwa anaenda na baiskeli na alikuwa amepanga room mbili. Ila kwasasa kajenga kwake.

Jamaa ni mbahili,mademu akiishi nao wanamkimbia . Kitu Cha anasa kwake kumuonya nacho ni maji ya kunywa ya chupa. Zaidi ya hapo Hapana.

Mademu walikuwa wanachambua dagaa kilasiku. Halafu yeye anajenga katikati ya mji sio site. Ananunua nyumba ya mtu anajenga
 
Kuna jamaa kwa Sasa atakuwa na miaka 35 ya kuzaliwa. Yupo bank moja Dar es Salaam. Hata miaka mitano hajafikisha. Jamaa ana nyumba nyingi aisee..... Hostel na frame za biashara Kigamboni. Nyumba kwa ajili ya apartment. Jamaa hana cheo wala nini. Kazini alikuwa anaenda na baiskeli na alikuwa amepanga room mbili. Ila kwasasa kajenga kwake. Jamaa ni mbahili,mademu akiishi nao wanamkimbia . Kitu Cha anasa kwake kumuonya nacho ni maji ya kunywa ya chupa. Zaidi ya hapo Hapana . Mademu walikuwa wanachambua dagaa kilasiku. Halafu yeye anajenga katikati ya mji sio site. Ananunua nyumba ya mtu anajenga
Inawezekana kwa mfumo wa maisha yake. Maana watu wa benki huwa na mikopo mizuri kwa wale wanaojua kuwekeza ni rahisi kufanikiwa sana.
 
Kuna jamaa kwa Sasa atakuwa na miaka 35 ya kuzaliwa. Yupo bank moja Dar es Salaam. Hata miaka mitano hajafikisha. Jamaa ana nyumba nyingi aisee..

Hostel na frame za biashara Kigamboni. Nyumba kwa ajili ya apartment. Jamaa hana cheo wala nini. Kazini alikuwa anaenda na baiskeli na alikuwa amepanga room mbili. Ila kwasasa kajenga kwake.

Jamaa ni mbahili,mademu akiishi nao wanamkimbia . Kitu Cha anasa kwake kumuonya nacho ni maji ya kunywa ya chupa. Zaidi ya hapo Hapana.

Mademu walikuwa wanachambua dagaa kilasiku. Halafu yeye anajenga katikati ya mji sio site. Ananunua nyumba ya mtu anajenga
Sasa hii inahusianaje na thread ya jamaa?
 
Back
Top Bottom