Je, ipi ni nafasi ya dalali kwenye upangishaji wa nyumba?

Je, ipi ni nafasi ya dalali kwenye upangishaji wa nyumba?

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Joined
Aug 7, 2018
Posts
685
Reaction score
1,124
0001-15298689639_20210108_155937_0000.png

Upangishaji wa nyumba au chumba unaendeshwa na Sheria ya Ardhi ya mwaka 1999 , ambapo sheria hiyo imetaja wahusika wawili tu katika upangishaji.

Wahusika hao ni mpangaji na mpangishaji, sheria hii haijataja nafasi ya dalali, hivyo dalali anakuwepo kwa makubaliano kati ya mpangishaji au mpangishwaji.

Kwakua dalali yupo kimakubaliano ya mmoja wapo kati ya wahusika wawili, makubaliano hayo yataendeshwa na sheria ya mikataba.

Hivyo kwenye sheria hiyo dalali anatambulika kama wakala.

Ambapo wakala ni mtu aliyeajiriwa kufanya kitu chochote kwa niaba ya
mwingine, au kumuwakilisha mtu mwingine katika shughuli mbalimbali.

Mtu ambaye anafanyiwa shughuli hizo au anayewakilishwa anaitwa "mhusika mkuu".
 
Upvote 1
Siko busy kiivo mpaka nianze kutafuta dalali nawakati naweza kuzunguka nusu saa napata chumba
 
serikali ilishakemea suala la madalali lakini hakuna hatua inayochukua na jamaa wanazunguka tu mtaani bila kulipa kodi.
 
Dalali ni nani?
Watu wengi katika kupata ardhi zao au nyumba za kupangisha wametumia watu wanaoitwa madalali. Tunafahamu kwa uchache juu ya shughuli zao wanazofanya kila siku.
Dalali ni mtu yeyote au taasisi inayofanya kazi ya uwakala ili kufanikisha biashara baina ya mteja na mtoa huduma fulani. Dalali ni mtu wa kati anayewaunganisha mteja na mwenye mali kwa kupata ujira unaotokana na kuwakutanisha pande mbili.
Nafasi ya Udalali
Ni kweli kwamba kwa sasa shughuli nyingi na biashara nyingi zinafanikishwa na uwepo wa madalali. Madalali wamekuwa kiungo kikubwa cha kufanikisha biashara na huduma mbali mbali sehemu za mjini na hata maeneo ya vijijini. Hali ya biashara ya kukutana mteja na mwenye mali imekuwa tofauti, matumizi ya madalali yamekuwa makubwa na yanaongezeka kila kukicha.
Katika sekta ya ardhi yaani ununuzi na ukodishaji wa nyumba, madalali wamekuwa kiungo muhimu katika kuwakutanisha wahitaji wa ardhi na nyumba pamoja na wamiliki na kufanikisha biashara au huduma.
Nisisitize kuwa kazi hii ya udalali ni nzuri pia ina tija kwenye jamii lakini wahusika wanapaswa kuifanya kwa kufuata misingi ya kazi ili jamii ikubali na kutofautisha kati ya udalali na utapeli.@Kitomai
 
Madalali sio wafanikishaji tu bali ni complicators wa biashara. Essence yao ni maslahi binafsi wala sio kufanikisha biashara na wana overcharge sana.
 
Too general kusema wana overcharge sana.
 
Madalali wamerahisisha maisha ya watu wengi. Wamesaidia kuokoa muda na gharama kwa wengi wanaotafuta viwanja na nyumba za kupanga au kununua. Pia, kwa upande wa wamiliki wa nyumba na viwanja hivi, madalali wamekuwa daraja muhimu la kuwafikia wateja.
 
Biashara ya udalali inahitaji uvumilivu mkubwa, hasa kwa madalali wapya wanaofanya kazi miongoni mwa madalali wenye uzoefu mkubwa wa kazi. Ili kuwa katika njia sahihi, dalali mpya lazima atambue na kuzitumia vyema fursa mpya zinazojitokea.

Dalali mpya azungumze na madalali wenye idadi kubwa ya nyumba au viwanja vya kuuza au kukodisha. Pia, kumbuka fursa kama haijitokezi basi inabidi zitafutwe kwa namna yeyote ile. Ukipata wateja, hakikisha unakuwa na wakati wa makubaliano ili ujifunze na kuonesha nia ya kufanya kazi kama dalali. Madalali wenye uzoefu wakikuamini kuwa unaweza kuwaletea wateja, basi itakuwa rahisi kukutafuta wakiwa na nyumba au kiwanja kingine. Na huo ndio utakuwa mwanzo wako mzuri.@Kitomai
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom