Je, Israel ni Taifa la Mungu?

Je, Israel ni Taifa la Mungu?

Just Distinctions

JF-Expert Member
Joined
May 5, 2016
Posts
3,230
Reaction score
6,742
Niliwahi kuhudhuria ibada ambayo mchungaji Peter John wa Kanisa la Waadventista Wasabato alihubiri na kufundisha kuhusu Taifa la Mungu ndio nikaelewa vyema kuhusu suala la Israel

(nitajitahidi kutafuta lile hubiri kwenye youtube natumai itatusaidia wengi kwani tangu baada ya hapo uelewa wangu umekuwa tofauti sana kuhusu Israel)

Kwa kifupi alihubiri hivi (mtaniwia radhi ikiwa ntaiwasilisha isivyo maana nilisikiliza tu sikunukuu popote)

Mungu aliiumba hii dunia akiwa na lengo maalum na hutumia watu kwa ajili ya kutimiza kusudi lake la kuiumba dunia hii, (hapa alinukuu Mwanzo na vifungu vile vya binadamu kuijaza dunia na kutawala vilivyomo)

Hivyo huchagua mtu maalum kwa ajili ya kutimiza kusudi lake na kuwafikishia ujumbe wake kwa watu wote ili lengo lake litimie (manabii, mitume etc.)

Yoyote anaechaguliwa na Mungu sio kwamba yeye ni bora sana kuliko wengine bali hutumika kama chombo ili kufikisha kusudi kwa watu na akatoa mfano wa bomba akasema sio bomba ndio linalokata kiu bali ni maji yanayopita ndani yake

Unaweza kutandaza bomba kuanzia Dar mpaka Songea lakini isiwe na faida yoyote ikiwa hayatapita maji ndani yake

Hivyo wana Israel ni kama Bomba ambalo lilichaguliwa na Mungu ili kupitisha hayo maji ya uzima ili habari imfikie kila mtu hatimae wote wapate kuokolewa na ndio ahadi ya Mungu kwa Abrahamu Baba wa Taifa la Israel kuwa atamfanya Taifa Kubwa na kila ataembariki atambariki na kila atakayemlaani atalaaniwa na kupitia yeye mataifa yote watabarikiwa

Kitu bora sio watu wa Waisrael ila ni ule ujumbe ambao Mungu aliupitisha kwa wana Israel ili uwafikie wote Ulimwenguni

Wao wanachokosea (sio wote) ni kujiamini kuwa wao ni bora sana kuliko wote na kusahau ujumbe ambao walipewa ndio jambo la msingi zaidi, na kuwa lengo la Mungu ni yeye atukuzwe na sio binadamu hivyo kwa chochote chema sifa, shukrani na utukufu ni vyake daima

Je ukichaguliwa halafu ukawa unakosea utabaki hivyo hivyo? Hapana ni lazima uendelee kutii maagizo ya Mungu ili kuwa mchaguliwa, na ndio maana hata Yuda alichaguliwa kuifanya kazi ya Mungu ila baada ya kuasi kibali kiliondolewa nafsini mwake

Hivyo kuwa mkristo au mtu mwengine yoyote yule hakukusaidii kitu ikiwa hufati maagizo ya Mungu ya kumtukuza na kumkiri kuwa yeye ndio muweza wa yote na ndio kaiumba dunia hii, kuyafata mapenzi yake yote, kutotegemea miungu mingine, kupendana etc.

Hiko ndio nilichopata ila natumai ukitafuta mafundisho mbalimbali kwenye mtandao kuhusu suala la Israel utakutana na wachungaji au wahubiri ambao wamefafanua zaidi na utaelewa msingi wa imani ya wakristo wengi juu ya Israel kuwa Taifa la Mungu
 
Huwa najiuliza sana Mungu aliumba dunia tu? sayari zingine je? na je kama aliumba ulimwengu na dunia ikiwamo ndani yake, alitumia muda gani? tunaambiwa kwamba kuumba/kutengeneza dunia alitumia siku saba, vipi Jupita alitumia siku ngapi?

Neptune je? kwa maana binadamu hata huko wapo, japo haizungumziwi, na wapo wanaoenda huko na kurudi, na wapo wanaoishi huko, najua hapa kuna watu watapinga lakini huo ndio ukweli, binadamu huko wapo na mchanganyiko na viumbe wengine kama ilivyo hapa Duniani, kwanini dini hailizungumzii hili? je haikujua kwamba Binadamu yupo sayari zote?

Ama walifanya kusudi tu kukausha. na hili la Taifa linaloitwa Israel pia ni utata tu, sidhani kama wana u special huo mbele za Mungu maana kuna mi vitu huko kati ina akili na teknolojia kubwa kuliko hao jamaa..naamini humu wapo pia waotoka nje ya Sayari Dunia na kurudi, waje watupe shuhuda japo kidogo, nna uhakika humu wapo kwa 100% labda wanaamua kukausha tu kwa sababu zao binafsi, lakini suala la dini kuzungumzia, Mungu, Dunia na waisrael pekeyao kuna shida mahali.
 
Huwa najiuliza sana Mungu aliumba dunia tu? sayari zingine je? na je kama aliumba ulimwengu na dunia ikiwamo ndani yake, alitumia muda gani? tunaambiwa kwamba kuumba/kutengeneza dunia alitumia siku saba, vipi Jupita alitumia siku ngapi?

Neptune je? kwa maana binadamu hata huko wapo, japo haizungumziwi, na wapo wanaoenda huko na kurudi, na wapo wanaoishi huko, najua hapa kuna watu watapinga lakini huo ndio ukweli, binadamu huko wapo na mchanganyiko na viumbe wengine kama ilivyo hapa Duniani, kwanini dini hailizungumzii hili? je haikujua kwamba Binadamu yupo sayari zote?

Ama walifanya kusudi tu kukausha. na hili la Taifa linaloitwa Israel pia ni utata tu, sidhani kama wana u special huo mbele za Mungu maana kuna mi vitu huko kati ina akili na teknolojia kubwa kuliko hao jamaa..naamini humu wapo pia waotoka nje ya Sayari Dunia na kurudi, waje watupe shuhuda japo kidogo, nna uhakika humu wapo kwa 100% labda wanaamua kukausha tu kwa sababu zao binafsi, lakini suala la dini kuzungumzia, Mungu, Dunia na waisrael pekeyao kuna shida mahali.
Kwa mujibu wa Biblia aliumba Dunia na kula kilichomo kwa siku sita pekee, ya saba hakuumba chochote

Baadae ndio akaja kumuumba mwanadamu ili atawale vilivyomo

Kuhusu binadamu kuishi huko kwingineko na kuumba sayari zinginezo sina hakika kuhusu hilo

Mara zote nazobahatika kuangalia video mbalimbali za sayari nyingine sijaona fununu za kuishi watu huko lada dalili za kusupport uhai kama uwepo wa maji na vinginevyo

All in all, hii nimeileta kwenye anga ya kidini na imani zaidi ila kisayansi itabidi nifanye utafiti zaidi kuhusu waisrael na wengineo
 
Back
Top Bottom