Je itakuwaje akija kudai mtoto baadae?

Strong

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2013
Posts
515
Reaction score
454
Wapendwa habari ya weekend naombeni msaada wenu kuna mwanaume amezaa mtoto na mwanamke bila kua katika ndoa halali wakiwa wanaishi pamoja na hakutoa mahari pia wala hakuna ndoa kama nilivosema mtoto alipofikisha mwaka na miezi 7 walitengana baada ya mwanamke kuona amegeuka mlezi wa mtoto na mwanaume yaan mwanaume anadelay majukumu kwakua wote ni watumishi serikalini.

Sasa tokea mwanamke aamue kuondoka na kuishi mwenyewe baba wa mtoto hajawahi kutoa huduma yoyote na mama wa mtoto hajawahi kumwomba je huyu mwanaume atakapotaka mtoto wake itakuwa vp au nini kifanyike?
 
Hili ni suala la kisheria hivyo naomba wana sheria humu JF mumsaidie huyu Mama ili ajue haki yake
 
Yan mwanaume akatae kulea mtoto alafu baadae aje kumdai yan mim cjui ntamfanyaje yan kwanza asahau tu kama anamtoto coz hatakaa ampate
 
Mtoto; kibaiolojia atabaki kuwa na Baba mmoja, Mama mmoja.

Kimazingira, anaweza pata Wazazi walezi kwa kadiri ya mazingira atakayokutana nayo/yaliyomzunguka. Huyo baba, amlee au la, ni jukumu la mtoto kuja kuamua amuweke nafasi ipi Mzazi wake huyo atakapokuwA amefikia umri wa kung'amua mambo.

Si jukumu la mama kumtenganisha mtoto na baba, wala usijaribu kummezesha SUMU, inaweza kukugeukia siku za usoni au kumuharibu mtoto mazima.

Itategemea na malezi utakayompa sasa, malezu hayo ndio jibu la swali lako siku za usoni.

Mama, mlee mwana, ni mwana toka tumboni mwako.
 
Acha kukurupuka. Amueleze mtoto kila kitu. Maana MTT atakua
 
Yan mwanaume akatae kulea mtoto alafu baadae aje kumdai yan mim cjui ntamfanyaje yan kwanza asahau tu kama anamtoto coz hatakaa ampate

Tuko jukwaa la sheria...sio la mahusiano
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…